issue za magendo zina pesa ndefu unatoka kimaisha dk zero tu.Sana angetoboa hapo siyo mwenzetu ndio maana utajiri una siri nzito sana hao wapo 20 kila kichwa minimum usd 2000 maana yake alikuwa anapiga 100m kama amesimama
sheria zinawabana.Kwani angewaacha waende zao huko South Africa angepungukiwa nini?
Sheria gani nchi hii, roho mbaya tu. Wao wanaenda kwingine shida tunapata sisi?sheria zinawabana.
ila kuna mmoja raia wa Ethiopia anasema wanandugu zao Europe&U.S,ndugu zao kuwafanyia mpango wa kwenda huko ulaya kwa kutokea south Africa ni rahisi sana kuliko kuwafanyia mpango wakiwa Ethiopia au Erytria ni ngumu zaidi ya ngumu.
Hahaha hii imeendaHapo angewavesha tisheti na kofia, ukiulizwa unawaambia wajumbe wametoka Hanang
Pesa hzo huwa wanazitoa wapi maana Ni pesa ndefu Sana wanatumiaaa kufika S AKweli mkuu ajali kazini
Hao vijana nawaona sana tena unaona kabisa ni fresh wanavyozubaa zubaa
Wakifanikiwa wao mwisho wa safari ni Ulaya
Ila wakishikwa wanarudishwa halafu wanaanza upya tena
Ni majaaliwa kufika ila wapo wanaofika huku na kuwasaidia wenzao waje pia
Jamaa sio kachomwa ila kabeba wengi sana lakini pia kwa waswahili linawezekana
Na inakuwa mzigo Sana kuwa hifadhi kwa gharam zetu piaSheria gani nchi hii, roho mbaya tu. Wao wanaenda kwingine shida tunapata sisi?
Hata Meli za Iran walitumia flag yetuMnasemaga ukiwa CCM kila kitu ni bwerere sasa imekuwaje huko na bendera juu?.
Mchawi wa taifa letu ni CCM wala hakunaga mwingine.Mtanzania Edward Erihard (31) Mkazi wa Dodoma anashikiliwa na Polisi Mkoani Manyara kwa kosa la kusafirisha kinyume na sheria Wahamiaji 20 Raia wa Ethiopia.
Akiongea na AyoTV Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoani Manyara ACP Lucas Mwakatundu amesema tukio hilo limetokea March 23 2024 ambapo gari hilo limekamatwa katika kizuizi barabara ya Arusha Babati eneo la Minjingu likiwa na Wahamiaji ishirini Raia wa Ethiopia kwenye gari namba T.774 BDL Land Cruiser likiwa na bendera ya Chama cha Mapinduzi CCM.
“Gari hili V8 lilikuwa na Bendera ya Chama cha Mapinduzi (CCM) na kwenye upekuzi tulipoona sura tofauti na Watanzania ilibidi tuweke gari pembeni na baadae kuwashusha tukakuta wapo Wahamiaji 20 kwenye gari V8 na wote uelekeo wao ni kusini mwa Afrika wakitokea usawa wa Arusha, Dereva wa gari hili ni Mkazi wa Dodoma tunamshikilia mpaka sasa na kesho tunatarajia kuwakabidhi Uhamiaji” ——— kaimu RPC Manyara. #MillardAyoUPDATES
View attachment 2943836
Kakosea, hapo jumla haizidi dola elfu 5 japo nazo ni nyingi tuUna uhakika hujakosea lkn
Gari halijapakwa rangi ya kijani, yeye hajavaa magwanda ya kijani, wahamiaji hawajavaa nguo za kijani, ana akili fupi.Mtanzania Edward Erihard (31) Mkazi wa Dodoma anashikiliwa na Polisi Mkoani Manyara kwa kosa la kusafirisha kinyume na sheria Wahamiaji 20 Raia wa Ethiopia.
Akiongea Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoani Manyara ACP Lucas Mwakatundu amesema tukio hilo limetokea March 23 2024 ambapo gari hilo limekamatwa katika kizuizi barabara ya Arusha Babati eneo la Minjingu likiwa na Wahamiaji ishirini Raia wa Ethiopia kwenye gari namba T.774 BDL Land Cruiser likiwa na bendera ya Chama cha Mapinduzi CCM.
“Gari hili V8 lilikuwa na Bendera ya Chama cha Mapinduzi (CCM) na kwenye upekuzi tulipoona sura tofauti na Watanzania ilibidi tuweke gari pembeni na baadae kuwashusha tukakuta wapo Wahamiaji 20 kwenye gari V8 na wote uelekeo wao ni kusini mwa Afrika wakitokea usawa wa Arusha, Dereva wa gari hili ni Mkazi wa Dodoma tunamshikilia mpaka sasa na kesho tunatarajia kuwakabidhi Uhamiaji”
Chanzo: Ayo TV
Huyo sio ccm kaweka bendera tu, ila siti ya mbele kungekuwa na mnene wa ccm wasingekamatwaMnasemaga ukiwa CCM kila kitu ni bwerere sasa imekuwaje huko na bendera juu?.
Huoni walivyojichanganya? Pale mbele alitakiwa aweke Watanzania. Sasa yeye anawaacha wanaonekana. Sura ndizo zimewaponza vinginevyo walikuwa wanatoboza!Mnasemaga ukiwa CCM kila kitu ni bwerere sasa imekuwaje huko na bendera juu?.
Duh! Hapo ni ku-cross Tz tu! Je, Kenya? Zambia? Zimbabwe? Botswan? Hadi kuingia SA how much do they pay? Kama wana ukwasi hivyo why wawe wahamiaji haramu? Kwanini wasifuate taratibu badala ya kuji-risk hivyo? Sielewi!Wauza Unga wengi wameacha hiyo biashara maana kifungo ni kirefu sana
Ila kuvusha wakimbizi ni
a slap on the wrist
Na inalipa kweli
Kuna wanaolipa safari moja mpaka $30,000