#COVID19 Askofu Gwajima: Wapo waliochanjwa chanjo feki ili kuwashawishi watu wachanjwe. Sijachanjwa na haitatokea

Kwa nini anaposema gwajima kuhusu madhara ya chanjo iwe anapotosha na so freedom of speech
Hakuna Chanjo ambayo ni effective kwa asilimia mia moja, ila kuzihusisha Chanjo na Mnyama 666 pamoja na mitandao ya Simu ya 5G bila bila ya ushahidi wowote ni upotoshaji
 
Tukichanjwa wote Hatutaambukizwa ? ... Hapana bado unaweza Ambukizwa
Nikichanjwa Je niache kuvaa Mask?.. Unavaa Mask
Nikichanja naweza kuendelea na maisha ya kawaida?... Hapana
Nikichanjwa sitaambukizwa?.. Unaweza ambukizwa

Sasa kuchanja kunanisaidia Nini?.. Nyie mnakazania tu Chanjo hazina madhara ni Salama.


1. Tukichanjwa zaidi ya asilimia 80 tutakuwa na herd immunity ambapo maambukizi yatapungua sana na mwisho kuisha kabisa. Kama ilivyokuwa kwa ndui.
2. Unatakiwa kuvaa mask kwa sababu kuna wengi ambao wanaweza kukuambukiza. Tukumbuke chanjo haizuii kwa asilimia 100. Umezekano wa kuambukizwa upo lakini si mkubwa kama ulivyo kwa wasiochanjwa. Sasa hivi 99 % ya maambukizi mapya ni katika wale wasiochanjwa. Idadi ya wasiochanjwa inapokuwa kubwa ndio uwezekano wa kuambukizwa unavyozidi.
3. Natumaini unaposema maisha ya kawaida ni yale ya kutovaa mask? Kama ni hayo, utaweza pale idadi ya waliochanjwa wakiwa wengi.
4. Unaweza kuambukizwa Kama nilivyosema hapo juu. Lakini hata ukiambukizwa hautaathirika sana kama wale ambao hawajachanjwa. Hautahitaji oksijen au ventileta.

Ni ubinafsi uliokithiri kupima ubora wa kitu kwa namna unavyofaidikq wewe binafsi tu. Umuhimu wa chanjo sio tu kwa mtu binafsi bali pia kwa wale ambao hautawaambukiza.

Majibu haya ni kwa mbunge wa Kawe. Bado hatujasahau meli zetu za uvuvi na ambulance kila tarafa.

Amandla...
 
Character ya true prophet ni pamoja na kusimamia unachoamini ni sahihi hata kwa gharama ya maisha yako... Wale wengine wanacheza mziki kadiri ya mdundo wa bi mkubwa.
We huna aibu kumuita huyu tapeli "tru prophet ".
Alidai anafufua wafu hali ya kuwa mama yake mzazi kafa na yeye katoa macho tu.
Amerekodiwa anamtafuna kondoo dakika 1 bila aibu. Anaishi kwa udanganyifu na kila mtu anaona we unamuita "true prophet "!?
Kweli nchi imejaa utopolo
 
Tunasimama na baba askofu.
Huyu tapeli anatakiwa AKAMATWE NA TCRA akajibu mashtaka ya kupotosha ummah.
TCRA isipomkamata GWAJIMA isije kuonea wananchi wengine wanaoropoka ovyo.
Huyu mtu hana adabu kabisa na sheria za nchi hii.
Adanganya watu na serikali inamtazama tu.
Sheria lzm ifuatwe hapa. Au hatutoelewa kabisa nini kazi ya TCRA
 
Itasaidia ndani ya chama chetu.....

Atabaki nje aendeleze misimamo yake.....

Tumeshafukuza wengi tu huko nyuma ilitusaidia.,. ..

#CCMImfukuzeGwajima
#KaziIendelee
Kama nia ni kumtenga na chama, na siyo kudhibiti madhara ya kauli zake, upo sawa mkuu.
 
Sasa kwa kuwa mna mwamko mkubwa wa kukwepa chanjo ili mabeberu wasiwaue basi serikali inaweza kuingia mkataba na hao mabeberu na kuzihadilisha chanjo na kunyunyuzia hizo sumu kwenye maji mnayokunywa, kuoga, mikate, nyama na vyakula mbali mbali mnavyotumia kila siku...kufa kupo tu ! 🐒
 
Yeye keshachagua fungu lake la kutokuchanjwa aache kushawishi watu wengine wasichanjwe. Kila mtu abebe msalaba wake mwenyewe.
Ana uhuru wa kuzungumza!! Ana dhamana mbele ya Mungu kwa washirika wake!! Waambie na wanaoshawishi watu kuchanjwa waache!! Usizuie upande mmoja kuzungumza! Aidha wazungumze wote au waache wote kuzungumza!!
 
