Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Usiwe na expections kubwa mkuu. Huu msimu tuliyumba sana kuanzia ndani ya uwanja mpaka nje. Hakuna quick fix kwenye mpira.

Umesahau mashabiki walikuwa wanazomea wachezaji, nidhamu ilikuwa mbovu kupitiliza.

Tumpe lengo Arteta la kuingia msimu ujao salama. Aendelee kujenga timu. Msimu huu tuwe tayar na matokeo yote

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwa sasa wengi tunajua tunaanza upya next season ila shda nayoiona ni kuwa tumepishana point 6 pekee na Aston Villa ya 17 sasa na tabia hii ya sare sare na kiwango kushuka ni tatizo kwa EPL inabidi dawa itafutwe mapema sana hao ambao wapo chini ni wabaya sana mechi za mwisho na wengi hatujacheza nao na kuna ambao wanagombania top 4 pia bado hatujacheza nao ni hatari sana kwa timu mwanzoni hatukutegemea Leo mambo yatakuwa hivi ila kadri muda unavyoenda tusipobadilika na dawa kutafutwa mapema tutapishana point 3 na Norwich
ARTETA yeye ndo Mwalimu hii tabia ya sare sare itatuzamisha majini aiangalie mapema sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hata mimi najua Ceballos anauwezo kuliko Willock, wala sijapinga!.. Ila hija yangu ni kwamba kwa sasa mimi na wewe hakyna anaejua kiwango cha Ceballos kama ni kile tunachokihua au kashuka! Anaejua ni kocha na benchi lake la ufundi!.. Kwa kuwa sijui kinachosababisha anamuweka Ceballos benchi, itoshe kusema tu kocha kaona bado aendelee kukalia hilo benchi!.. Vipi kocha akimuanzisha halafu akaboronga kuliko hata Ozil, si tutaanza kulalamika hapa kuwa bora Ozil! Ninachoshauri ni kuwa tumuache kocha afanye kazi yake akiboronga atatimuliwa.. Kwa upande wa pepe bado ni kweli pepe ana kiwango hasa akiwa kwenye kiwango chake!.. Lakini kweli wewe hujui kuwa hao wanacheza position tofauti? Pepe ni winger na dogo ni Center forward, sasa sijui ulitaka pepe aingizwe aende akipige pale mbele, hapo mimi sijakuelewa!.. Bora ungelalamikia kitendo cha Martinell kucheza wing ya kulia, au ungesema pepe angeanza kulia, Auba kati na dogo akae pale kushoto!.. Lakini kwa kesi ya Nketia ni tofauti kidogo!.. Kocha alimwingiza Nketia ili kuforce goal maana kiuhalisia pale mbele kulikuwa na Auba, Laca, Martinell ambao wote ni washambuliaji nguli, sasa Lacazete kaflop na zimebaki dakika tano, sasa kama kocha unafanyaje? Unamtoa forward unaingiza forward! Huwezi kutoa forward halafu unaingiza Winger na unahitaji kushinda mechi!.. Kwa hiyo nia ya kocha ilikuwa njema!. Kwa kweli inakatisha tamaa, lakini titafanyaje na hao ndio wachezaji tulionao!.. Poleni wana Gunners lakini tusikate tamaa maana tuko kwenye transition, naamini timu itakaa vizuri soon!...

Sent using Jamii Forums mobile app

Kwa uelewa wangu licha sio kocha Pepe alitakiwa aingie dk hata ya 60 then laca aende nje na AUBA angekaa centre pepe kulia martinelli kushoto hili lilitakiwa lifanyike mapema sana
Nketiah jana hakustahili kuingia then pepe awe nje kama nlivyooanisha hapo juu Sema ARTETA kwa hili inabidi ajirekebishe la sivyo mambo yatakuwa magumu EPL kwa upande wa mashabiki na yeye mwenyewe cha kushukuru bado tupo top 10 ila tungepigwa jana nakwambia hata hizi kauli zingebadilika sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukiwaita watoto unawapa sifa kubwa.

WATOTO

1. Haaland - 19 Yrs
2. Ansu Fati - 17 Yrs
3. Sancho - 19 Yrs
4. Rodrigo - 19 Yrs

VILAZA

1. Willock - 20 yrs
2. Guenduz - 20 yrs
3. Kieran - 22 yrs
4. Nketiah - 20 yrs
5. Nelson - 20 yrs.

Sent using Cash Money Wings
Hapo katika vilaza ongeza

Mount
Odoi
Abraham
Tomori

Tafadhali

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sure. Mpira una mambo mengi, Arteta amekuja kujenga timu, mashabiki mnawaza kuingia top 4. Timu imeshajengeka sasa?

Msije na plan zenu za mfukoni. Arteta amekuta timu inakata roho, ghafla mnataka Mambo makubwa kwa muda mfupi. Timu haijengwi kwa mwezi mmoja wazee

Kwa sasa kuweni bega kwa bega na Arteta nafasi zipi zifanyiwe marekebisho, nani asajiliwe, nani auzwe na atolewe kwa mkopo. Mfocus kwenye plan za msimu ujao.

Timu imejaa matakataka mnataka kwenda UCL kwahiyo mnataka tena mkashikishwe ukuta na bayern munic.

Sent using Cash Money Wings
Kama wewe unavyoenda kuushika ukuta wa mererani hivi karibuni.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa uelewa wangu licha sio kocha Pepe alitakiwa aingie dk hata ya 60 then laca aende nje na AUBA angekaa centre pepe kulia martinelli kushoto hili lilitakiwa lifanyike mapema sana
Nketiah jana hakustahili kuingia then pepe awe nje kama nlivyooanisha hapo juu Sema ARTETA kwa hili inabidi ajirekebishe la sivyo mambo yatakuwa magumu EPL kwa upande wa mashabiki na yeye mwenyewe cha kushukuru bado tupo top 10 ila tungepigwa jana nakwambia hata hizi kauli zingebadilika sana

Sent using Jamii Forums mobile app
Nimeelewa hoja yako kaka!.. Ngoja tusubiri tuone hii mechi inayofuata hali itakuwaje!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimeelewa hoja yako kaka!.. Ngoja tusubiri tuone hii mechi inayofuata hali itakuwaje!

Sent using Jamii Forums mobile app
Halafu kitu kingine ambacho nakiona na hiki ni Wachezaji wenyewe ndo wanatakiwa kukifanya na kukiondoa ni kuwa sasa hivi tuna udhaifu mkubwa sana wa kimwili na kiakili kwa wachezaji na bahati mbaya sijui kwa nini wanashindwa kufight kuepukana na hali hii na NEWCASTLE na EVERTON wametupania wanajua huu muda timu imeyumba watakuja na spirit ya ajabu kama tutashindwa kupambana na kusema we are ARSENAL sisi ni BIG club itatuwia vigumu sana kupata matokeo mfano wapinzani wetu wote ni wachovu kama Mancity nae ni yule yule ndo maana kafungwa game 6 kama sisi ila utofauti wao na sisi wao huwa wanapambana na akianza kukufunga hutoki ila sisi karibia mechi 4 za EPL ukiacha ya CHELSEA ya marudiano chini ya ARTETA unakuta tunaongoza goli 1 ila mechi inaisha sare hapa ni Wachezaji kutambua thamani yao ila kila nkiangalia sijui kama watakuja kubadilika ngoja tusubiri hizo 2 next matches zinazokuja

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom