Anne Semamba Makinda's Profile!

Anne Semamba Makinda's Profile!

Kwa kweli kuchaguliwa kwa huyu mama ni maafa kwa taifa. Anakana kuwekwa na mafisadi wakati huohuo anasema yeye hajui kama kuna mafisadi kwani kwa ufahamu wake fisadi ni mwanaume anayeiba mke wa mtu (nukuu ya gazeti la Mwananchi la leo). Tanzania ya leo tunahitaji Spika mwenye ufahamu wa kiwango cha chini kiasi hicho?
Sikutegemea huyu mama kusema maneno haya kwa wakati huu, hasa akiwa amechaguliwa kama speaker wa bunge. Hili linanipa shaka katika ufanisi wake wa kazi, kwani ameanza vibaya kwa kutumia siasa za maji taka.

Wote tunajua kuwa suala la kuongelea kuhusu 'wizi wa mke wa mtu' ni nini na linamlenga nani. Ni maji taka hayohayo ambayo yalitumiwa na viongozi wa ccm dhidi ya Dr. Slaa wakati wa kampeni za uchaguzi. Kwa hili tunaweza kusema kwel kama atafanya kazi yake vizuri? Leo hii hakuna haja ya kutafuta maana ya neno 'fisadi'. Kila mtu anajua hata mtoto wa darasa la 3 anajua.

Kwa kutamka hivyo hadharani, ameuhakikishia umma wa Kitanzania kuwa amewekwa pale kuetetea hoja za mafisadi, hakuna mjadala zaidi. Kama yeye alikuwa halijui hilo, basi imeliwa kwake!
 

- Mkuu matokeo ya uchaguzi yako very clear kwamba wananchi wengi sana wamemuadhibu Rais kwa hayo makosa ya kwenye kampeni, kuna mahali nimesema kwamba Rais anahitaji kuwafukuza kazi maramoja wale wote waliomshauri kwenda kwenye majimbo ya wagombea wanaotuhumiwa kuhusika na corruptions, kwamba haikuwa lazima aende kwenye hayo majimbo na pia haikuwa lazima wagombea hao wawepo kwenye kampeni za Rais, ninaamini matokeo yamemfahamisha Rais na CCM kwa ujumla kwamba hatuwezi kuwa-take wananchi for granted kama zamani.

- Again my point ni kwamba ninafahamua standing za Mama Makinda, kuanzia kwenye CC na ndani ya bunge, na kuchaguliwa kwake ni lazima kuwepo na mkono wa Ikulu, sasa why would Ikulu support her to be a Speaker kama hawana nia ya mabadiliko na hasa kuyasikiliza matokeo ya uchaguzi wa juzi na knowing huyu mama standing? Ndipo ninaposema kwamba ninaamini kwamba huenda kuna mabadiliko makubwa yanakuja ni imani yangu tu, looking at political facts at hand.


William


Mkuu kama kuchaguliwa kwa Anne Makinda kuwa spika kuna mkono wa Ikulu basi kwa lugha nyepesi kabisa bila kuzungusha mdomo ni kusema kuchaguliwa kwake kuna mkono wa mafisadi.
Kila mmoja anafahamu jinsi JK alivyo na mafungamano na mafisadi papa sasa tena unatuzuga eti mafisadi walimtaka Anna Abdallah? hapana bana acha hizo. As long uchaguzi wa spika Makinda ulikuwa na mkono wa ikulu basi uchaguzi wa spika ulikuwa na mkono wa mafisadi, wala hatuhitaji longo longo juu ya hilo pamoja na kwamba uko karibu na ikulu.
 
- Mkuu ninaomba kutofautiana na wewe respectively kwamba mafisadi will never let this woman to be a Speaker maana wametumia mbinu chafu sana kujaribu kumzuia asirudi bungeni, unless tukiulizana mafisadi ni nani! Mimi ninaamini sana kwamba huu ulikuwa ni uamuzi wa Ikulu kitu ambacho kinaninfanya niamini kwamba kuna mabadiliko makubwa sana yanakuja na term ijayo, mkuu ninaomba nikuhakikishie kwa Miungu yangu yote ni kwamba mafisadi ninaowajua wametumia kila njia kuhakikisha huyu mama harudi bungeni na jana wameumia sana kuona anakuwa Spika.

- Chaguo lao mafisadi lilikuwa Mh. Anna Abdallah, na Mh. Kate Kamba siku zote ni chaguo la Wazee Butiku na Warioba.


William.


mkuu sijakusoma vizuri hapo unaweza kutoa ufafanuzi kidogo? i mean ufisadi na Butiku na Warioba inakuwaje hapo?
 
Mkuu kama kuchaguliwa kwa Anne Makinda kuwa spika kuna mkono wa Ikulu basi kwa lugha nyepesi kabisa bila kuzungusha mdomo ni kusema kuchaguliwa kwake kuna mkono wa mafisadi.
Kila mmoja anafahamu jinsi JK alivyo na mafungamano na mafisadi papa sasa tena unatuzuga eti mafisadi walimtaka Anna Abdallah? hapana bana acha hizo. As long uchaguzi wa spika Makinda ulikuwa na mkono wa ikulu basi uchaguzi wa spika ulikuwa na mkono wa mafisadi, wala hatuhitaji longo longo juu ya hilo pamoja na kwamba uko karibu na ikulu.

- Mkuu siko karibu na mahali popote isipokuwa niliyoyasema ni mtizamo wangu kuhusu matokeo ya uchaguzi kuanzia wa taifa mpaka huu wa Spika, na wewe uko entitled na mtizamo wako, wangu uko based only na facts za matokeo ya uchaguzi na understanding siasa zetu bongo kwamba Spika hawezi kuchaguliwa toka chama tawala bila ridhaa ya Ikulu,

- Otherwise wako pia ni mtizamo wako on the ishu at hand na wala hakuna tatizo ni wananchi wanaosoma ndio wataamua upi unaweza kuwa muelekeo halisi wa kinachoendelea.


William.
 
uyo mama SIYO MNYALU, msiharibu kabila la watu bure. huyo mama ni MBENA yaani from bena tribe. wabena wanatoka wilaya ya njombe, wilaya ya iringa mjini na vijijini na kilolo ndo kuna wahehe, wilaya ya Ludewa wapo WAPANGWA, wilaya ya Makete wapo wakinga na wawanji...Mufindi wapo wahehe. huyu mama ni mbena na ni mkabila vibaya mno...anapendelea sana wabena. katika list yao, wapo yeye, Luhanjo, Deo yule mbunge aliyekuwa lawyer wa Barick, mkuu wa mainjinia hapa tz, kina makweta etc. kuna siku nilishawai kuhudhuria graduation moja hivi waliifanya pale mabibo mimi nilijifanya mbena mwenzao, nilichoshuhudia ni kwamba tz ukabila upo mkubwa sana underground.

Huyo mama ndiye aliyeipigania sana njombe hadi kuomba kuanzishwa kwa mkoa mpya wa Njoluma/njombe ili kujing'oa kwenye mkoa wa wahehe, hivyo yeye hatoki tena iringa, anatoka mkoa wa njoluma/njombe. kama kuna mtu mwenye swali uliza.
 
- Mkuu ninaomba kutofautiana na wewe respectively kwamba mafisadi will never let this woman to be a Speaker maana wametumia mbinu chafu sana kujaribu kumzuia asirudi bungeni, unless tukiulizana mafisadi ni nani! Mimi ninaamini sana kwamba huu ulikuwa ni uamuzi wa Ikulu kitu ambacho kinaninfanya niamini kwamba kuna mabadiliko makubwa sana yanakuja na term ijayo, mkuu ninaomba nikuhakikishie kwa Miungu yangu yote ni kwamba mafisadi ninaowajua wametumia kila njia kuhakikisha huyu mama harudi bungeni na jana wameumia sana kuona anakuwa Spika.

- Chaguo lao mafisadi lilikuwa Mh. Anna Abdallah, na Mh. Kate Kamba siku zote ni chaguo la Wazee Butiku na Warioba.


William.

Mkuu umechukua dhamana kubwa sana hapo. Kwa kweli naomba uhai na afya njema tu nishuhudie huo "muujiza". Manake wengine imani ilishatutoka kitambo sana.
 
Kaka kuna mijadala mingi mimi personal nimeandika kwamba Sitta is opportunist who happened to take our side. Sitta kajenga lile jengo kule kwako for what money? Sitta ni mwizi, plane and simple.

Now jee mama Makinda anatufaa? The answer is simple no. The women didn't achieve any substantial achievement that you can pin point despite being in the Bunge for over 35 years. Hii ni recycle ya GIGO za CCM......

Mtanganyika
Mimi siku zote nimekuwa naeleza kuhusu huyu opportunist Sitta na ninakubaliana na wewe kabisa, na kwa huyu mama, again hamna cha maana zaidi ya party politics atakazofanya bungeni, kamati na maamuzi ya kamati kwa kwenda mbele, nakuhakikishia atajitahidi tu kuhakikisha kuwa wapinzani hawaongei au kuuwa hoja zao bungeni na hakuna zaidi.
 
Mtanganyika
Mimi siku zote nimekuwa naeleza kuhusu huyu opportunist Sitta na ninakubaliana na wewe kabisa, na kwa huyu mama, again hamna cha maana zaidi ya party politics atakazofanya bungeni, kamati na maamuzi ya kamati kwa kwenda mbele, nakuhakikishia atajitahidi tu kuhakikisha kuwa wapinzani hawaongei au kuuwa hoja zao bungeni na hakuna zaidi.

Ukitaka kumjua Sitta, fuatilia record yake CDA na TIC. Ni mwizi aliyevaa ngozi ya kondoo.

Mmesahau dawa za milioni mbili? Mmesahau ofisi ya Spika kule kwao?

Ni sawa alikuwa upande wa wananchi kwenye suala la ufisadi sio kwasababu yeye mwenyewe anapinga ufisadi kwa matendo bali kwasababu hao mafisadi walikuwa ni maadui zake kisiasa.
 
- Ni mchapa kazi asiyependa mchezo hata kidogo, infact huyu ni nightmare ya mafisadi wanajua sana na the fact kwamba amechaguliwa inaweza kwua dalili za mabadiliko makubwa sana katika uongozi wa Term ya pili ya Awamu ya nne, ni mpenda haki na mfuatilaji wa details za ishus, hivi karibuni alikuwa DC kwenye semina ya uongozi bora aliniambia kufurahishwa sana na system ya uwajibikaji kwa viongozi ya huku USA, Wapinzani bungeni wakiwa makini bila mapepe atawasaidia sana as long wanapeleka ishus zenye uhakiika na hasa FACTS,

- Mkuu hivi ndivyo ninavyomjua Mama Makinda kuhusu masilahi ya taifa!
na kwamba hata kurudi kwake bungeni ilikuwa kazi kubwa sana na ya ziada sana!

William.

Writing style kama ya Field Marshal ES. Not implicating you though, kufanana siyo kosa.
 
Kwenye moral value hazina uhusiano katika kuchapa kazi kama mtu ni commited kwenye kazi na yuko fair. Kuna watu wangapi ambao kwenye moral value unweza kuwapa 99.9% lakini kwenye kazi hovyooooo na wale ambao maral value unaweza kuwa 30% lakini kwenye kazi ana-score 99.9% kama vile Rais wa Marekani wa zamani Bill Clinton.

