Andrew Nyerere on Mwalimu humble children!

Andrew Nyerere on Mwalimu humble children!

really?

And this will warrant a corresponding toe to toe... with dyslexia coherent critical thinking?!!!?


bwa ha hahha haha haaa ha ha .... priceless..... and yet you call 'em Nyereres - zombies?!?!

bwa ha ha haha bwa ha hahh

Dyslexia persists, myopic dyslexia at that.
 
Bluray una pointi ila maneno unayotumia ndio makali,maneno kama zombies nk...Usiielezee familia kwa chuki bali chambua tu kwa maslahi ya historia ya Taifa letu,na definetly makosa tuliyoyafanya ili tusiyarudie.
Ni kweli mwalimu alikuwa hana time na watoto,sasa mwenye kubisha hilo ni lazima aje na pointi za kupingana na hoja za Bluray, isipokuwa Bluray ni muhimu ujaribu kutumia maneno ambayo hayatakuwa ya kuidhalilisha familia.
 
Nilichokipata katika thread hii ni kuwa bado watu wanaamini kuwa shida ni mwalimu wa yote na shida ni uaminifu.
 
Andrew Nyerere ni mimi Ganesh.
Mkuu yamezungumzwa mengi humu nadhani wewe unaweza kuwa na majibu ya kutosha pamoja na kwamba wengi wamekuwa na chuki na mwalimu hadi familia yake.. sababu sizifahamu.

Mimi nakumbuka vizuri miaka ya 70 nilikuwa nikikutana sana na watoto wa mwalimu pale Upanga kwa marehemu Mama Mtebe..Pia kuna jamaa zangu walifanya kazi Ikulu wakati huo kina Mama Specy wote walizungumza mazuri tu kuhusu mwalimu na wanawe..

Ni kweli kabisa Nyerere alitakiwa kufanya mengi sana lakini tunasahau tu kwamba miiko ya Ujamaa ni pamoja na kiongozi kuishi maisha tofauti sana na wananchi wake. Kiongozi anatakiwa kuwa mfano wa maisha anayotaka kuyaandaa kwa wanawe, tofauti na maisha ya Kibepari.
Mnakumbuka pia enzi zetu mzee akiwa mgumu sana tulikuwa tukimwita Mjamaa.. Haijalishi kama mzazi alikusudia kuweka akiba ili apate kujenga nyumba au kununua trekta, sisi tulichukulia Ujamaa kama ni uzito wa matanuzi..

Kwa hiyo wakuu zangu sidhani kama mnamtendea haki mwalimu ambaye alikubali kuiweka familia yake ktk hali ambayo angeweza kabisa kuibadilisha kwa siku moja..Na sidhani kama kati yetu mna furaha mioyoni mwetu mnapomwona Mwinyi na Mkapa wakiwarithisha watoto na wajukuu zao majumba na mali ambayo hawakuichuma..Na sidhani kama hiki ndicho kipimo cha uongozi bora ua familia bora...
Isipokuwa kama kawaida yetu sisi - Waaafrika ndivyo Tulivyo..kila issue ni lazima iwe na mtu wa kuzungumziwa..
We TALK about people!
 
Bluray una pointi ila maneno unayotumia ndio makali,maneno kama zombies nk...Usiielezee familia kwa chuki bali chambua tu kwa maslahi ya historia ya Taifa letu,na definetly makosa tuliyoyafanya ili tusiyarudie.
Ni kweli mwalimu alikuwa hana time na watoto,sasa mwenye kubisha hilo ni lazima aje na pointi za kupingana na hoja za Bluray, isipokuwa Bluray ni muhimu ujaribu kutumia maneno ambayo hayatakuwa ya kuidhalilisha familia.

- Mwalimu did everything he could asingeweza kwenda madarasani kuwafanyia mitihani watoto wake, kwani wazazi wa Mwalimu walimfanyia nini cha ajabu mpaka akafikia elimu au nafasi aliyokuwa nayo katika taifa?

