Mkuu hii division ulonipa ni muhimu sana kwani inahusiana na masuala yoote ya mbinu au "tactical purposes".
Nashukuru sana kwa wadhifa huo na ntakuwapo hapa mwezi ujao.
Arsenal huwa wanafanya mambo yao bila kutumia vyombo vya habari maana vyombo vyenyewe siku hizi vimekuwa kama vya kwetu tu Africa, yaani kuongea mambo bila kufanya upembuzi yakinifu.
Wachezaji waliosajiliwa mpaka sasa ni mmoja tu Gervinho ambae Mzee Wenger anataka acheze pembeni namba kumi akichukua nafasi ya Samir Nasri na Nasri atakuwa akicheza pale kati yaani namba nane. Nasri kwenye mechi zote za karibuni amekuwa akicheza namba nane akiwa amechukua nafasi ya Fabregas (hii ni mbinu pia ikiwa Fabregas atauzwa au atakuwa akikaa bench).
Gervinho (miaka 24) amesajiliwa na kwa gharama za paundi milioni 10.6 kutoka timu ya Lille ya France.
Phil Jagielka mpaka sasa ni mchezaji wa Everton ya Uingereza.
Juan Mata mpaka sasa ni mchezaji wa Valencia ya Spain.
Christopher Samba mpaka sasa ni mchezaji wa Blackburn.
Kuna kila uwezekano wa Arsenal kutoa kitita cha fedha kulipa gharama za usajili wa wachezaji muhimu watatu Juan Mata (Paundi Milioni 17.5) kutoka Valencia ya Spain, Phil Jagielka (Everton wanataka Paundi Milioni 18) na Chris Samba wa Blackburn ambao wanataka paundi milioni 12. Hizo ni jumla ya paundi milioni 44.5 na Arsenal ina akiba ya pesa benki mpaka sasa (ambayo haijaguswa ) paundi 110 milioni.
Ikiwa mambo yatakwenda sawa tactically Arsenal watakuwa na moja ya ngome ngumu kupitika ikijumuisha Kipa- Szczesny, Sagna, Vermaelen, Djourou na Jagielka ( kama deal likikubali) au Cocsielny.
Kiungo- Song, Wilshere, Nasri na Gervinho
Washambuliaji- Van Persie, na Carlos Vela
Wachezaji wa akiba- Juan Mata (kama deal litakubali) , Chris Samba(kama deal litakubali) , Arshavin, Aaron Ramsey na Thomas Rosicky.
Jumamosi tuna mechi ya kirafiki na Boca Juniors na Jumapili pale Emirates kutakuwa na Emirates Cup na timu yetu itaanza kucheza na Red Bull New York ambayo itakuwa na Thiery Henry miongoni mwa kokosi chake cha kwanza.