Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Assalam Aleyqum....!!!
Nawatakia mashabiki wenzangu wote wa Arsenal + Haterz EID MUBARRAK..... M/Mungu awajaalie afya njema katika sikukuu hii....More over aijaalie Arsenal under pro. AW ikamilishe usajili ili tuanze ligi....

EID MUBARRAK.

Q.

Tunashukuru, ila wenzako tunaamini ni binadamu anaeamua aya mambo, kwa hilo basi tunataka na wewe uamuombee kwa mungu wako afanye maamuzi yakinifu!
 
Mimi sifagilii usajili wetu kwa sababu tumerudi style ileile ya kusajili un-proven na nje ya premiership ama vijiligi vidogo-vidogo.
Kwangu mimi Mertesacker pekee pengine ndio ni kiwango, watu tunafurahia kwamba tunasaini wachezaji? Jee viwango vyao na kuhimili ligi ya Premiership vikoje? Tukumbuke wengi tulikuwa na matumaini na Chamakh lakini matokeo yake amekuwa flop.


Timu yetu sasa inahitaji tusajili proven world class players ama at least wachezaji wenye uzoefu wa kucheza kwenye premiership, binafsi sifurahii kusajiliwa kwa Santos kwa sababu bado hajawa proven in EPL na hatujui atafiti vipi, ni afadhali unipe Samba ama Cahill najua watafiti moja kwa moja na watanifanyia kazi gani.
Nahisi hata huyu striker wa ki-korea Park hakukuwa na umuhimu wa kumsajili kwani naamini tatizo letu kubwa sana ni kwenye difensi na kidogo pengine viungo baada ya kuondoka kwa Cesc na Samir, hili la viungo naona kwangu mimi sio tatizo kubwa kwa sababu tuna wachezaji watakaorudi Song, Wilshere na Frimpong na ninaamini Rosicky na Wilshere wanaweza kufanya mambo makubwa msimu huu watu wakawasahau hata kama kulikuwa na akina Nasri.
Back four ndio backbone ya timu yetu na ukiondoa TV5 na Sagna hatuna tena qualities defenders, Traore ameondoka leo kwa hio huku kushoto tunawategemea Gibbs na huyu new signing Santos. Santos pengine ni mzuri lakini bado hajawa proven katika EPL.
Suala bado ni kwamba kwa nini hatukusajili uzoefu na umahiri wa Cahill ama Samba na tumeenda kubahatisha kwa Santos?
 
Kweli, in arsene wenger i trust. Arsene knows better. Hizo flip flops ni ajali kazini. Ukizungumzia uzoefu, hata Mikael silvestre alikuwa mzoefu, alitusaidha? Lassana Diarra alishacheza Epl, alitusaidia?

Unproven players i.e TH14, Anelka, Cpt Viera, Ljunberg, et al hawa walisajiliwa bila majina makubwa, but prove to be world class. Mfumo wa Wenger Arsenal, ana blend academy players, na 'outsiders' ...world class managers wanampa credit AW kwa hilo, who are we to criticize that?

Tusiwe kama Man city, team haina foundation. Santos tayari anachezea Brazil national team, dont underestimate him aisee... Unamkumbuka Silvinho? He was unproven but ended up a top notch. Song sio wa kutegemea sana, Africa Cup ipo corner, , Diaby ndio hivyo tena..wodini nusu msimu.

We need players kusaidia mabadiliko ya formations zetu ambao pia ni team players na adaptable, and Only Arsene Wenger knows better.

Pamoja we stand, We are the Gunners.
Eid njema wakuu.
 



article-2031953-0DA39D5B00000578-647_468x712.jpg

 
article-2031771-0D977ED700000578-237_468x348.jpg


Chu Young Park anapenda kuitwa Ju na nyuma ya jezi yake jina litasomeka J.Y.Young

Huyu amesajiliwa kama centre forward na Van Persie atacheza namba yake ya kawaida 10.

Santos anaingia straight kwenye first XI, yaani beki wa kushoto.

Chamakh na Arshavin kwa sasa hawawezi ni wazito mno.

Arsenal Probbale team for Swansea game.

Szczesny, Sagna, Santos, Vermaelen, Mertesacker, Rosicky, Ramsey, Walcott, Arshavin, J.P Young, Chamakh
Tunasubiri tuone
 
kuna tetesi Keisuke Honda has arrived in London for a medical .. kama kweli... itakuwa safi sana... ni aina ya mchezaji tunaye muhitaji pale kati
 
Arsenal have agreed a deal to send squillaci to south korea, to serve two years of nation service army on behalf of Chu Young Park.
 
Mkuu wangu sana Kweli.....Nimekusoma vizuri sana....

Timu yetu(kwa kiwango walichoonesha juzi wakati wa game na Newcastle) bado ni mbovu mkuu...Hatuna kiungo cha kuaminika,hatuna beki 4 mzuri wa kusaidiana na kitasa TV5, hatuna beki 3 mzuri(Gibbs akiumia sijui nani atacheza,Traore?),hatuna mshambuliaji mfungaji mzuri wa kusaidiana na RVP pale mbele.....Pia Sagna akiumia sijui itakuwaje....