- Mambo kama haya tunamsingizia tu bure Mwalimu, sikubaliani na ideas nyingi za Mwalimu, lakini hili la watoto wake sio lake ni lao wenyewe yaani watoto, hawakuchangamka na hakuna wa kumalaumu isipokua wao wenyewe!

- Magige ni Electrical Engineer tena wa Mlimani ya enzi hizo, by now alitakiwa awe Chief Engineer mkubwa sana mahali, elimu anayo, jina analo, lakini anachofanya sasa hivi hata sielewi, Madaraka alikuwa mtu babu kubwa malori wka wingi ya kupewa na Mama, akadanganyika na yule demu mtoto wa Mageni na yeye miguu juu, sasa eti bado wa kulaumiwa ni Mwalimu, acheni hizo wakuu hebu mpeni pumzi Mwalimu kidogo huko kaburini, Mkapa amejaribu weee kuwasaidia lakini hawasaidiki hawa!

FMES!
 


..ya unasema ni lunatic ambao hawaku miss target wakarusha mizinga sokoni au stendi ya basi wakadondosha bumu ...kwa ndege..kaaz kweli kweli!!!

....tembelea pale lugalo na wengine wapo vijijini ukawaone askari ambao hadi leo wanatembelea wheel chairs .......kutokana na madhara ya medani...

women..maisha ni duara...nadhani bila shaka kijana mtanashati ,msomi tena pilot miaka ya 70"s....ambaye hakuwa na matatizo ..atakuwa waliopoa vifaa vya nguvu ,wakaowa na kuzaa watoto........,kwa waafrika ni aibu kwa mwanamke kuzeekea nyumbani...lakini kwa mtoto wa kiume mazingira yakimruhusu au kumlazimisha kuolea na kuzeekea kwenye moja ya mji wa mzee wake ..hiyo ni ruksa....yupo kwake!!!!

hawa wanao watoto ....nadhani wako vizuri tu ..wanasoma ndani na nje ya nchi!!!..sina taarifa kamili juu ya hili...labda FMES anaweza kusaidia details hapo!

Mkuu PM, samahani sana nilikuwa sijaiona hii topic, pole sana mkuu naona unabishana na wasioelewa vizuri ukweli,

- Ni kwamba Mwalimu aliwapeleka watoto wake shule kama vile wazazi wetu, sasa kilichojalisha zaidi ilikuwa either akili ya maisha au ya shule, watoto wa Mwalimu hawakuwa na vyote sio siri kwa wale tunaowafahamu, sasa what else Mwalimu alitakiwa kufanya? Hivi unafikiri DK. Hussein asingesota na shule kule Turkey sasa hivi angekua waziri? Hivi unajua maisha ya Turkey yalivyo mkuu kwa mtoto wa rais kusoma kule mpaka kua Doctor?

- Hebu tizama watoto wa Joseph, yaani Matare na Milton, hawa walikuwa na akili ya shule na maisha pia, sasa hivi hawalali njaa na wala hawana shida, pamoja na kwamba wao ni Joseph tu, sasa ndio iwe Mwalimu?

- Watoto wa Mwalimu ni wa kulaumiwa wenyewe and they know that, wewe tizama mtu kama Magambo alivyotajirika kwa jina la Mwalimu na ni ndugu tu, the real Mwalimus wanasota eti wa kulaumu ni Mwalimu? Steven Kiboko anakula kuku ile mbaya tena longtime, na yeye ni Kiboko tu sasa ndio iwe watoto wa Mwalimu?

Mwalimu kwenye watoto wake hana lawama kabisaa, ni noma lao wenyewe!

FMES!

 
- Mwalimu did everything he could asingeweza kwenda madarasani kuwafanyia mitihani watoto wake, kwani wazazi wa Mwalimu walimfanyia nini cha ajabu mpaka akafikia elimu au nafasi aliyokuwa nayo katika taifa?

- Mambo kama haya tunamsingizia tu bure Mwalimu, sikubaliani na ideas nyingi za Mwalimu, lakini hili la watoto wake sio lake ni lao wenyewe yaani watoto, hawakuchangamka na hakuna wa kumalaumu isipokua wao wenyewe!

