Askofu KKKT: Rais Samia aitwe Mama wa Taifa

Askofu KKKT: Rais Samia aitwe Mama wa Taifa

Nimeona hii katika vyombo vya habari! Bila aibu mtumishi wa Mungu akisimama na kushauri aitwe Mama wa Taifa na watu waliovaa nguo za kijani wakashangilia sana akiwamo Mwigulu Nchemba ambaye almanusura ajisahau na kupanda juu ya meza utadhani Stars imefunga goli!

Nauliza jee naye bila aibu amekubali ombi hilo la hovyo?

View attachment 2784102
Nauliza jee naye bila aibu amekubali ombi hilo la hovyo?[emoji23]
Ndio maana Mama Maria Nyerere akakataa ujinga ule wa juzi siku ya kumbukumbu ya kifo cha mumewe

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mwigulu ameamua kutumia hii Ziara kuiteka Nyara kwa kubagua hata baadhi ya madhehebu kwa sababu tu yanapinga UWEKEZAJI BANDARINI …, lakini ameenda mbali kufikia kutumia dhehebu lake kufikisha maatamanio yake ya kisiasa.
Nazan labda wanabadishana uchawa maana kipindi cha magufuli katolik walikuwa WA magu,kipindi kile kkkt wameandika waraka WA kupinga maovu ya magufuli ,katolik walimuunga mkona wakisema anapiga KAZI ,nakumbuka kkkt walipita kipindi kigumu Sana kiasi vyuo vyao vikataka kufungwa ,mabenki walilazimika kulipa mabilioni ya fedha kutetea Mali zao ,ilifikia mpaka kipindi magu alitaka kufunga kanisa lao akagundua kila kanisa linausajili wake labda Leo kanisa kama kkkt lisingekuepo.kipindiicho katolik wanatetea hata maovu ili wapate kibali Kwa raisi ivi unazani magufuli amekufa juz Tu unazan KKKT wamesahau?
 
Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Singida, Mchungaji Dkt. Cyprian Hilint amependekeza Rais Samia Suluhu Hassan aitwe ‘Mama wa Taifa’ kwa kuwa ndiye mwanamke wa kwanza Tanzania kushika nafasi ya Urais.

Kuwa Rais tu si kigezo pekee cha kupewa hadhi hiyo, hadhi ambayo kwa kawaida hupewa mtu aliyeasisi taifa...

Hata hivyo, matokeo yatayoonekana pindi mihula ya uongozi wake kumalizika ndiyo yatayoamua kama kweli anastahili au lah...
 
Nyerere ni baba kwa huyu mama. Umri wa huyu mama ni sawa na Umri wa Makongoro mbaye sijui ni mtoto wa tatu wa wa nne wa Nyerere. Kwa hiyo sasa mnataka Baba wa Taifa Nyerere awe na mwenza mwingine Mama wa Taifa. Dah! Labda tushauru tu kuwa tufute hiyo ya Baba wa Taifa kabisa na kuanzisha ya Mama wa Taifa tu halafu tuache historia ituhukumu huko mbeleni.
Mama wa Taifa ni hadhi ya Kiongozi sio swala la Kuwa Mke wa Rais wa kwanza.
 
Kuwa Rais tu si kigezo pekee cha kupewa hadhi hiyo, hadhi ambayo kwa kawaida hupewa mtu aliyeasisi taifa...

Hata hivyo, matokeo yatayoonekana pindi mihula ya uongozi wake kumalizika ndiyo yatayoamua kama kweli anastahili au lah...
Sio tuu ni Rais Bali Rais wa kwanza Mwanamke na ambae anaweza tofauti kubwa na watangulizi wake.

Samia amewafunika hao wote
20231016_210250.jpg
 
Amkaribishe katika Ukoo wake na amuite Mama wa Ukoo wake itatosha na itapendeza mno.

Mama wa Taifa la / wa Tanzania bado hajazaliwa na huenda hata asije Kuzaliwa.
Samia ndio mama wa Taifa,amemfunika yule mliyekuwa mnamuimba kutwa kucha eti baba wa pili wa Taifa 😂😂😂

Sasa hivi tushasahau mambo ya legacy uchwara za propaganda
 
Sio tuu ni Rais Bali Rais wa kwanza Mwanamke na ambae anaweza tofauti kubwa na watangulizi wake.

