Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Asante bana, kilio cha wengi London (Arsenal, Spurs, Chelsea)---"harusi!"---
Jiji la Manchester ni furaha naona wiki hii kwao,na j5 wanakutana Manchester derbies na West London derbies(Chelsea vs Fulham)wiki hii hakuna hata timu 1 ya London imeshinda ktk ligi kuu ya England,kasoro fulham na west ham zimeambulia sare ktk mechi zao za mwishoni mwa wiki.
 
Walianza Albion na sasa Magpies, hizi timu zote ndio zimepanda tena daraja msimu huu zinatunyanyasa nyumbani?
Na nikikumbuka misimu ya nyuma akina Hull City nao walikuja Emirates na kuondoka na ushindi, hakuna heshima tena , sio intimidated ground kama ilivokuwa Highbury, Westham nao chupuchupu wajiondokee na pointi!!
Wenger na arudie formula ile ya zamani ambayo ilitupatia mafanikio,na turudie kusajili Wanaume, hivi vitoto havitoshinda kombe (labda Carling) tunahitaji wapiganaji kama walivokuwa The Invincible,akina Gilberto, Pires, Vieira, Ljunberg, Campbell, Parlour,Keown wote ni wapiganaji ambao kama ni urembo wanaweza na ukitaka vita poa vilevile, nakumbuka ile mechi Old Trafford Van Nistelrooy v Keown, Vieira v Keane, aah masikini timu yetu, eti akina Andy Caroll, Tiote na Ameobi wanakuja Emirates na kuweka authority?
kweli kbisa mkuu,tatizo hili miaka nenda rudi tunakosa plan b ya kushinda mechi kama hizi.

Sawa timu inaweka watu 10 golini,kwanini tunalazimisha kutembea na mpira kwenye nyavu wakati tunajua wamejaa ndani ya box? inama hatuwezi kujaribu vishuti vya nje ya kumi na nane? kwangu mimi hawa wachezaji ni wazembe kama hawawezi kutafuta plan b wakizidiwa kisa wenger kawaambia watembee na mpira mpaka ndani ya goli.

hatuwezi kuchukua kombe kama tutakuwa tunapoteza mechi kama hizi.
 
Sawa mkuu lakini Arsenal wakibanwa huwa hakuna jinsi.

Hakuna jinsi kwa vile tunatumia style hile hile tu na kutaka kulazimisha ifanye kazi badala ya kuwapa presha na mashuti ya mbali.mtu ndani ya box anataka kutoa pasi wakati ana nafasi nzuri tu ya kujaribu.wanakera sana mkuu.
 
One of the bad days in the office, if you listened to Arsene you will agree with him. Cesc, Van Perse, Walcott and Bendtner all coming from injuries aren't as sharp as they are supposed to be, but give them at least two weeks we will be flying. Cesc passes were allover just relax guys .. ... ....
 
ila wenzangu mbona angalau nyie kina arsenal,chelsea na man utd mpo ktk ushindani wa ubingwa,sasa mngekuwa washabiki tena wafurukutwa wa timu kama yangu ya Nottingham Forest ingekuwaje si mngekufa kwa ugonjwa wa moyo,BP ,Shell na Agip kabisa lol!
 
Hakuna jinsi kwa vile tunatumia style hile hile tu na kutaka kulazimisha ifanye kazi badala ya kuwapa presha na mashuti ya mbali.mtu ndani ya box anataka kutoa pasi wakati ana nafasi nzuri tu ya kujaribu.wanakera sana mkuu.

Hatuna Striker....Tunahitaji striker mmoja kama si wawili pale wenye nguvu mithiri ya Andy Caroll,Didier Drogba ama Wayne Rooney na si mlegevu na mviziaji kama Marouane Chamakh.......


Btw.....Salama wakuu?,habari za siku mingi.....Poleni na pilika pilika za............
 
