Asili ya majina ya maeneo mkoani Manyara

Asili ya majina ya maeneo mkoani Manyara

TUnawachanganya watu in all spheres of life.Ndo hivo Mungu ametupendelea sana.💃🏻❤️🕺🏻🙏🙏
 
Hii nimeeileta baada ya kufikwa na mafuriko maeneo ya Hanang, katesh Manyara

Kwenye mitandao ya kijamii wengi kwenye comment wakisikia jina Hanang au katesh, wanauliza ni wapi wakidhani mafuriko yametokea china au Japan, kutokana na majina ya eneo husika, wengi hawajui kama ni Tanzania.

Nimejaribu kuangalia majina ya maeneo ya mkoa WA manyara kweli yanashangaza, ni tofauti kabisa na maeneo mengi Tanzania, yanafanana na majina ya nchi za nnje.

Pia nilitaka kujua mkoa WA Manyara mbona hautajwi kama ni mkubwa hapa nchini? Wakati ukiangalia ni mkubwa sana, ukiwa Hedaru Same, Kilimanjaro unaweza kwenda Simanjiro kiurahisi ni karibu sana, Ukiwa Arusha ndio pua na mdogo, ukiwa Singida napo ni jirani sana.

Baadhi ya majina ya maeneo ya mkoa WA Manyara:

*Hanang
*Gitting
*Katesh
*Maghang
*Loiborsoit
*Muslur
*Getanuwas
*Haydom
*Murkuchida
*Datlaa
*Bargish
*Kainam
*Terat
*Waang'waray
*Orkesumet
*Hoshan
*Dareda
*Dongobesh

Na mengine mengi.

NB: kule Kuna watu wanaitwa wa Iraq na wambulu wanawake wao ni pisi Kali balaa
Umepakana na mikoa ya tanga,arusha kilimanjaro,singida,dodoma
 
Dongobesh,

Hata lugha yao ngumu sana, pole kwa janga lililowapata kila nikivuta picha ya katesh mlima hanang nasisimka na haya nayosoma humu ni km nakumbuka pote nilipopita katika harakati za kimaisha ni juzi tu nilikuwa huko laiti tungejua haya tungehamisha watu wote, ila yote kwa yote wapumzike mahali pema,😭😭😭
Karibu nikufundishe kipolpole lugha yetu.
 
Sindikiza na picha tafadhali.
Hizo ziko bongo movie
20231205_184148.jpeg
20231205_184135.jpeg
 
Majina ya maeneo wanapo toka Wairaqw

Wilaya ya Mbulu

Ayamaami | Ayamohe | Bargish | Bashay | Dongobesh | Endagikot | Endamilay | Eshkesh | Gehandu | Geterer | Gidihim | Gunyoda | Hayderer | Haydom | Imboru | Kainam | Maghang | Marang | Maretadu | Masieda| Masqaroda | Murray (Mbulu) | Nahasey| Nambisi | Sanu Baray | Tlawi | Tumati | Yaeda Ampa | Yaeda Chini


Wilaya ya Hanang
Balangdalalu | Bassodesh | Bassotu | Dirima | Endasaki | Endasiwold | Ganana| Gehandu | Gendabi | Getanuwas | Gidahababieg | Gisambalang | Gitting | Hidet | Hirbadaw | Katesh | Laghanga | Lalaji | Masakta | Masqaroda | Measkron| Mogitu | Nangwa | Simbay | Sirop

Wilaya ya Karatu
Baray | Buger | Daa | Endabash | Endamaghang | Endamarariek | Ganako | Kansay | Karatu | Mang'ola | Mbulumbulu| Oldeani | Qurus |
Rhotia

Wilaya ya Babati

Arri | Ayasanda | Baoy | Bashnet | Dabil | Dareda | Duru | Endakiso | Gallapo | Gidas | Kiru | Madunga | Magara | Magugu | Mamire | Mwada | Nar | Nkaiti | Qash | Riroda | Ufana


Wairaqw ndio jamii ya watu waaminifu sana Tanzania na kuhusu urembo au sura zao hawa ni Waethiopia au Wasomali wa Tanzania kwa asili, ni karne kama 5 zilizopita ndio asili yao ilitoka huko, hata na majina na sura zao ni Ethiopia na Somali, ni warembo sana na katika kazi za kuajiriwa au biashara au serikalini ukimpata mwiraqw basi ni waaminifu sana, kweli atasema kweli, uongo atasema hii ni uongo, pia wapole ila majasiri sana sana..

Wanawake wa Kiiraqw ni warembo sana sana naturally na wanaume ma handsome kwelikweli, kama waethiopia au halfcast wa kiarabu. I love my home land Arusha & Manyara.
Hata sumaye Frederick ni muaminifu?
 
Wazawa wa Arusha na manyara si wabantu; wairaqw(wambulu), wamaasai, wahadzabe, wote sio wabantu, lugha zao ni za tofauti sana ndo maana unaona wana maneno ya ajabu

Wameru tu ndo wabantu
Uko sawa 100%, watu uwa wanasema eti watutsi ni nilotic wakati ni wabantu tu. hawa uliowataja ndo wanilotic haswaa kutokana na lugha yao na muonekano wao.
 
mkuu nadhani haiitwi Hanang, inaitwa Hanang’
Pia Hanang’ na huko Katesh hawakai Wairaq/Wambulu. Huko wanakaa Wabarbaig.
Wambulu wanaishia ishia hapo Dareda Centre na kidogo hapo Gitting ukija huku Endasak, Nangwa, Gidababia nk wengi ni Wabarbaig
Qatesh, Gidahababieg
 
Back
Top Bottom