Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Yani wewe jamaa sijui una hofu gani na sisi Manchester yani wa nyuma yako ni city lakini muda wote unatuwaza Manchester tu
Siwez kuwawaza nyie ,mbona hujiulizi why nyie mnajazana humu wakati Spurs na Newcastle wapo karibu kuwatoa top 4


Yaani nyie ndio mna Mandate ya kutusumbua sisi humu, mkiguswa nyie mnawaka
 
Saka 200k per week

Arsenal made an improved offer to Saka just before he departed to Qatar for the world cup. New deal was more in line with what Saka is worth and a broad verbal agreement was done (just before WC). Finer details were sorted out last week.
 
Saka 200k per week

Arsenal made an improved offer to Saka just before he departed to Qatar for the world cup. New deal was more in line with what Saka is worth and a broad verbal agreement was done (just before WC). Finer details were sorted out last week.
Great.....hivi computer wapi siku hizi?
 
KUNA WATU WANANUNA TUKIICHAMBUA TIMU YETU , NI HIVI KUNA TIMU ZINAVYOCHEZA HUWEZI KUZICHAMBUA ,PAPATUPAPATU NYINGI SANA

Na Ambangile

Arsenal v Everton

°Jinsi timu pinzani zinavyocheza dhidi ya Arsenal hiyo ni ishara tosha Arsenal walipo sasa hivi , timu nyingi zinapaki sana Bus maana yake wana hofu na ubora wa Arsenal

°Alichofanya Sean Dyche nafikiri hakuwa na namna na nafikiri alikuwa sahihi ni kukaa nyuma zaidi ya mpira , hakuna haja ya kupishana na Arsenal ( 4-5-1 bila mpira ) wanazuia pembeni na ndani na kwa takribani dakika 40 Arsenal walipata tabu kuwafungua Everton , kwanini ?

1: Hakukuwa na space nyuma ya safu ya ulinzi ya Everton

2: Hakukuwa na space nzuri katikati ya mstari wa ulinzi na kiungo wa Everton

3: Pembeni ya uwanja ( Iwobi na McNeil ) walihakikisha fullbacks wao wawili hawakabiliani na 1 Vs 1 za mara kwa mara dhidi ya wingers wa Arsenal ( Saka na Martinelli )

4: Sehemu pekee Everton walikubali kuacha space ni kwa mabeki wa Arsenal na Jorginho .

°Ukicheza aina hiyo ya Soka hakikisha hausinzii uwanjani ( dont switch off ) kwasababu wachezaji wazuri watakuadhibu na hapo ndio unasifia " POSITIONAL PLAY " ya Arsenal katika ubora wake ... inafanyaje hiyo Positional Play ?

1: Inahitaji muda na nafasi ( Space and Time ) maana yake ?

2: Ukiwa na nafasi ndogo , mchezaji anatakiwa kuwa mfanisi zaidi katika kila kitu anachofanya . Na ukiwa na muda mdogo maana yake unatakiwa kuwa haraka sana katika kitu unachofanya

3: Arsenal waliunganisha vyote hivyo : Ufanisi na Uharaka ( Zinchenko , Odegaard , Martinelli na Saka ) jinsi walivyokuwa wanabadilishana nafasi uwanjani kupatikana goli la kwanza

4: Zinchenko kutoka kushoto kwenda kulia kwenye namba 8 wa kulia , maana yake nafasi yake lazima awepo mtu ( Xhaka ) na nafasi ya Xhaka ikachukuliwa na Odegaard . Martinelli kutoka kushoto mpaka kulia kwa Saka . Maana yake Trossard akachukua nafasi ya Martinelli kushoto . Saka akachukua nafasi ya Trossard ndani namba 9 wakati Martinelli yupo kulia kwa Saka

POSITIONAL PLAY katika ubora wake

NOTE

1: Counter attacks walizopata Everton kipindi cha kwanza walikosa ufanisi

2: Zinchenko " Technician "

3: Saka ameboresha matumizi ya mguu wa kulia

4: Martinelli mechi 3 za mwisho magoli 4

5: KAMA EVERTON WAMEONEWA LETA TIMU YAKO

FT: Arsenal 4-0 Everton
 
Tetesi za Usajiri

Arsenal wana uhakika wa kumsajili Declan Rice msimu huu wa joto kwa £80m.