Hatuna Striker....Tunahitaji striker mmoja kama si wawili pale wenye nguvu mithiri ya Andy Caroll,Didier Drogba ama Wayne Rooney na si mlegevu na mviziaji kama Marouane Chamakh.......


Btw.....Salama wakuu?,habari za siku mingi.....Poleni na pilika pilika za............

dah, ulipotelea wapi kaka? hukukutana na BAK huko?
Karibu tena, ...sie tupo, Kweli, Arsene Wenger, Baba Mkubwa na Kiongozi Wacha1 bado wanaendeleza mapambano ya kifikra hapa mpaka kieleweke kwa jamaa wa 'Darajani!'
 
Hatuna Striker....Tunahitaji striker mmoja kama si wawili pale wenye nguvu mithiri ya Andy Caroll,Didier Drogba ama Wayne Rooney na si mlegevu na mviziaji kama Marouane Chamakh.......


Btw.....Salama wakuu?,habari za siku mingi.....Poleni na pilika pilika za............

Welcome back tuliku-miss sana mkuu, btw last time ulikuwa bize kwenye kampeni vipi mulifanikiwa ama ndio mulichakachuliwa?:doh:
 
Huyo Chamack sijui kwa nini Wenger anamchezesha
 
One of the bad days in the office, if you listened to Arsene you will agree with him. Cesc, Van Perse, Walcott and Bendtner all coming from injuries aren't as sharp as they are supposed to be, but give them at least two weeks we will be flying. Cesc passes were allover just relax guys .. ... ....
Nakubaliana na sababu za Wenger kwamba ni vigumu kupata match fitness haraka na mchezaji anahitaji mechi walau 2 ili arudishe makali (sharpness) ila nahisi hizi excuse zimezidi, there is no excuse losing to WBA and Newcastle at home full stop.
Kama alivosema Wenger (huyu wa kwetu) tunahitaji plan B ili kukabiliana na staili ya 10 men behind the ball.
Hakuna sababu kwa nini Chamakh as a striker apokee pasi ndani ya box na bado apasie mwengine kwanini asifikirie ku-hit the target na sio kutoa pasi?
Nahisi ni theory ya Wenger, kwa sababu Arshavin hata Nasri game yao walipoanza ilikuwa different, walikuwa wanajaribu kupiga shuti hata nje ya box lakini naona wamebadilika.
Lazima tuwe na plan B ambapo midfield players tries attacking from outside the penalty box, Man Utd wao wanao akina Scholes na Gibson, Chelsea wanao Lampard na Essien, sisi hatuna jinsi ila tunangangania kupasua ndani ya box na ndio tunasumbuka endapo timu zinaweka watu 10 ndani ya boksi.
 
dah, ulipotelea wapi kaka? hukukutana na BAK huko?
Karibu tena, ...sie tupo, Kweli, Arsene Wenger, Baba Mkubwa na Kiongozi Wacha1 bado wanaendeleza mapambano ya kifikra hapa mpaka kieleweke kwa jamaa wa 'Darajani!'
Sishangai kwa kuelekeza mapambano yenu darajani, maana tumewafunika kwa muda mrefu sasa.....lol.
 
Huyo Chamack sijui kwa nini Wenger anamchezesha
Mtani naona unapita kutusalimu, vipi leo una matumaini ya ushindi? Chamakh mzuri mkuu na anajituma ila anahitaji mechi zaidi kwa sababu maamuzi yake bado sio fresh.
 
Naona amepiga kitu,hata hivyo bado mchovu tu
 
Hatuna Striker....Tunahitaji striker mmoja kama si wawili pale wenye nguvu mithiri ya Andy Caroll,Didier Drogba ama Wayne Rooney na si mlegevu na mviziaji kama Marouane Chamakh.......


Btw.....Salama wakuu?,habari za siku mingi.....Poleni na pilika pilika za............
Karibu sana mkuu.
 
Back
Top Bottom