Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Haya masuala ya kumsubiri mtu ajifunze wakati ambao tunataka matokeo ndio jambo ambalo sisi mashabiki hatuwezi kulivumilia.

Kama kuna watu walioko tayari kama Fabio/ESR ni bora muda mwingi wapewe wao huku tukimpa muda kidogo kidogo Havertz wa kujifunza.. awe anaingia time kama zile anazoingia Fabio, dk ya 75 hivi muda huo tukiwa tunaongoza goli 2 na kuendelea au asubiri aanze mechi za Carabao na FA.
Uko sahihi kabisa na Fabio Vieira leo ametoa pasi murua sana kwa Jesus kwenda kufunga, na hivyo ndivyo Zinchenko apaswa kuangalia analink vipi mchezo na mchezaji wake wa kiungo (Havertz).

Hata mchezaji akiwa mzuri kiasi gani akijiunga na timu ni lazima ajifunze kucheza na wachezaji wenzie wapya mifumo mbalimbali yaani formations.

Kuna kutoa pasi kutoka kwa beki iwe Zinchenko kwa Havertz au Ben White kwa Bukayo Saka na weye kama beki watakiwa ufanye timning ya ile pasi yako na ikiwa mbovu au umechelewa ndo utaona Saka au Havertz ashindwa kuumudu mpira (ball control) na huupoteza kwa adui.

Pia Martinelli na Saka wakiwa wachezaji wa pembeni kuna kujenga mashambulizi na mabeki au Odegaard na kama hakuna hiyo link Arsenal hupata taabu sana kufanya mashmbuliz ya maana.

Hivyo kulink mchezo na mashambulizi hasi kufunga ni lile goli la kusawazisha la Arsenal yaani mchezo umeunganishwa tangia mwanzo hadi mwisho kwa Onana.

Hivyo wenzetu hawa hawauchezi tu mpira na ndo maana Tierney na Tavarez au Lokonga na wamepewa tena muda wa kujifunza namna ya kulink mchezo bila kukimbia tu kama wafukuza sungura wa kitoweo.
 
Wadau humu hatupingi Kai kupata time. Everyone anahitaji kucheza.

Vieira alipata time akianzia nje. Na Kai iwe hivi.
Yote sawa mkuu, Hakuna anayelazimisha aanze ,tatizo wadau wanaweka chuki Sana

Ilifika hatua mtu anadai Partey anacheza RB ili Kai acheze

Leo Partey alikuwepo?

Mchezaji anahitaji muda azoee , Kuna mchezaji alichukua muda Kama Partey kuzoea lone 6

Arteta on Havertz:

"I said to him yesterday beginings are hard. When I met my wife at beginning it was hard to conquer her, I had to try and message and go and go...

At end when she said yes we want to be together, it's beautiful."
20230903_214651.jpg
 
Nachokiona ni kwamba Kai siyo m bovu ila tu kwenye role ambayo anataka arteta acheze sana kuizoea kwa sababu yeye ni mshambuliaji . Xhaka ilikuwa rahisi kui master vizuri. Hata Fabio mwanzo alikuwa hivi hivi hasa lege lege Nashukuru sasa hivi Fabio anau wezo mzuri sana . Hata siku Ode akikosekana ntakuwa sina wasi wasi kutokana na uwepo wa Fabio. Ila leo naamin kama angeanza jorginho na rice game ilikuwa inaisha mapema sana
 
Nilikua naona Martinelli hamuamini Kai, akipata mpira Kai akitokea Martinelli anatafuta njia kwingine.

Katika games nne za points 12 tumepata 10. Siyo mwanzo mbaya hata kidogo. Kilichopo benchi lione ni kivipi tunaweza secure points nyingi zaidi
Nili Note hiki kitu na mimi, baada ya kupika pasi ya hovyo iliyoenda kuzaa bao la Man U.
 
Hapo ndipo kazi ya umeneja inapokuwa muhimu sana kwa timu.

Player management ni kitu kizuri sana na Arteta safari hii akiweza kuwamanage wachezaji basi Arsenal itafika mbali kwenye mechi za PL na CL.