Mimi nafikiri kiongozi yeyote tum-evaluate kwa utendaji kazi na si kwa ametemmbea na wangapi au na nani kimapenzi

Mheshimiwa boma;

Kuna magonjwa kwa mamia ambayo ni MORAL VALUE - BASED!! ..hata Ukimwi weneyewe ni moral value related.. Its very important kwa kiongozi ku observe moral supiriority kama mtindo wa maisha ..vingine atasimama vipi mbele ya majukwaa kwa kampeni mbalimbali?
 
Mtoto wa Anna atakuwa mkubwa kuliko huyo Neema. Neema atakuwa ni mtoto wa mke ambaye Prof alimuoa baada ya kuzaa na Anna. Watoto wa Prof kwa mke huyo wamesomea South Africa. I remain to be corrected .

uko sawa.
 
- Mkuu siko karibu na mahali popote isipokuwa niliyoyasema ni mtizamo wangu kuhusu matokeo ya uchaguzi kuanzia wa taifa mpaka huu wa Spika, na wewe uko entitled na mtizamo wako, wangu uko based only na facts za matokeo ya uchaguzi na understanding siasa zetu bongo kwamba Spika hawezi kuchaguliwa toka chama tawala bila ridhaa ya Ikulu,

- Otherwise wako pia ni mtizamo wako on the ishu at hand na wala hakuna tatizo ni wananchi wanaosoma ndio wataamua upi unaweza kuwa muelekeo halisi wa kinachoendelea.

William.
William asante kwa maelezo mengi uliyotoa kuhusu Anna, japo kuna maswali mengi watu bado yapo vichwani mwao na pengoine Anna will prove us wrong,
Lakini kwangu mimi ni kubwa ni moja na ambalo linanifanya nishindwe kuoanisha most of dots and details you have provided nalo ni kwamba Anna hakuwa chaguo la mafisadi na kwamba walipambana naye sana asirudi bungeni lakini wameshindwa. Swali langu mimi kubwa ni moja, mimi natoka Njombe na bahati nzuri najua kidogo upepo ulivyokuwa huko.
Anna alipita bila kupingwa katika mchakato wa ubunge na hivyo ilikuwa kazi rahisi kwake kusonga mbele, sasa hiyo nguvu ya ziada ilihitajika wapi naomba unieleweshe mkuu
 
William asante kwa maelezo mengi uliyotoa kuhusu Anna, japo kuna maswali mengi watu bado yapo vichwani mwao na pengoine Anna will prove us wrong,
Lakini kwangu mimi ni kubwa ni moja na ambalo linanifanya nishindwe kuoanisha most of dots and details you have provided nalo ni kwamba Anna hakuwa chaguo la mafisadi na kwamba walipambana naye sana asirudi bungeni lakini wameshindwa. Swali langu mimi kubwa ni moja, mimi natoka Njombe na bahati nzuri najua kidogo upepo ulivyokuwa huko.
Anna alipita bila kupingwa katika mchakato wa ubunge na hivyo ilikuwa kazi rahisi kwake kusonga mbele, sasa hiyo nguvu ya ziada ilihitajika wapi naomba unieleweshe mkuu


- Kwenye siasa za kisasa hakuna kuchaguliwa bila kupingwa kama kweli unatokea jimboni kwake, then ulipaswa kujua mengi yaliyotokea huko katika kujaribu kumzuia asirudi bungeni, mtu anayechaguliwa bila kupingwa hawezi kutumia muda mwingi sana jimboni wakati wa uchaguz,hope nimekusaidia.


William.
 
Nitajibu maswali mawili hapa.

Nimefanya kazi na Anna Wilson Makinda miaka ya 1980s, namjua kidogo. Nimewahi kufika kwao wakati baba yake alikuwa hai, na pia mara moja baada ya baba yake kufariki miaka ya 1990s. Baba yake aliwahi kuwa mkuu wa mikoa kadhaa, nakumbuka Tabora, Ruvuma, Tanga, wakati wa Mwalimu JKN.

