Ukiwa kwenye madaraka, wapambe, ambao wengi ni waongo na wachumia tumboni, wanatabia ya kukuaminisha una nguvu za kufanya lolote unalotaka.
Chonde chonde Rais wangu, usije kuingizwa chaka...acha muda uamue. Hawa wanaokuimbia hizi sifa leo, wakati kuna mengi yana changamoto, wengi ni sababu wananeemeka. Isije kuja kesho wakakengeuka.
JPM aliambiwa utake usitake uendelee kuongoza....Mzee Mwinyi enzi zile walimwambia tunataka usitoke, uendelee kuongoza maana umahiri wako haujawahi kuonekana.
Ila haikuwa hivyo. Mipango na maarifa ya Mwenyezi Mungu inazidi ya wanadamu. Tuombe hekima ya Mwenyezi Mungu itutangulie katika yote. Uganga wa ramli na matambiko hayana majawabu kwenye haya mambo ya msingi ya maisha
View: https://www.youtube.com/watch?v=4VJ0x4a6LKI