Ambacho watu hawajui au wanajua ila wanajitia uchizi ni kwamba timu inahitaji consistency. Kama leo umeshinda utaweza kufanya hivyo mara tano baadaye?
Katika points 15, Arsenal kadrop points 4, City kadrop points 9 na Villa kadrop 5. Villa mechi yake ya leo ndiyo ya points 15 so hizo points 5 ni kabla ya hii mechi.
Ila utasikia Arsenal hawezi kubeba kombe. Yaani anadrop points balaa. Ila hajui wanaomkaribia wamezidrop hizo points zaidi ya Arsenal.
City wameliona hilo wamejizatiti wamenunua beki na forward. Villa ni timu ambayo priority ni kubaki ligi kuu, ndiyo sababu watu hawaihesabu so haina mpango wa kujizatiti.
Watu wanakuambia Arsenal atadrop point kwa United. United ambayo haijapata ushindi tangu lini? Ikiwa inaenda kwa Arsenal ambayo hajapoteza game nyumbani, ila mtu yupo kijiweni anatema nyongo nonstop.
Nimependa confidence ya Dorgu yeye anasema wanakuja Emirates kuchukua points 3. I hope tutawakabidhi kama anavyofikiria, even better wana mechi moja tu wiki nzima so wana chance ya kupiga zoezi haswa.