Huo Urais kaupata kwa neema tu, na kitu pekee anastahili kuitwa sasa ni Rais wa kwanza mwanamke (hii ni fact).

Yeye mwenye Mh. Samia Suluhu anajua hilo na ndio maana kwa busara aliyonayo humuoni kujifaragua mbele za watu na kunyanyua bega zake juu ya madaraka hayo makubwa ambayo kayapata kwa upendeleo.

Being addressed as Baba au Mama wa Taifa inakuja na legacy mtu aliyoweka au kuiacha na sio kuwa wa awali, Samia anafanya majukumu ya kirais kama Rais mwingine wa jinsia yeyote.

Mwl. Nyerere hakuitwa Baba wa Taifa kwa sababu alikuwa Rais wa kwanza bali alipew la hadhi hiyo kutokana na harakati zake juu ya kutafuta uhuru na kupata taifa Tanganyika na hatimaye Tamzania.

Baba au mama huzaa na ndio sababu huitwa majina hayo, Nyerere alizaa taifa tulilonalo sasa akaitwa Baba wa taifa.

Swali, je Mh. Samia kazaa taifa lipi hadi impase kuitwa mama wa taifa?
 

Hii nchi nilisema na ninasema tena, wasomi ndio wanaoongoza kwa kuwa wajinga. Kuna muda mtu anaongea, unajiuliza huyu hii PhD yake aliitoa wapi?
Wewe Cha maana ulichoongea ni kipi?
 
Huo Urais kaupata kwa neema tu, na kitu pekee anastahili kuitwa sasa ni Rais wa kwanza mwanamke (hii ni fact).

Yeye mwenye Mh. Samia Suluhu anajua hilo na ndio maana kwa busara aliyonayo humuoni kujifaragua mbele za watu na kunyanyua bega zake juu ya madaraka hayo makubwa ambayo kayapata kwa upendeleo.

Being addressed as Baba au Mama wa Taifa inakuja na legacy mtu aliyoweka au kuiacha na sio kuwa wa awali, Samia anafanya majukumu ya kirais kama Rais mwingine wa jinsia yeyote.

Mwl. Nyerere hakuitwa Baba wa Taifa kwa sababu alikuwa Rais wa kwanza bali alipew la hadhi hiyo kutokana na harakati zake juu ya kutafuta uhuru na kupata taifa Tanganyika na hatimaye Tamzania.

Baba au mama huzaa na ndio sababu huitwa majina hayo, Nyerere alizaa taifa tulilonalo sasa akaitwa Baba wa taifa.

Swali, je Mh. Samia kazaa taifa lipi hadi impase kuitwa mama wa taifa?
Wewe unaangalia impacts ya Urais wake Kwa jamii au unataka kujua kaupataje huo Urais?

Pili uchaguzi ujao atashinda so utaongea na blaa blaa ipi tena?

Mwisho wote ambao ni kina Baba wa Taifa ni Marais wa kwanza hakuna Rais wa pili au wa tatu ni baba wa Taifa hapa Duniani and so automatically Samia kuwa mwanamama wa kwanza Rais ana qualify.

Mwisho nimekwambia Samia is delivering kushinda wote waliotangukia Hadi dakika hii na wewe unajua ila chuki binafsi zinakusumbua tuu.
 
Hizi dini ni Taasisi za wenye akili kuwavuna wajinga.
Miaka na miaka haijawahi kutokea nabii (mtumishi wa Mungu) kumtukuza mfalme au malkia ila hapa Tanzania ujinga huu ulianza kipindi cha Jiwe
 
Huyo askofu yeye na familia yake wakimuita mama wa taifa inatosha kabisa.
Uchawa kila eneo...
 
Askofu Mkuu wa KKKT Dayosis ya Singida Dk.Cyprian Hilint (PhD) amependekeza kwamba Rais Samia Aitwe Mama Wa Taifa.


My Take
Naunga mkono hoja, Samia anastahili hadhi hii.

Kama nawaona Machadema,TEC na Sukuma gang walivyojaa Chuki.

=====
Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Singida, Mchungaji Dkt. Cyprian Hilint amependekeza Rais Samia Suluhu Hassan aitwe ‘Mama wa Taifa’ kwa kuwa ndiye mwanamke wa kwanza Tanzania kushika nafasi ya Urais.