Anna hajawahi kuolewa, na wala hana mume sasa. Ana mtoto mmoja wa kike, alizaa na Bwana mmoja (nadhani jina ni Ndunguru) ambaye alikuja kuwa Prof pale SUA. Nadhani ni mtu wa Songea au Ruvuma.

Last time kuonana naye, aliniambia binti yake yuko Marekani na kaolewa na mtu wa huko (siyo m-Tanzania), ila hakusema kama ni mzungu au mweusi. Na mimi sikuuliza.

Anna hana CPA lakini ni trained Auditor na ni mzuri sana katika hiyo kazi.

Ni dada mmoja mwenye heshima sana, uelevu na si msahalifu, hiyo ni ki-binafsi.

Ki-siasa ana mtazamo na msimamo mwingine ambao wakati mwingine unaweza kukuacha unakuna kichwa.

Namtakia mafanikio mema, na nina imani hii kazi ataiweza vizuri tu.

Ana mtoto mwingine wa kiume....namfahamu fika mkuu lete data za uhakika.
 
uyo mama SIYO MNYALU, msiharibu kabila la watu bure. huyo mama ni MBENA yaani from bena tribe. wabena wanatoka wilaya ya njombe, wilaya ya iringa mjini na vijijini na kilolo ndo kuna wahehe, wilaya ya Ludewa wapo WAPANGWA, wilaya ya Makete wapo wakinga na wawanji...Mufindi wapo wahehe. huyu mama ni mbena na ni mkabila vibaya mno...anapendelea sana wabena. katika list yao, wapo yeye, Luhanjo, Deo yule mbunge aliyekuwa lawyer wa Barick, mkuu wa mainjinia hapa tz, kina makweta etc. kuna siku nilishawai kuhudhuria graduation moja hivi waliifanya pale mabibo mimi nilijifanya mbena mwenzao, nilichoshuhudia ni kwamba tz ukabila upo mkubwa sana underground.

Huyo mama ndiye aliyeipigania sana njombe hadi kuomba kuanzishwa kwa mkoa mpya wa Njoluma/njombe ili kujing'oa kwenye mkoa wa wahehe, hivyo yeye hatoki tena iringa, anatoka mkoa wa njoluma/njombe. kama kuna mtu mwenye swali uliza.

Agreed!ni mbena na ukabila wanao ndio haohao pamoja na kina Makweta, Thomas Nyimbo wote ni wabena na sio wahehe!
 

- Mkuu heshima sana, labda kwanza tungejadili hivi nani amewahi kuwa Spika mzuri toka tupate uhuru, au tumjadili Spika yoyote yule Africa na Dunia nzima, then tuangalie kama huyu mama anazo hizo sifa, maana sijui Mwalimu wakati anakuwa Rais wakati tunapta uhuru alikuwa amewahi kuwa Rais mahali popote pale, Spika anaweza ku-accomplish nini akiwa Spika bungeni ndio maswali magumu ya kujiuliza na Spika anawezaje kua mzuri au mbaya?

- Siamini kwamba Spika mpya anaweza kuwa judged na mafanikio ya uongozi wa alikotoka kabla ya kuwa Spika, halafu usisahau kwamba at the end of the day huyu ni Spika wa CCM, aliyechaguliwa na CCM kulinda na kuendeleza ilani na sera za CCM !


William.

Ndg William,

Ni wazi kabisa Tanzania ya mwaka 1961 sio Tanzania ya leo. Nakubaliana na wewe kabisa kwamba Mama Makinda ni spika wa CCM na amechaguliwa kuendeleza policy za CCM. Hapo kwa watu wenye ueleo tunafahamu kabisa kwamba kanzu ndio mpya lakini shekh ni yule yule. Ukweli ni kwamba hakuna kipya tutakacho kiona kwa huyu mama. Tusahau mchakato mzima wa kubadilisha vifungu kibao vya katiba na mambo mengine.