Nimepona covid-19 delta variant niliyougua zaid ya wiki, shida niliyobaki nayo hata harufu kali ya kitunguu swaumu pua haziinusi, pilau nakula tu harufu hakuna....nimegoogle kumbe hii shida naweza kuwa kilema jumla (10%) au nitapona ndani ya hadi siku 90 (90%)

Wakuu achaneni na ujinga wa hawa wazungu....pigeni nyungu na covido ya NIMRI baasi! Chanjo muachieni Dorothy tu! Naandika haya sio kama Ndebile tu, bali pia mtu mwenye ujuzi wa kuhudumia wagonjwa kwa kutumia elimu yao hao watu magharibi!
 
Sasa ARV wanywaji wamezihakikisha??

Hizo chanjo zingine kina mama wanaopeleka watoto clinic wamezihakikisha??

Yellow fever, hepatitis e.t.c vaccination??

Dawa na madrip na masindano wagonjwa wanazihakikisha??

Je, zile dawa za kina dada za kuzuia mimba, kitanzi, vijiti, sijui vidonge, nani kavihakikisha??

Kumekuwa na hype, madaktari na wataalam wa VIRUS, hawasikilizwi, ila waliodandia fani, wanatafuta political mileage na followers kwa kasi ya upotoshaji ya ajabu.

Everyday is Saturday............................... :cool:
Acha umbumbumbu!! Madaktari bingwa ambao hawajapewa kitu kidogo ndio wanaotoa taarifa sahihi za chanjo hii yenye utata. Huyu hapa daktari bingwa na anakumwagia CV yake kwanza halafu anakumwagia nondo za kueleweka kuhusu chanjo ya corona. Msikilize huyu hapa, kama huijui lugha ya malkia tafuta mtu mkalimani! Linganisha CV ya huyu na ya huyu wa kwetu aliyepata chanjo ya placebo/feki na kujifanya yuko fiti na kujikimbiza mchakamchaka!
 
Hii ni fujo gani? Chanjo na Sumakuumeme???? Jamani kila mtu aliyewahi kusikia neno la kigeni analimwaga....
Ujue wenzio walishaonngezeka Sana Kwa maarifa walikuwa kwenye biological weapons sasa wameenda mbele zaidi biological weapons wameadvance into electromagnetic electronic killings
 
Huyu tapeli anatakiwa AKAMATWE NA TCRA akajibu mashtaka ya kupotosha ummah.
TCRA isipomkamata GWAJIMA isije kuonea wananchi wengine wanaoropoka ovyo.
Huyu mtu hana adabu kabisa na sheria za nchi hii.
Adanganya watu na serikali inamtazama tu.
Sheria lzm ifuatwe hapa. Au hatutoelewa kabisa nini kazi ya TCRA
Wewe umejuaje kama anapotosha umma? Una evidence beyond doubts kuwa chanjo hii ni genuine?
 
Hakuna Chanjo ambayo ni effective kwa asilimia mia moja, ila kuzihusisha Chanjo na Mnyama 666 pamoja na mitandao ya Simu ya 5G bila bila ya ushahidi wowote ni upotoshaji
Mimi nilimsikiliza hapa.alikuwa na points ambazo hazijajibiwa mpaka leo.
 
Ana uhuru wa kuzungumza!! Ana dhamana mbele ya Mungu kwa washirika wake!! Waambie na wanaoshawishi watu kuchanjwa waache!! Usizuie upande mmoja kuzungumza! Aidha wazungumze wote au waache wote kuzungumza!!
Kwani mpaka adana years ndiyo aweze kushawishi hao wafuasi wake? Umesikia serikali ikilazimisha mtu yeyote kuchanjwa? Kama ana taarifa za ukweli kuhusu viongozi kuhongwa ili waipitishe chanjo kwa nini yeye kama kiongozi na mbunge asipeleke taarifa PCCB wafanye uchunguzi na kuchukua hatua stahiki?
 
Ni sawa pia... Kama aliamini yule dada ni mtamu ilibidi asimamie msimamo wake to the extent ya kumla.
Askofu anafanya hivyo...Tena ingia sexhubb andika askofu....utamuona anavyojatika...ebu mwambieni aongee na hao wenye mtandao watoe hiyo clip maana baba Yuko mnyaMA KABISA
 
Askofu anafanya hivyo...Tena ingia sexhubb andika askofu....utamuona anavyojatika...ebu mwambieni aongee na hao wenye mtandao watoe hiyo clip maana baba Yuko mnyaMA KABISA
Alijitahidi kupiga uno mbili tatu ila manzi ndiyo hakutoa ushirikiano, Chidi alikuwa anatoa miguno ya hatari. Ila pamoja na ufuska wake safari hii kawanyoosha maccm.
 
Back
Top Bottom