Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

United anaongoza. Goli limetokana na kona.

Nacheka kwamba hili ni goli la kona mfululizo kwa United na mashabiki wao hawalalamiki. Ni mashabiki wa Arsenal tu ndiyo watalalamika timu yao kupata ushindi kwa magoli ya kona.

We can criticise tactics na team selection lakini magoli siyo kitu cha kulalamika. United wana furaha isiyo kifani kumaliza ndani ya top four.

Liverpool wana furaha wapo nafasi ya nne.

Chelsea anabana pumbu angalau ashike nafasi ya 7.

Arsenal ipo nusu fainali CL dhidi ya Atletico na bado ana uwanja wa kupambania PL ila shabiki analalamika. Atletico kamtoa Barca, Atletico hajawahi kutolewa nusu fainali na timu ya kiingereza.

Shabiki wa Arsenal analalamika kwanini game iliisha moja moja.

It's weird
 
Kwa kumbukumbu zangu ni Will Jr ndiye alikua anasema Partey ni mbovu. Mimi badi nina imani na Zubimendi mchezaji ambaye ametakwa na timu zaidi ya nne sidhani kama ni kiazi kiasi hicho.

HUyu jamaa ni Busquet mwingine. Kichekesho ni kwamba zile through balls na penetration passes siyo kwamba hawezi ila ghafla tu amekua hazipigi, hizi ambazo Partey alikua hahofii kuzipiga.

Loose balls za nje ya 18 Partey alikua anazipiga nonstop ila Zubimendi hazipigi. Ni kweli anahitaji kujirekebisha, yeye na Odegaard.

Kwa Saka na Martinelli ninaona wote hao siyo wabaya kiasi cha kusema mchango wao kwenye game unaweza upuuzia na kuamua kuwauza au kuwaweka benchi.
YEs, alikuwa anamkataa partey..
Zubi ajiongeze, kwanza awe na confidenve kisha afanyie sana mazoezi bàadhi ya vitu, ubora mwingine sio wa kuzaliwa nao ni mazoezi tu.

Ishu ya saka na martinelli kiukweli martinelli ni bora awe ST kuliko winger,
Saka kwake ni 50 50, yaank sijawahi kumuamini ni kama anabahatisha tu
 
Wanigeria wamecharuka wanamdiss Odegaard kuna jamaa kambatiza jina anamuita 'King of Looking Busy'

Kwenye game dhidi ya Kairat Odegaard anapokea mpira akiwa nyuma robo tatu ya 18. Eze yupo mbele yake karibu na dimba.

20260504_055226.jpg


Hoja ni kwamba kwa mchezaji anayejali kwamba tunatakiwa kushambulia haraka ilibidi ampe pasi Eze hapa huku yeye akiwa anasogea mbele. Ila Odegaard hakutoa pasi akaanza kudribble kuja hapa dimbani.

Alivyofika dimbani kulia kwake kukawa na wachezaji wawili ambao angeweza kuwapa mpira.

20260504_055650.jpg


Badala ya kutoa pasi kule kulia Odegaard akampa mpira Eze aliyekua kushoto kwake kwenye hii picha.

Yaani amempa mpira mchezaji ambaye angeweza kumpa sekunde 6 nyuma ila akadribble mpaka dimbani halafu akaacha kuendeleza shambulizi kwa kumpa mpira mchezaji yupo pembeni yake.

Goli la pili dhidi ya Fulham ni Ben kampa mpira Saka, Saka akaachia fasta kumpa Ben, Ben hakukaa nao akamuachia Eze.

By this time wachezaji wa Fulham wakawa wanakuja kwa presha juu wakiamini pale wanaondoka na mpira.

MPira unafika tu kwa Eze. Arteta akasogea pembeni ya Eze.
20260504_060241.jpg


Hapo Arteta anamuonyesha Eze ishara ya "Tulia" maoni yanasema uzuri Eze hakumsikiliza kwakua kumsikiliza ilimaanisha kuondoa presha ambapo angekua Odegaard angetoa back pass kwa mchezaji aliye nyuma yake.

Ila Eze akatoa through ball kwa Gyokeres, ambapo watu wawili wakasogea kuufuata mpira. Wakaacha gap ambalo Saka akalitumia kupokea mpira na kuscore.

Kwa maoni ya wadau ni kwamba Odegaard angekuepo uwanjani tungeishia moja bila, kwakua hiyo pasi ya Eze asingepiga.
 
Kwa msimamo ulipo sasa mtu wa 13 anaweza pia kushuka daraja lakini ili iwe hivyo inabidi mtu wa 18 ashinde mechi zake tatu alizobakisha.