Partey kwa sasa ni kwa mechi chache akipona na kwa kuangaliwa sana ila nahisi Arsenal watatafuta DM mwingine ikifika January.
Kwann asianze na jorginho na rice kipind hiki partey hayupo naona kam mchele utatupa faida san ukiwa juu kidogo sabb jamaa anatupa energy y kutosha kila angle y uwanja
 
Nachokiona ni kwamba Kai siyo m bovu ila tu kwenye role ambayo anataka arteta acheze sana kuizoea kwa sababu yeye ni mshambuliaji . Xhaka ilikuwa rahisi kui master vizuri. Hata Fabio mwanzo alikuwa hivi hivi hasa lege lege Nashukuru sasa hivi Fabio anau wezo mzuri sana . Hata siku Ode akikosekana ntakuwa sina wasi wasi kutokana na uwepo wa Fabio. Ila leo naamin kama angeanza jorginho na rice game ilikuwa inaisha mapema sana
Muda wote alochezea Chelsea Havertz alitumika kama mashambuliaji na ndipo alipopata shida ya kutofunga magoli mengi.

Kai Havertz ni deep lying Midfielder nafasi alokuwamakicheze atimu yake ya Borussia Dortmund.

Hiyo ndo nafasi ambayo Arsenal wataka awe akicheza.
 
Havertz amechukua nafasi ya Xhaka na ataweza kuwa sawa.

Anatakiwa awe na maelewano mazuri ya Zinchenko upande wao wa kushoto.

Atakuwa sawa tu na atafunga magoli kama ilivyokuwa kwa Xhaka.

Mpira wa wenzetu ni mipango na mifumo na ili kuipatia kucheza yatakiwa uwe na ustahamilivu.

Meneja ana imani na Harvetz na atakuwa acheza kila mechi ili kufit in katika mfumo wa uchezaji wa Arsenal.

Ila huko mbele Jesus atarudi kuanza mechi na Nketia atarudi bench.

Pia hali ya hewa kulikuwa na joto kali hivyo kuathiri uchezaji kwa kuufanya uwe slow sana.
Harvertz kachukua Nafasi ya Xhaka ???? How

May be kabadilishiwa majukumu ila kusema amechukua nafasi ya Xhaka ni uongo

Nafasi ya Xhaka ilikua inatoa Assist na Magoli

Kwa sasa kitu icho hakipo mpaka sasa

Nguvu ya kuzuia wakati hatuna mpira now zinazibwa nafasi ambapo kwenye hilo Kai anasaidia

Mtu naemuona anauwezo wa kuchangia Goals & Assist kwenye LCM alipokua anacheza Xhaka ni Fabio na Trousard ila kwa Kai naona Awe ST tu basi wawe wanaachiana nafasi na Nketia,Jesus
 
Harvertz kachukua Nafasi ya Xhaka ???? How

May be kabadilishiwa majukumu ila kusema amechukua nafasi ya Xhaka ni uongo

Nafasi ya Xhaka ilikua inatoa Assist na Magoli

Kwa sasa kitu icho hakipo mpaka sasa

Nguvu ya kuzuia wakati hatuna mpira now zinazibwa nafasi ambapo kwenye hilo Kai anasaidia

Mtu naemuona anauwezo wa kuchangia Goals & Assist kwenye LCM alipokua anacheza Xhaka ni Fabio na Trousard ila kwa Kai naona Awe ST tu basi wawe wanaachiana nafasi na Nketia,Jesus
Alipokuwa akicheza Xhaka ndipo anapocheza Kai Harvetz na ndo maana Xhaka akaruhusiwa kuondoka.
 
Kwanini Trossard/Rowe/Vieira wasianze kwenye LCM kisha kama kocha ana mahaba na Kai amu-intergrate taratibu kwenye kikosi kwa kuingia sub? Mbona anafosi sana
 
Havertz wengi wadhani ni striker au "deep lying midfielder" jambo ambalo si sahihi.

Arteta ataka Havertz awe analink mchezo kati ya Zincheko na Ben White na awe anakuja mwisho kumalizia shambulizi kwa kufunga goli.

Ndo maana mechi zingine zilopita amecheza kama "false 9" au attacking midfielder nafasi ambayo leo amecheza Odegaard kwa ufanisi mkubwa ikiwemo kufunga goli la kusawazisha.

Hivyo Havertz ni "deep lying midfielder", Odegaard ni attacking midfielder na Declan Rice ni central Midfielder nafasi ambayo ilikuwa ni ya Thomas Partey.

Havertz atakiwa sasa akazanie kujifunza kutopoteza mipira sana na pia kutokuwa slow kwenye kulink mchezo.

Hivyo mechi ijayo na Everton utashangaa Arsenal ikiwa ni timu ingine kabisa kwa kutumia mfumo mwingine ili kumzuia Sean Dyche asicheze "10 men behind the ball" kisha kuvizia kufanya counter attack kama alivyokuwa akifanya Rashford leo.
Iyo game inaitaji mafundi tupu hasa LT19
 
Back
Top Bottom