Pia soma: Mwita Waitara: Rais Samia aitwe Mama wa Taifa
Uyu askofu wenda amejikuta ni askofu, ila haelewi kwa nini yuko pale, huwezi kuamka from no where na kubwabwaja maneno ya namna hii, kama Askofu ambaye jamii kwanza inakueshimu kama mtumishi wa Mungu na pia inaamini kwamba uwezo wako wa kufikili upo juu kisomi , kifikra n.k

Kwanza pamoja na kwamba mama wa taifa Mama Nyerere yupo, na haitakuja tokea mama wa taifa mwingine kama ambavyo haitakuja tokea Baba wa Taifa mwingine ilo lijulikane lakini hata iyo nafasi ingekuepo

Uyu SSH haitwe mama wa taifa kwa vigezo vipi,? Kwamba kisa kuwa rais mwanamke wa kwanza kuwa makam na kuwa Rais baada ya kifo cha mwendazake ? Huu utakua ni ushamba , kwani ni tz tu Afrika,na Dunia kuwa na Rais mwanamke au makam mwanamke ,

Kwamba kafanya makubwa kuliko watangulizi wake? Hii itakua ni kujizima data ,SSH amefanya yapi , hakuna kipya ni yale yale ambayo watangulizi wake walisha fanya ,sema mengine katika kipindi chake yamezidi ,mfano Rushwa, utendaji mbovu wa serikali yake, umaskini wa kutisha kwa wananchi n.k

Kwa machache hata iyo nafasi ingekuepo SSH hasingeweza kustahili, sasa hawa wapambe ni lazima kufanya hivyo kwa nalengo wajuayo wenyewe, mfano mtu kama Mchengelwa atashindwa sifia haiwezekani
 
Askofu, ameamua kumtenganisha Mwalimu Nyerere na Mama Maria?
 
Uyu askofu wenda amejikuta ni askofu, ila haelewi kwa nini yuko pale, huwezi kuamka from no where na kubwabwaja maneno ya namna hii, kama Askofu ambaye jamii kwanza inakueshimu kama mtumishi wa Mungu na pia inaamini kwamba uwezo wako wa kufikili upo juu kisomi , kifikra n.k

Kwanza pamoja na kwamba mama wa taifa Mama Nyerere yupo, na haitakuja tokea mama wa taifa mwingine kama ambavyo haitakuja tokea Baba wa Taifa mwingine ilo lijulikane lakini hata iyo nafasi ingekuepo

Uyu SSH haitwe mama wa taifa kwa vigezo vipi,? Kwamba kisa kuwa rais mwanamke wa kwanza kuwa makam na kuwa Rais baada ya kifo cha mwendazake ? Huu utakua ni ushamba , kwani ni tz tu Afrika,na Dunia kuwa na Rais mwanamke au makam mwanamke ,

Kwamba kafanya makubwa kuliko watangulizi wake? Hii itakua ni kujizima data ,SSH amefanya yapi , hakuna kipya ni yale yale ambayo watangulizi wake walisha fanya ,sema mengine katika kipindi chake yamezidi ,mfano Rushwa, utendaji mbovu wa serikali yake, umaskini wa kutisha kwa wananchi n.k

Kwa machache hata iyo nafasi ingekuepo SSH hasingeweza kustahili, sasa hawa wapambe ni lazima kufanya hivyo kwa nalengo wajuayo wenyewe, mfano mtu kama Mchengelwa atashindwa sifia haiwezekani
Kwa Tanzania ni WA kwanza,wewe mapovu ya nini? Ukiacha kuwa Rais wa kwanza Mwanamke ila sifa zingine ambazo wengine Wameshindwa ni
-Kuleta Mageuzi ya Kilimo
-Mageuzi makubwa ya uchumi hasa viwanda
-Mageuzi makubwa ya uwekezaji na Biashara
-Mapinduzi kwenye sekta za jamii kama.maji,Elimu,Afya
-Demokrasia na Haki za binadamu
-Miundombinu ya uchumi
 
Kwamba hujui, waulize wakina Mseveni,kagame n.k ndo utajua ni mchango gani amekua nao katika taifa ,kama mama na mke wa alie kua baba wa taifa
Hao uliowataja ndio Watanzania? Nakuuliza wewe Mama Maria ni mama Yako Kwa mchango gani aliotoa Kwa Taifa hili? Taja mbona Mimi nakutajia mchango wa Samia?
 
Back
Top Bottom