Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Yule partey ni mtu na nusu. Huyu zubi hafiki anga zile
Rice ni mzuri ana ile damu ya upambanaji, ni bora kuwa na rice kuliko odergad ama zubi..

toka kutoka mwa partey rice hana mchango mkubwa sana kwenye mashambulizi kama msimu uliopita, kuna mwanangu alikuwa per game anampa rice shots,3,4 na hiyo siku ni akimuona partey kacheza na alikuwa anampiga muhindi mara nyingi mnoo
Sahihi .... kuna namna unaona kabisa pengo la Partey lipo .....! Pengine next season, Zubi anaweza kubadilika !!!
 
Huyu zubimendi kwangu hapana,
Gyokeres mfumo wa arsenal ni mgumu kwake.
Odergard kiazi, saka kiazi..

Arteta ajitathmini
Zubimendi huu msimu wake wa kwanza. Mkumbuke Partey msimu wa kwanza alikuaje.

Gyokeres na ugumu wa mfumo ana jumla ya magoli 21. ST wengine wana hali gani?

Odegaard amekua hovyo. Saka kawa hovyo. Utetezi utakua kwamba wametoka majeruhi
 
Zubimendi huu msimu wake wa kwanza. Mkumbuke Partey msimu wa kwanza alikuaje.

Gyokeres na ugumu wa mfumo ana jumla ya magoli 21. ST wengine wana hali gani?

Odegaard amekua hovyo. Saka kawa hovyo. Utetezi utakua kwamba wametoka majeruhi
Uzuri mie nawe tupo humu miaka dahari wa dahari.. partey mie nilimuelewa siku ya kwanza tu, kuna vita hapa ilikuwepo na will jr, akimkataa partey mimi nikisema partey ni fundi,
shida sio zubi kuwa msimu wa kwanza shida ni aina yake la soka, asipobadilika atakuwa hana jipya. Mazoezi ajifunze baadhi ya vitu, ili aongeze ubora, haiwezekani mido inapiga back pass nyingi, side passes za kutosha, afanye mazoezi ya utulivu akiwa na mali na kupiga pasi za mbele, kiungo hutakiwi kuogopa mpira utafikiri mi moto,
saka na martinelli nilwagomea wakiwa kwenye peak yao, msimu ule wanafanya vizuri, nikasema ni wachezaji wa kawaida muda utatuambia, saka ana kaubora kidogo kuzidi martinelli ila ndio wale wale.

Odegard tayari ufaza ushamuingia, anajiona legend tayari, wakati alitakiwa kuongeza juhudi, siku hizi karelax mnooo.
 
Hakuna jema
MPira mchezo wa wazi kabisa, sote tunaona jinsi wachezaji wanazingua, we huoni pengo la partey? Huoni kiwango kibovu cha saka? Huoni odegard, huoni gyokeres anavyoteseka kwa kukosa kupewa pasi stahiki, huoni raya anavyotustili, huoni white kiwango kimeshuka kwa kuwekwa sana benchi, huoni ubovu wa martinelli kwenye kushambulia?
 
MPira mchezo wa wazi kabisa, sote tunaona jinsi wachezaji wanazingua, we huoni pengo la partey? Huoni kiwango kibovu cha saka? Huoni odegard, huoni gyokeres anavyoteseka kwa kukosa kupewa pasi stahiki, huoni raya anavyotustili, huoni white kiwango kimeshuka kwa kuwekwa sana benchi, huoni ubovu wa martinelli kwenye kushambulia?
Sasa tunafanyaje na msimu uko mwishoni?!
 
Maisha yaendelee kwakweli. Kama haya unayoyasema wenye timu hawayaoni au hawajali basi matako yao.
😂🤣
Kutokana na vitu hivi ndio maana siku hizi sina mapenzi yale ya kuumiza moyo eti arsenal kafungwa naona tabu hapana, haiwezekani kocha aweke kepa golini mie namtaka raya kisha timu ifungwe mie niumie 😂🤣
 
Uzuri mie nawe tupo humu miaka dahari wa dahari.. partey mie nilimuelewa siku ya kwanza tu, kuna vita hapa ilikuwepo na will jr, akimkataa partey mimi nikisema partey ni fundi,
shida sio zubi kuwa msimu wa kwanza shida ni aina yake la soka, asipobadilika atakuwa hana jipya. Mazoezi ajifunze baadhi ya vitu, ili aongeze ubora, haiwezekani mido inapiga back pass nyingi, side passes za kutosha, afanye mazoezi ya utulivu akiwa na mali na kupiga pasi za mbele, kiungo hutakiwi kuogopa mpira utafikiri mi moto,
saka na martinelli nilwagomea wakiwa kwenye peak yao, msimu ule wanafanya vizuri, nikasema ni wachezaji wa kawaida muda utatuambia, saka ana kaubora kidogo kuzidi martinelli ila ndio wale wale.

Odegard tayari ufaza ushamuingia, anajiona legend tayari, wakati alitakiwa kuongeza juhudi, siku hizi karelax mnooo.
Kwa kumbukumbu zangu ni Will Jr ndiye alikua anasema Partey ni mbovu. Mimi badi nina imani na Zubimendi mchezaji ambaye ametakwa na timu zaidi ya nne sidhani kama ni kiazi kiasi hicho.

