KUNA WATU WANANUNA TUKIICHAMBUA TIMU YETU , NI HIVI KUNA TIMU ZINAVYOCHEZA HUWEZI KUZICHAMBUA ,PAPATUPAPATU NYINGI SANA
Na Ambangile
Arsenal v Everton
°Jinsi timu pinzani zinavyocheza dhidi ya Arsenal hiyo ni ishara tosha Arsenal walipo sasa hivi , timu nyingi zinapaki sana Bus maana yake wana hofu na ubora wa Arsenal
°Alichofanya Sean Dyche nafikiri hakuwa na namna na nafikiri alikuwa sahihi ni kukaa nyuma zaidi ya mpira , hakuna haja ya kupishana na Arsenal ( 4-5-1 bila mpira ) wanazuia pembeni na ndani na kwa takribani dakika 40 Arsenal walipata tabu kuwafungua Everton , kwanini ?
1: Hakukuwa na space nyuma ya safu ya ulinzi ya Everton
2: Hakukuwa na space nzuri katikati ya mstari wa ulinzi na kiungo wa Everton
3: Pembeni ya uwanja ( Iwobi na McNeil ) walihakikisha fullbacks wao wawili hawakabiliani na 1 Vs 1 za mara kwa mara dhidi ya wingers wa Arsenal ( Saka na Martinelli )
4: Sehemu pekee Everton walikubali kuacha space ni kwa mabeki wa Arsenal na Jorginho .
°Ukicheza aina hiyo ya Soka hakikisha hausinzii uwanjani ( dont switch off ) kwasababu wachezaji wazuri watakuadhibu na hapo ndio unasifia " POSITIONAL PLAY " ya Arsenal katika ubora wake ... inafanyaje hiyo Positional Play ?
1: Inahitaji muda na nafasi ( Space and Time ) maana yake ?
2: Ukiwa na nafasi ndogo , mchezaji anatakiwa kuwa mfanisi zaidi katika kila kitu anachofanya . Na ukiwa na muda mdogo maana yake unatakiwa kuwa haraka sana katika kitu unachofanya
3: Arsenal waliunganisha vyote hivyo : Ufanisi na Uharaka ( Zinchenko , Odegaard , Martinelli na Saka ) jinsi walivyokuwa wanabadilishana nafasi uwanjani kupatikana goli la kwanza
4: Zinchenko kutoka kushoto kwenda kulia kwenye namba 8 wa kulia , maana yake nafasi yake lazima awepo mtu ( Xhaka ) na nafasi ya Xhaka ikachukuliwa na Odegaard . Martinelli kutoka kushoto mpaka kulia kwa Saka . Maana yake Trossard akachukua nafasi ya Martinelli kushoto . Saka akachukua nafasi ya Trossard ndani namba 9 wakati Martinelli yupo kulia kwa Saka
POSITIONAL PLAY katika ubora wake
NOTE
1: Counter attacks walizopata Everton kipindi cha kwanza walikosa ufanisi
2: Zinchenko " Technician "
3: Saka ameboresha matumizi ya mguu wa kulia
4: Martinelli mechi 3 za mwisho magoli 4
5: KAMA EVERTON WAMEONEWA LETA TIMU YAKO
FT: Arsenal 4-0 Everton