Mabishano yangu ni kwa wale wanao tetea kwamba huyu mama ni substantial leader. Kusema kweli hakuna hata mmoja aliyekuja hapa akasema kwamba wakati huyu mama akiwa body ya Mwatex alihoji matumizi mabaya ya xxx or wakati huyu mama akiwa naibu waziri fulani alihoji kadha wa kadha.

Mwisho kama huyu mama ameshindwa kufanya mabadiliko katika sekta zote alizofanya kwa miaka 35, jee atabadilisha mfumo wa bunge kwa miaka 5? I doubt.
 

1268.jpg



GENERAL
ID No.: 1268
Salutation: HONOURABLE
First Name: Anne
Middle Name: Semamba
Last Name: Makinda
Member Type: Constituency Member
Constituent: Njombe Kusini
Political Party: CHAMA CHA MAPINDUZI
Office Location: P.O. Box 38, Njombe
Office Phone:
Office Fax: 2112538
Office E-mail: amakinda@parliament.go.tz
Member Status: Current Member
Start Date:
End Date:
Date of Birth 15 July 1949

EDUCATIONAL HISTORY
School Name/Location Course/Degree/Award Start Date End Date Level
Institute of Development & Management - Morogoro Administration Course 1971 1975 ADV DIPLOMA
Kilakala Girls' Secondary School(Marian College) A-Level Education 1969 1970 HIGH SCHOOL
Masasi Girls' Secondary School O-Level Education 1965 1968 SECONDARY
Peramiho Girls' Middle School Primary Education 1961 1964 PRIMARY
Uwemba Primary School Primary Education 1957 1960 PRIMARY

EMPLOYMENT HISTORY
Company Name Position From Date To Date
- Regional Commissioner 1995 2000
Ministry of Community Development, Women Affairs and Children Minister 1990 1995
State,Prime Minister's & First Vice President Office Coordination of Union Matters 1983 1990
State,Prime Minister's & First Vice President Office In charge of Central Government Coordination 1983 1990
Tanzania Government In charge of Information and Broadcasting 1983 1990
State,Prime Minister's & First Vice President Office Minister 1983 1990
National Bank of Commerce Board Member 1978 1983
Surveyors Building Contractors Consultants Board Member 1978 1983
Tanzania Railways Corporation Board Member 1977 1983
Tanzania Legal Corporation Board Member 1977 1983
Mbeya Textile Company Board Member 1977 1983
National Textile Company Board Member 1976 1983
Tanzania Elimu Supplies Board Member 1976 1983
The Public Accounts Committee of the Parliament Member 1975 1983
Tanzania Audit Corporation Auditor 1975 1976
The Institute of Development Management-Mzumbe Board Member 1971 1976

POLITICAL EXPERIENCE
Ministry/Political Party/Location Position From To
CCM-Chama Cha Mapinduzi Member of National Executive Council 1977 Todate
TANU/CCM-Chama Cha Mapinduzi Ten Cells Leader 1975 1983
TANU Chairman -Youth League-IDM, Mzumbe 1971 1975
TANU Chairman -Youth League-Kilakala 1969 1970
TANU Chairman of Youth League 1965 1968

Hiyo advanced diploma ilikuwa inachukua miaka minne au mitatu? Kuna repeat a year nini hapo?
 
sio uongo....huyo kijana jina lake aliitwa maurice ....ni mtoto wa anna makinda banaa alisomea arusha.

Anna Makinda ana mtoto mmoja tu wa kike, na ndiyo anavyojieleza mwenyewe. Hakuna mwanamke anayekana mwanae. Tungekuwa tunazungumzia mwanaume hapa ningefikiria mara mbili kuwa huenda kuna mahali alipitia na anataka iwe siri kwa mkewe, lakini wanawake huwa hawafichi wala kukataa watoto wao. Ana mtoto mmoja tu huyu mama.
 
Back
Top Bottom