Peasant
JF-Expert Member
- Sep 27, 2007
- 3,949
- 699
Hakuna excuse, ila makosa yetu wenyewe na wa kubeba lawama ni Wenger kwa kushindwa kubadili tactics, hivi ndio hakuna plan B kwa Professa? Mfano nilishangaa kuona akimtowa Andre na sio Gervinho? Andre leo gemu ilimkubali na alikuwa anawasumbua sana difensi ya Blackburn, nahisi kama angebakia na kuingia Theo na kucheza kama 2nd striker kwa staili ya 4-4-2, kwa sababu kwa mtindo wa 4-3-3 na mido 3 jamaa walikuwa wanakatiza sana pale kati na tatizo hili ni hata ile mechi ya ManU.
Mikel yuko poa ila Aaron pamoja na kuwa ni mzuri lakini hayuko creative na gemu yake huwa hawezi kusaidia difensi mfano wa Jack. Kwa nini AW kwa muda huu kwa vile tumewakosa Jack na TV5 asibadilike na tukacheza 4 in the middle ili kuwapa extra security difensi yetu?
Anyway Professa ndio anajua ila kuachia mabao 14 katika mechi 5 sio mchezo, tunaongoza katika ligi kwa rekodi ambayo sio familia kwetu kwa kufungwa mabao mengi. Wenger lazima aamke sasa ili kuunusuru msimu wetu.
Matatizo yetu makubwa ni mawili:
1. Difensi yetu inasumbuka kwenye kona na free-kick na hii ni dhahiri kutokana na idadi nyingi ya mabao ambayo tumefungwa ni aidha kona ama free-kicks, ukiachilia hii mpya ya leo ya kujifunga. Kwa kumkosa TV5 hakuna calm influence kwa CB zetu, Per bado hajachanganya na Djourou na Koscielny ni ajali tupu, hawakawii ku-panick.
2. Mido yetu ni nyepesi - kuondoka kwa Samir na Cesc na ukichanganya na majeruhi ya Jack tumebaki watupu hapa kati, Mikel ni ongezeko zuri ila bado jukumu la ku-supply zile service kwa RVP in zito kwake. Aaron pamoja na uzuri wake ameshindwa kupeleka service kikawaida ingawa namsifu sana kwa pasi yake kwa Mikel iliyotupatia bao la pili.
Andre ni mzuri kwenye attack lakini defensively yuko poor. Nimemwona kama mara2 au 3 hivi akiwa hayupo kwenye position na hivyo kuwapa Blackburn nafasi kushambulia, hii ni pamoja na goli la nne mlilofungwa.