Timu ya nafasi ya 18, Westham, imebakisha mechi dhidi ya Arsenal, Newcastle na Leeds. Timu ya 13 ikishinda games zake zilizobaki anaweza kwenda Europa.

Nimekuta baadhi ya mashabiki wa Arsenal wanasema dhid ya Westham itakua easy pia game dhidi ya Burnley itakua easy kwavile Burnley ameshashuka daraja.

Nimekuonyesha kwanini game dhidi ya Westham haitakua nyepesi halafu nakukumbusha kwamba West Bromwich walimpiga Chelsea 5 huku West Bromwich ikiwa imejihakikishia kushuka daraja.

Kama unamkumbuka Maitland Niles alikua kwa mkopo WestBrom wakati wanawanyoosha tano. Notice kwamba hiyo timu itacheza kwa kurelax kuzidi wewe, inaweza kuamua kwamba inapaki basi tu wala hawana haja ya kuvuka hata dimba na hauna unachoweza kuwafanya.

Westham hawatokua relaxed ila wanapambanis uhai, sielewi ni kivipi hii mechi watu wanaona itakua nyepesi.

Kwa sasa kwetu kila game ni final. Hua tunashinda magoli matano games za mwisho wa mwaka halafu hua naandika "Haina haja kwa tulipofikia kuscore magoli mengi" maajabu yake msimu huu yale magoli mengi hatufungi tena.

Arsenal to death
 
Huyu Heaven anayechezea Utd nasikia mlimuuza kwa £1m ,? Bonge moja la mistake, nimemuangalia mechi hizi mbili, anacheza vizuri, ana vision pia haogopi .... . Still ana mature , huyo mtu wenu aliyefinalize hili dili anatakiwa anyongwe mbele ya halaiki !

Same mistake kwa Chelsea kumuuza dogo Rhio Ngumoha kwenda Liverpool...ana potential sana..atakuja kuwa mchezaji mzuri



Utd waliwahi fanya makosa ya kumuachia PoGba wakaja kumrudisha kwa pesa ndefu sana ....



Hii ndio football.....inatokeaga
KdB Chelsea walimtema
Salah Chelsea walimtema

Kuna dogo yupo pale Everton utd walimuachia, nadhan watajuta, ameanzA kuonyesha potential..... Tuchel anamuita WC ! James Garner
 
Wanigeria wamecharuka wanamdiss Odegaard kuna jamaa kambatiza jina anamuita 'King of Looking Busy'

Kwenye game dhidi ya Kairat Odegaard anapokea mpira akiwa nyuma robo tatu ya 18. Eze yupo mbele yake karibu na dimba.

View attachment 3583553

Hoja ni kwamba kwa mchezaji anayejali kwamba tunatakiwa kushambulia haraka ilibidi ampe pasi Eze hapa huku yeye akiwa anasogea mbele. Ila Odegaard hakutoa pasi akaanza kudribble kuja hapa dimbani.

Alivyofika dimbani kulia kwake kukawa na wachezaji wawili ambao angeweza kuwapa mpira.

View attachment 3583554

Badala ya kutoa pasi kule kulia Odegaard akampa mpira Eze aliyekua kushoto kwake kwenye hii picha.

Yaani amempa mpira mchezaji ambaye angeweza kumpa sekunde 6 nyuma ila akadribble mpaka dimbani halafu akaacha kuendeleza shambulizi kwa kumpa mpira mchezaji yupo pembeni yake.

Goli la pili dhidi ya Fulham ni Ben kampa mpira Saka, Saka akaachia fasta kumpa Ben, Ben hakukaa nao akamuachia Eze.

By this time wachezaji wa Fulham wakawa wanakuja kwa presha juu wakiamini pale wanaondoka na mpira.

MPira unafika tu kwa Eze. Arteta akasogea pembeni ya Eze.
View attachment 3583555

Hapo Arteta anamuonyesha Eze ishara ya "Tulia" maoni yanasema uzuri Eze hakumsikiliza kwakua kumsikiliza ilimaanisha kuondoa presha ambapo angekua Odegaard angetoa back pass kwa mchezaji aliye nyuma yake.

Ila Eze akatoa through ball kwa Gyokeres, ambapo watu wawili wakasogea kuufuata mpira. Wakaacha gap ambalo Saka akalitumia kupokea mpira na kuscore.

Kwa maoni ya wadau ni kwamba Odegaard angekuepo uwanjani tungeishia moja bila, kwakua hiyo pasi ya Eze asingepiga.
Ukitaka kujua Arteta ni mpumbavu anaamini kuanza na Ode anamuacha Eze.

Kafungwa na city game 2 kwa upumbavu wake.

Ode ametoka mejeruhi anamuanzisha game ya city yaani ni kama jinga lile kocha.
 
Back
Top Bottom