HUyu jamaa ni Busquet mwingine. Kichekesho ni kwamba zile through balls na penetration passes siyo kwamba hawezi ila ghafla tu amekua hazipigi, hizi ambazo Partey alikua hahofii kuzipiga.

Loose balls za nje ya 18 Partey alikua anazipiga nonstop ila Zubimendi hazipigi. Ni kweli anahitaji kujirekebisha, yeye na Odegaard.

Kwa Saka na Martinelli ninaona wote hao siyo wabaya kiasi cha kusema mchango wao kwenye game unaweza upuuzia na kuamua kuwauza au kuwaweka benchi.
 
Tupe maoni yako mkuu baada ya mtanange kuisha🤠🤠....tunaanua mkeka tunaenda nao j4 mapema kabisa....tunakwenda fainali...na tutaomba sana PSG wapite ili tukutane nao watuelezee mwaka jana walitutoatoa vipi🤠🤠
Mmeanza mbwembwe zenu sasa
 
Mtoto wa Hale end, Myles lewis skelly, amekuzwa kwenye basics za total voetbal by papa Arsene Wenger, yani dogo ameanza leo na tumeona mpira wa Arsene Wenger tulioumiss muda mrefu, liquid and attacking football, the things we love the most, hivi ndio vitu vilivyofanya tukaipenda Arsenal, Arsenal is about sexy football.
And not about trophies, I agree kaka
 
Twende polepole hapa.

Newcastle imetoa 55M kwaajili ya Wissa. Mpaka leo Wissa ana magoli 2 mashindano yote.

Newcastle pia ikatoa 70M kwaajili ya Woltermade. Mpaka leo Woltermade ana magoli 8 mashindano yote.

United imetoa 71M kwaajili ya Mbeumo. Mpaka sasa Mbeumo ana magoli 9.

United pia ikatoa 74M kwaajili ya Sesko. Mpaka sasa Sesko ana magoli 11.

Liverpool ikatoa 79M kwaajili ya Hugo. Mpaka sasa Hugo ana magoli 17.

Liverpool pia ikatoa 130M kwaajili ya Isak. Mpaka sasa Isak ana magoli 3.

Arsenal imelipa 65M kwaajili ya Gyokeres. Mpaka sasa Gyokeres ana magoli 21.

Kwanini shabiki wa Arsenal haoni kwamba ana ST mzuri hii sina sababu. Gyokeres angekua na magoli 3 au 9 nyimbo zingekua nyingi, Gyokeres ana magoli mengi zaidi ila mashabiki wa Arsenal hawaongelei hili swala.

Bado wanaamini Gyokeres ni mbovu.
 
Bado ajifunze baadhi ya vitu,Zile faulo zake za hovyo ajidhibiti lakini kunwa zaidi ukiwa middle bila scanning ni shida sana, kila wakati ni mwemdo wa 360° ni wachezaji wachache sana ndio wanafanya hii kitu na lazima awe bora eneo hilo..
Ila sio mbaya bora yeye kuliko kiazi zubi, ye ni kukaba tu, ila kucheza mpira unavyokuja ndio unavyorudi kama TRENI.
Apewe video za partey yule zubi ajifunze, aangalie hata legends waliocheza postion yake aboreshe kiwango
inawezekana zubimendi sio premier league material natamani msimu ujao aje kivingine atuprove wrong.
 
Skelly kacheza vizuri lakini Fulham siyo kipimo sahihi cha kusema sasa akabidhiwe dimba. Kwenye ile mid ya Fulham ile bado haijakamilika pale, Reed ana miaka 2 ndiyo jana kaanza game.

Tukicheza na decent mid Skelly anaweza onekana kaingia kina hakiwezi. But this guy has potential I will be glad to watch him again. Mfano game tumeshinda asindikuze dk za mwisho yeye na Norgaard.
 
Twende polepole hapa.

Newcastle imetoa 55M kwaajili ya Wissa. Mpaka leo Wissa ana magoli 2 mashindano yote.

Newcastle pia ikatoa 70M kwaajili ya Woltermade. Mpaka leo Woltermade ana magoli 8 mashindano yote.

United imetoa 71M kwaajili ya Mbeumo. Mpaka sasa Mbeumo ana magoli 9.

United pia ikatoa 74M kwaajili ya Sesko. Mpaka sasa Sesko ana magoli 11.

Liverpool ikatoa 79M kwaajili ya Hugo. Mpaka sasa Hugo ana magoli 17.

Liverpool pia ikatoa 130M kwaajili ya Isak. Mpaka sasa Isak ana magoli 3.

Arsenal imelipa 65M kwaajili ya Gyokeres. Mpaka sasa Gyokeres ana magoli 21.

Kwanini shabiki wa Arsenal haoni kwamba ana ST mzuri hii sina sababu. Gyokeres angekua na magoli 3 au 9 nyimbo zingekua nyingi, Gyokeres ana magoli mengi zaidi ila mashabiki wa Arsenal hawaongelei hili swala.

Bado wanaamini Gyokeres ni mbovu.
wanaosema Gyokeres ni mbovu mm mwenyewe huwa nashangaa sana, striker msimu wa kwanza tu anaweka kamba 20+
 
Back
Top Bottom