Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

eti hamna mtu anaepaki basi lile mlilopaki kipindi cha pili lilikua behewa la treni?
Hivi mnamjua Liverpool akiwa Anfield nyie kima?
Tena bahati yenu mngejifanya kutaka kupishana 7up ya nyumbu na nyie mngeikunywa vizuri tu kima nyie.




#Arsenyo Kondoo
#Haaland kiatu
#Mancity bingwa Epl 2022/2023
Rashford nje miezi miwili ,una habari ?au unapayuka tu humu
 
Huu uzi pia sio mbaya una unyama flani

Ila third kit ya season hii ni hatari na nusu
20230411_142542.jpg
 
Unajua me nashangaa sana ... watu wanavyoibeza hii arsenal.
Ipo hiv ... kila timu ilikuw imebakisha mechi tisa kuelekea mwisho wa msimu. Lakini ni ukweli usiopingika kuwa miongoni mwa mechi ngumu kwa arsenal ilikuwa ni ya liver. Hasa ukizingatia mechi inapigwa Anfield. Ile mechi laiti kama ingekuwa inapigwa emirates arsenal alikuwa ameshashinda kabla ya mechi
Katika mechi nilizokuwa najua arsenal atapotezani dhidi ya liver tena na ndo mechi ngumu kuliko zote alizokuwa amebakisha arsenal. Yawezekana man city asipoteze mechi yoyote kati ya zilizobaki.
Na arsrnal nia yake kubwa ilikuwa asipoteze mechi yoyote kati ya zote 10 zilizokuwa zimebaki.
Naona hili wazi kabisa linaenda kutimia. Kuna mtu nilimwambia kuwa kati ya big six zote hakuna atakayechomoka Anfield.
Arsenal inabidi washukuru kuondoka na point Anfield.
Kombe bado lipo mikononi kwa arsenal.
Nyie kweli misukule, si ndio nyie mlituaminisha game ngumu pekee ni brighton na newcadtle? Leo baada ya kupakishwa basi ndio mnajua Anfield pagumu.
sasa nyie vilaza taarifa tu chelsea wabovu lakini lazima awachezee makalio. Nimekaa pale.
 
Tulikuwa 2:0 ahead , xhaka panic sijuiii alikua anazileta za nini wakati timu inaongoza tayariii. Huyu refa wa leo nae sijuii ameacha gemu ichezeke ki ubabe sana mara amezingua sana!!
Sub ya zincheko ilitakiwa ifanyike kabla hata goli halijarudii dk ya 75-80 huko ukizingatia tierney ni bora sana kwenye defense way, huyu kiwior ilikua haina haja ya kuingia.
The way tumetoka 2:0 up to2:2 daah hii gemu ilikua tayariii tushaimaliza panic baadhi za wachezaji wetu hasa xhaka zimefanya game kuisha hivi maana toka muda ule mpira ulikua haukaiii kabisa kwetu , duels nyingi tumepoteza, pasi zikawa hazifikiii.

From 2:0 to 2:2 hii ndo imeniuma zaidiii .
Umeandika kinyongeeeee Labyrinth 84 Ha ha haaaaaaaaaaaaa
 
Bayern walichobugi ni kupenda wachezaji wa beii chee huyu kipa siyo wa level yao
Sasa kati ya Bayern na nyie Arsenyau ni nani anaependa wachezaji wa bei chee?
Umeona kwanza mpira wa wanaume waliokomaa unaochezwa kwenye Uefa?
Haya nyie pelekeni hicho kikosi chenu cha wanywa uji muone mtakavyotolewa mapema tu kwenye group stage.
 
Pointi 6, Man City anakuja kuchukua 3 na magoli ya kutosha afu na bado mtakuwa na mechi moja zaidi yake 😂
Anakuja mgonjwa Chelsea anakuja kupata draw
Anakuja mnyonge flani kutoka pasipojulikana anawalisha vumbi
 
Back
Top Bottom