1.
- Mwalimu hakupenda kuona watoto wake wanatajirika, huo ni uongo wa mchana, kama unaamini ni ukweli weka source yake mkuu!
2.
- Ni wapi uliposoma ambapo Mwalimu alisema hataki watoto wake kujilimbikizia mali? Na ni wapi ambapo hakutaka viongozi wake kutojilimbikizia mali? Mwalimu alichokuwa hataki ilikuwa ufisadi kujilimbikizia mali kwa ufisadi, lakini sio kwa njia za halali, hebu nitajie m-Tanzania yoyote unayemjua aliyekuwa na utajiri wake under Mwalimu na akamnyanga'anya mali zake bila sababu?
- Mzee Mbowe hakuwa tajiri wakati wa Mwalimu? Ndesamburo hakuwa tajiri under Mwalimu? Mzee Kanyamala hakuwa tajiri under Mwalimu? Kurgisi hakuwa tajiri under Mwalimu? Komanya hakua tajiri under Mwalimu? Mengi hakuwa tajiri under Mwalimu? Sasa kama alikuwa hataki wananchi kujilimbikizia mali ilikuwaje akawaacha hawa? Sasa what is your point kuhusu watoto wake? Ni lini uliwahi kusikia mtoto wake mmoja amekwua tajiri akamnyanga'anya mali zake?
- Hivi unajua kua Mwalimu akiwa kwenye power mtoto wake Madaraka, alikuwa akimiliki malori ya mchanga mengi tu, na kwamba Magige alikua ni Engineeer mkubwa sana kiwanda cha Sukari Kilombero tena akila kuku zake ile mbaya sana! Na kwamba Anna alikuwa Italy akisoma na kuishi huko kwa muda mrefu sana! Rosemary akaja kuwa mbunge wa kupewa na Mkapa, Makongoro akawa mbunge na sasa ni Mwenyekiti wa CCM Musoma, sasa ni nini kosa la Mwalimu hapa? Wewe huwezi kuona kwamba hapa ndipo uwezo wa akili zao kimaisha zilipoishia, sasa Mwalimu ulitaka afanye nini?
3.
- Elimu kubwa inatakiwa kuku-guarantee maisha mazuri au utajiri, sasa kama huna akili za darasani basi uwe na akili za maisha, kama huna zote hakuna msaaada na hakuna wa kulaumiwa, wewe ulitaka Mwalimu afanye nini hasa? Achukue hela hazina awape ndio ungefurahi? Kama hawana akili ya kuzitunza then what?
4.
- Ulitaka Mwalimu awape madaraka watoto wake are you serious au unatania? Mkapa si aliwapa then what happened? Yaani mkuu kilio chako chote hapa ni kwa sababu ulitaka Mwalimu awape madaraka watoto wake bila sababu kwa kuwa yeye ni rais tu?
5.
- Hapa unasema nini eti watoto wa Mwalimu walikuwa hawapewi hela za matumizi ndio maana leo hawana maisha mazuri? I s that so? Hela za matuimizi kwa watoto ndio guarantee ya maisha mazuri wakikua? Hebu rudia tena hii point mkuu!
6.
- Wewe mkuu ndio hujui source ya unachokiongea, je unawafahamu vizuri hawa watoto wa Mwalimu, au na wewe unarukia tu habari za mtaani? Madaraka alioa mtoto wa waziri mmoja then Mageni, ambaye alikua Hotel Manager pale Twiga Hotel huyu demu alikua opportunists na wote pale mjini tulikuwa tunamshitukia jamaa yangu akaupanda mkenge akaishia kuachwa malori yote miguu juu, sasa wewe unasema ninaongea habari za mtaani wakati ninaongea habari nilizozionai, sasa kama huyajui si uulize, hao kina Magambo, Steven Kiboko, Milton na Matare wanaokula kuku sasa hivi kwa jina la Mwalimu wewe unawafahamu mkuu? Huna hoja hapa mkuu!
7.
- Sasa eti unasema kwamba watoto wote waliopewa malezi mazuri na wazazi wao duniani ndio peke yao wanaokula kuku? Una maana wananchi wote walioko kwenye majela ni kwa sababu hawakupewa malezi mazuri na wazazi wao? Mbona mkuu huna hoja?
8.
- Good point, sasa ilikuwaje ndugu wa pembeni wa Mwalimu wakalitumia jina na kutajirika wakati watoto wenyewe wakishindwa? Unasema hili ni kosa la Mwalimu? Utamlinganisha Bush aliyekua akimiliki timu ya Baseball ya Texas Rangers na watoto wa Mwalimu aliyekua hamiliki anything? Watoto wa Mwalimu walikwua na kila kitu on their hands ni matatizo yao wenyewe wakashindwa kutumia nafasi, DK. Hussein asingesota Turkey leo asingekua waziri period.
Respect.
FMES