Ukiona kitu ukikifikiria kichwani kinamake sense basi jua Arsenal hawatokifanya.
Una shida na kipa.
Unajiandaa kutumia 30M kumnunua Ramsdale.
Wakati kuna Mat Ryan na Onana unaweza kuwanunua wote kwa 7M. Ryan ameshatudakia msimu uliopita na ni kipa mzuri kusema kweli.
Lakini vinabo wanataka kutumia 30M kisa ati 'home grown'.
Unataka kumnunua Maddison kwa 65M.
Lakini Aouar ana asking price ya 25M na Odegaard ana asking price ya 35M na hapo odegaard unaweza kumnasa kwa mkopo. Kuna Renato ana asking price ya 23M.
Yaani kwa chini ya 70M unaweza kumpata Aouar, Renato na Odegaard.
Ukabakiwa na pesa ya kutafuta RB au kusubiri kiangazi na kipindi hichi kumpa namba Cedric na Bellerin.
Lakini Edu na genge lake hawafikirii hivi. Chochote ambacho wewe unaona mbona hii option inaokoa pesa na unapata ziada wao hiyo option ndiyo hata hawaiwazi.
Badala yake wako bize kuficha udhaifu wa uongozi wao kwa kutweet 'Trust the process' na kujisnap IG usiku wa manane wakidai wako bize na usajili.
Sijui kwamba ni hakuna pesa na hapa inapigwa kanyamazongo au vipi lakini kuna shida kubwa sana kuanzia kwa mmiliki mpaka yule bwana anayependa kumpa namba Chambers