- Magige ni Electrical Engineer tena wa Mlimani ya enzi hizo, by now alitakiwa awe Chief Engineer mkubwa sana mahali, elimu anayo, jina analo, lakini anachofanya sasa hivi hata sielewi, Madaraka alikuwa mtu babu kubwa malori wka wingi ya kupewa na Mama, akadanganyika na yule demu mtoto wa Mageni na yeye miguu juu, sasa eti bado wa kulaumiwa ni Mwalimu, acheni hizo wakuu hebu mpeni pumzi Mwalimu kidogo huko kaburini, Mkapa amejaribu weee kuwasaidia lakini hawasaidiki hawa!

FMES!

FMES, Taratibu....Ni muhimu uelewe msingi wa hoja kuhusu mwalimu na familia yake,mwalimu kama muumini wa Ujamaa,kamwe hakupenda kuona wengine wanatajarika na wengine wanabaki masikini.....

Na kwasababu alitaka kuwa mfano halisi,ni wazi then hasingependa kuona watoto wake kwenye familia yake wanakwenda kinyume na anacho preach...Kwasababu sikubaliani na wewe kuwa mwalimu angependelea kuona mtoto wake anajilimbikizia mali.Na usitake kusema eti hao watoto wa Mwalimu wangesaidiwa vipi darasani,acha hizo mkuu kwasababu siyo wote wenye akili za darasani ndio wanakuwa matajiri,matajiri wengi sana hapo bongo na hata duniani kwa ujumla hawajasoma...Na kwahiyo basi upambanaji wa kutafuta mali haukutegemea sana elimu.

Hata hivyo nafasi za uongozi zilipatikana base on uwezo wa kielimu,na kwa jinsi mwalimu alivyokuwa kimsingi kutokana na imani zake,hasingeweza kamwe kumpa mtoto wake madaraka yoyote yale hata kama angekuwa na elimu...Na kwahiyo sasa wewe unataka kusema yote hayo yametokea bahati mbaya?

Turudi kwenye issue ya pesa za matumizi kupewa Butiku nk....Malezi ya kijamaa unayajua? Ama labda na wewe ni sapota? Watoto watakapolaumiwa sambamba na malezi nayo yatakuwa questioned,ama kwasababu mnataka kumpa mwalimu utakatifu?

Kama unavyoelewa hapa JF tutajadili pande zote,hayo maneno uliyosema hapo juu ni stories za watanzania kibao tu...Ila cha ajabu hujui source yake na hivyo unabakia kusema eti sijui kuhusu yule mtoto wa Mageni na yeye miguu juu! What is that mkuu?!

Unachotakiwa uelewe ni kuwa hayo yote ni matokeo misingi ya malezi period.

Mambo ya kwenye ujasiariamali wa dunia ya sasa unaona hata mbumbumbu wana opportunity simply because theyre born eith a silver spoon in their mouth....Mfano rahisi ni Bush,ambaye amekuja mpaka kuwa rais...Mifano ni mingi.
 
Mkuu PM, samahani sana nilikuwa sijaiona hii topic, pole sana mkuu naona unabishana na wasioelewa vizuri ukweli,

- Ni kwamba Mwalimu aliwapeleka watoto wake shule kama vile wazazi wetu, sasa kilichojalisha zaidi ilikuwa either akili ya maisha au ya shule, watoto wa Mwalimu hawakuwa na vyote sio siri kwa wale tunaowafahamu, sasa what else Mwalimu alitakiwa kufanya? Hivi unafikiri DK. Hussein asingesota na shule kule Turkey sasa hivi angekua waziri? Hivi unajua maisha ya Turkey yalivyo mkuu kwa mtoto wa rais kusoma kule mpaka kua Doctor?

- Hebu tizama watoto wa Joseph, yaani Matare na Milton, hawa walikuwa na akili ya shule na maisha pia, sasa hivi hawalali njaa na wala hawana shida, pamoja na kwamba wao ni Joseph tu, sasa ndio iwe Mwalimu?