Wanaweza kurudi kwa Caicedo.

Arteta anataka wachezaji 2 wa kati, winga na beki wa kulia msimu huu wa joto.

Kieran Tierney, Sambi Lokonga na Nuno Tavares wanaweza kuondoka msimu huu wa joto.
 
𝐅𝐎𝐎𝐓𝐁𝐀𝐋𝐋 𝐌𝐀𝐃𝐄 𝐈𝐍 𝐀𝐑𝐒𝐄𝐍𝐀𝐋.

Hawa Kenge tumewapiga 4 na Mpira mwingi wakagawane na vibaraka wao shubaamitt

Michezo sawa and FIVE POINTS CLEAR.Umenisikia au niirudie?

Kama utasema team yako inacheza mpira mzuri,nitakuuliza kama Arsenal? Watu wanapasiana kutoka nyuma haijalishi Kuna Presha kiasi gani.Kila mchezaji yupo kwenye movement muda wote kuhakikisha Kuna options ya pasi haijalishi ni Eneo gani la uwanja.I ,You,We they call it Football organism

Arsenal ndo team ya kwanza msimu huu kuwa na wachezaji 2 wenye Goli 10+ , Bukayo Saka na Gabriel Martinelli

Kwenye magoli 10 ya Bukayo Saka, magoli 6 Yalikuwa niya kuipa Arsenal Uongozi kwenye Mechi.Na magoli 4 niya Kusawazisha.Ni Harry Kane peke yake ndo amefunga Magoli ya maamuzi zaidi ya Saka (11)

Let's talk kidogo kuhusu lile bao lake.Ile Movement ya Zinchenko ndo exactly alitakiwa kufanya.Kupunguza watu Peke yake ili kuifungua Ile Midfield ya Everton.Then Bukayo Saka anapokea na Mguu wa kushoto,on the turn na ule Mguu wake wa kuvukia Barabara.Baaaaang.

Infact Bukayo Saka amehusika kwenye goli 19 katika michezo 25 msimu huu.Ni ulimwengu wa Bukayo Saka tuishi humo.

Everton walikuja na Plan kama ya mechi ya kwanza.Arsenal wacheze ,sisi tuharibu.Waliziba Space na 4-5-1 kama kawaida,Lakini Arteta alikuwa na Plan nyingine.Kivipi?

Leandro Trossard amechukua tena nafasi ya Eddie ENKETIAH kikosini.Movement yake Kushuka kwenye Midfield,maana yake ilikuja ku Overload Midfield ya Everton.Ikawa ni Zinchenko, Jorginho/ Partey, Xhaka, Trossard vs Onana,Gana GUEYE na DACOURE.

Leandro Trossard pia Kuna Wakati alikuwa anabadilishana nafasi na Gabriel Martinelli, pembeni na katikati.Hii ilivuruga kabisa Muundo wa kuzuia wa Everton.Nafikiri Gabi Martinelli akicheza ndani kidogo na kuingia kwenye box anakuwa hatari zaidi kuliko kucheza kwenye mstari wa pembeni anakabika kwake urahisi.Na amefunga goli 2 Leo kufikisha goli 11 na assist 3

Nafikiri hii Plan ya LEANDRO TROSSARD Kwa team ndogo zinazopaki bus.Na Eddie ENKETIAH kwenye Mechi zile kubwa Kubwa itakuwa saafi tu

Note; Nia Yetu ni kukaa Kileleni Mpaka mwezi wa 5 halafu ubingwa mtaamua wenyewe wakumpa Kenge nyiee
IMG-20230302-WA0002.jpg
 
Naandika hapa kwa mara ya mwisho.

4 3 3 false 9 inahitaji wachezaji sahihi kwa sasa Arsenal hatuna CF wa kufit hapo zaidi ya Jesus, Nketiah hawezi anafaa kwenye 4 2 3 1. Bila Jesus 4 3 3 inatufanya tuwe dominant ila siyo constant threat.

Idea ya kumuweka Trossard au Martinelli kama CF ni sahihi kwakua hawa wawili wanalink up play vizuri kuliko Nketiah.

Hua mnatumia nini ili kuelewa?
Aliyekwambia Jesus anafaa Nan,unadhan pep mjinga alipokuuza uyo Jesus ,Jesus ni unpredictable player
 
Back
Top Bottom