Askari Polisi waweka ulinzi mkali Kanisa la Ufufuo na Uzima lililopo Ubungo, Dar es Salaam

Heparin

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2021
Posts
440
Reaction score
3,211
Nimepita maeneo ya Ubungo nikiwa naelekea kwenye harakati zangu, naona Polisi wamejaa kanisani kwa Gwajima baada ya yeye kutangaza atashiriki ibada ya Jumapili ya leo.

Wengi wapo barabarani wanafunga utepe. Kwakuwa speed ya gari ilikuwa kubwa sijafanikiwa kuchukua picha ya haraka.

Pia sijafanikiwa kuona upande wa pili wa kanisa ili kubaini kama wapo pia au la.

===

Askari waliovalia sare za Jeshi la Polisi wameweka ulinzi mkali katika Kanisa la Glory of Christ Tanzania Church (Nyumba ya Ufufuo na Uzima), eneo la Ubungo Dar es salaam huku njia zote zinazowezesha Watu kufika kwenye kanisa hilo zikiwa zimezuiwa.

Ikumbukwe Juni 13, 2025, Naibu Katibu wa Kanisa la Glory of Christ Tanzania Church, Askofu Maximilian Machumu “Mwanamapinduzi” amesema taarifa kuwa Msajili wa Jumuiya za Kiraia, Emmanuel Kihampa amefungia Kanisa lao, si za kweli bali lililofungiwa ni Kanisa la Glory of Christ Church ambalo halina uhusiano na Kanisa lao, hivyo Jumapili hii wanatarajia kurejea Kanisani kuendelea na Ibada.

Baadhi ya waamini wamejitokeza maeneo ya karibu na Kanisa hilo lililopo Ubungo.

IMG_20250615_094410_194.jpg
IMG_20250615_094410_666.jpg
IMG_20250615_094410_402.jpg
IMG_20250615_094410_175.jpg


Polisi wafanya doria kwenye Kanisa la Gwajima kutawanya waamini wanaokusanyika
Pichani Mwanamke mmoja ambaye jina lake halijafahamika akilia baada ya kuzuiwa kuingia kwenye Kanisa la Glory of Christ Tanzania Church (Nyumba ya Ufufuo na Uzima) lililopo eneo la Ubungo.

Baadhi ya waamini wanazuiwa na kuambiwa kwamba hawaruhusiwi kukusanyika eneo la karibu na Kanisa hilo, ambapo askari Polisi wanafanya doria kuwatawanya waamini wanaokusanyika katika makundi.
photo_2025-06-15_11-04-00.jpg





Pia soma
 
Nimepita maeneo ya Ubungo nikiwa naelekea kwenye harakati zangu, naona Polisi wamejaa kanisani kwa Gwajima baada ya yeye kutangaza atashiriki ibada ya Jumapili ya leo.

Wengi wapo barabarani wanafunga utepe. Kwakuwa speed ya gari ilikuwa kubwa sijafanikiwa kuchukua picha ya haraka.

Pia sijafanikiwa kuona upande wa pili wa kanisa ili kubaini kama wapo pia au la.

Pia soma Askofu Gwajima kuongoza Ibada ya Jumapili Juni 15, itafanyika Jimbo Kuu Dar Saa 4 Asubuhi
Simbaya na wao police wakisali kwa Gwajima, uenda Kamanda Mulilo ndiye atasoma neno la Mungu. Alafu askari wengine wataimba kwaya.
 
Nimepita maeneo ya Ubungo nikiwa naelekea kwenye harakati zangu, naona Polisi wamejaa kanisani kwa Gwajima baada ya yeye kutangaza atashiriki ibada ya Jumapili ya leo.

Wengi wapo barabarani wanafunga utepe. Kwakuwa speed ya gari ilikuwa kubwa sijafanikiwa kuchukua picha ya haraka.

Pia sijafanikiwa kuona upande wa pili wa kanisa ili kubaini kama wapo pia au la.

Pia soma Askofu Gwajima kuongoza Ibada ya Jumapili Juni 15, itafanyika Jimbo Kuu Dar Saa 4 Asubuhi
Picha ya hao waumin tafadhali
 
Back
Top Bottom