Mpira wa sasa ni pesa mkuu,ni pesa ndizo zimeifanya Chelsea ikawa tishio kwani iliweza kusajili wachezaji wa maana kiasi cha kutupoka ile nafasi yetu ya kuwa wapinzani na washindani wakubwa wa Man Utd kwenye title race ya EPL.....Ni pesa ndizo zinaifanya Man City kutuondoa kwenye Big 3 ya EPL....Na ni pesa ndizo zitatufanya tusiwepo hata kwenye Big 4 ya EPL.....Tatizo Arsenal si pesa,tatizo ni sera mbovu za AW na Directors wake.....Wanaweka pesa mbele kuliko maslahi ya timu.....

Haiwezekani Arsenal iliyokuwa tishio kubwa katika EPL,ambayo ilikuwa ikipokezana ubingwa na Man Utd leo hii ikawa nyuma ya Man City na Chelsea.....Haiwezekani hata kidogo.....AW na bodi yake wanatakiwa wafanye maamuzi magumu,wazitumie pesa watakazozipata kwa kuwauza Fabregas na Nasri kuwanunua wachezaji wa maana....Nashangaa sana kusikia eti AW anabargain kumnunua beki mahiri kama Chris Samba kwa paundi mil 12,eti anataka kununua chini ya hapo....Huu ni upuuzi.....Pia juzi kasema hana mpango wa kuwanunua Jadson wala Mata,hii ina maana hana mpango wa kununua kiungo atakayeziba pengo la Nasri wala nafasi ya Fabregas?.....Hiki kitakuwa ni kichekesho,maana huyo Ramsey ambaye anategemea ndiyo ataziba pengo la Nasri/Fabregas sijaona lolote alilolifanya juzi zaidi ya kukimbiakimbia uwanjani na kupoteza mipira....Hata Frimpong bado sana kumtegemea......

AW anapaswa kusajili wachezaji wa maana(bila kuangalia bei zao),tumechoka kwa kweli kweli kuwa wasindikizaji kwa misimu zaidi ya mitano.....Tusiitumie timu ya wakubwa kuwaandaa/kuwatengeneza wachezaji,wachezaji waandaliwe kwenye academy na kwenye timu ya reserves lakini si kwenye timu ya wakubwa,hii ni bahati nasibu na ni utaratibu ambao tayari umeonesha kufeli(kwa miaka mitano iliyopita)......Nina uhakika Liverpool,Newcastle na Spurs wakiendelea kusajili na kukaa sawa na sisi tusiposajili msimu huu tutakuwa nyuma yao......Kwangu mimi kuwa nyuma ya timu hizi hakuna tofauti na kuwa nafasi ya 10 kama sio ya 15....

Arsenal haikupaswa kuwa nyuma ya Chelsea wala Man City,Arsenal size yake ilikuwa ni Man Utd basi.......Arsenal siyo timu ya kukosa hata kombe la Carling kwa kufungwa na vibonde walioshuka daraja Birmingham....

Nawakumbuka sana The Invincibles

Asante sana kwa Arsene na Bodi kwa kusikia kilio changu.....

Arsenal........Together We Stand!!!!!
 
Hahahaha! braza AW bana....unajua leo nimekaa kimajungumajungu lakini nashangaa nachelea ku post apa kwa nyie watani zangu....
BTW kudos kwa usajil wa gafragafra......kumbe nane zile zimewaamsha...mkipigwa sita tena weekend ijayo bila shaka mtamleta ad Sneijer...lmao..
Alamsiki mtani!
 
Leo hakulaliki mpaka kieleweke.

Arsenal muda mfupi ulopita wameamua kuachana na kumsajili Mikael Arteta na kuelekeza juhudi zote kwa Yosi Benayoun. Arsenal wanataka wamsajili Benayoun kwa mkopo na kuna uwezekano wa kumsajili mchezaji huyo usiku huu kabla ya saa tano.

Club ya Everton inataka paundi milioni 10 lakini Arteta ana miaka 29 kwahio ni pesa nyingi kuzingatia umri.
 
Leo hakulaliki mpaka kieleweke.

Arsenal muda mfupi ulopita wameamua kuachana na kumsajili Mikael Arteta na kuelekeza juhudi zote kwa Yosi Benayoun. Arsenal wanataka wamsajili Benayoun kwa mkopo na kuna uwezekano wa kumsajili mchezaji huyo usiku huu kabla ya saa tano.

Club ya Everton inataka paundi milioni 10 lakini Arteta ana miaka 29 kwahio ni pesa nyingi kuzingatia umri.

Na sie wabishi lakini , Mil 10 hio itajilipa tu kwa sasa kwani upinzani mkubwa mno.
 
Na sie wabishi lakini , Mil 10 hio itajilipa tu kwa sasa kwani upinzani mkubwa mno.

Mkuu tatizo wamekosea ku-log deal kwa wachezaji wawili kwa wakti mmoja, yaani Arteta na Benayoun. Kwahio Arteta ameona anaweza akakaa benchi kama Benayoun atakuwa akianza na Song pale katikati.

Hivi vitu vilitakiwa vifanyike mapema.

Lakini hamna tabu kwanio pale katikati pana Song, Diaby, Ramsey, Rosicky na ikiwa atasaini leo basi itakuwa na Benayoun.
 
Arteta wamekataa bana 10mil + bendtner wamepiga chini
 
Back
Top Bottom