- Watoto wa Mwalimu ni wa kulaumiwa wenyewe and they know that, wewe tizama mtu kama Magambo alivyotajirika kwa jina la Mwalimu na ni ndugu tu, the real Mwalimus wanasota eti wa kulaumu ni Mwalimu? Steven Kiboko anakula kuku ile mbaya tena longtime, na yeye ni Kiboko tu sasa ndio iwe watoto wa Mwalimu?

Mwalimu kwenye watoto wake hana lawama kabisaa, ni noma lao wenyewe!

FMES!


FMES:

Mtu akisoma posti zako mbili za mwisho, humble ya watoto wa Mwalimu ambayo mwanzilishi wa thread aliyotaka kuonyesha, haionekani. Kama kuna failure haitokani na wao kuwa humble bali kwenye miti hakuna wajenzi.

Vilevile Mwalimu yeye ni nusu tu ya watoto wake. Mama pia ana mchango wake. Tena mchango wa mama ni mkubwa.

Kwa maoni yangu binafsi, familia za watu hazitakiwi kuwa kwenye majadiliano. Lakini mtu akizileta zinakuwa fair game.
 
Ila watu mnashangaza sana. Mmemlaumu Nyerere kwa jinsi 'alivyoilostisha' nchi. Hiyo haijatosha. Sasa mnamlaumu hata jinsi alivyolea watoto wake. Mwishowe mtamlaumu hata kwa nini alikufa!!!
 
1.
jmushi1:

FMES, Taratibu....Ni muhimu uelewe msingi wa hoja kuhusu mwalimu na familia yake,mwalimu kama muumini wa Ujamaa,kamwe hakupenda kuona wengine wanatajarika na wengine wanabaki masikini.....

- Mwalimu hakupenda kuona watoto wake wanatajirika, huo ni uongo wa mchana, kama unaamini ni ukweli weka source yake mkuu!

2.
Na kwasababu alitaka kuwa mfano halisi,ni wazi then hasingependa kuona watoto wake kwenye familia yake wanakwenda kinyume na anacho preach...Kwasababu sikubaliani na wewe kuwa mwalimu angependelea kuona mtoto wake anajilimbikizia mali.

- Ni wapi uliposoma ambapo Mwalimu alisema hataki watoto wake kujilimbikizia mali? Na ni wapi ambapo hakutaka viongozi wake kutojilimbikizia mali? Mwalimu alichokuwa hataki ilikuwa ufisadi kujilimbikizia mali kwa ufisadi, lakini sio kwa njia za halali, hebu nitajie m-Tanzania yoyote unayemjua aliyekuwa na utajiri wake under Mwalimu na akamnyanga'anya mali zake bila sababu?

- Mzee Mbowe hakuwa tajiri wakati wa Mwalimu? Ndesamburo hakuwa tajiri under Mwalimu? Mzee Kanyamala hakuwa tajiri under Mwalimu? Kurgisi hakuwa tajiri under Mwalimu? Komanya hakua tajiri under Mwalimu? Mengi hakuwa tajiri under Mwalimu? Sasa kama alikuwa hataki wananchi kujilimbikizia mali ilikuwaje akawaacha hawa? Sasa what is your point kuhusu watoto wake? Ni lini uliwahi kusikia mtoto wake mmoja amekwua tajiri akamnyanga'anya mali zake?

- Hivi unajua kua Mwalimu akiwa kwenye power mtoto wake Madaraka, alikuwa akimiliki malori ya mchanga mengi tu, na kwamba Magige alikua ni Engineeer mkubwa sana kiwanda cha Sukari Kilombero tena akila kuku zake ile mbaya sana! Na kwamba Anna alikuwa Italy akisoma na kuishi huko kwa muda mrefu sana! Rosemary akaja kuwa mbunge wa kupewa na Mkapa, Makongoro akawa mbunge na sasa ni Mwenyekiti wa CCM Musoma, sasa ni nini kosa la Mwalimu hapa? Wewe huwezi kuona kwamba hapa ndipo uwezo wa akili zao kimaisha zilipoishia, sasa Mwalimu ulitaka afanye nini?


3.
Na usitake kusema eti hao watoto wa Mwalimu wangesaidiwa vipi darasani,acha hizo mkuu kwasababu siyo wote wenye akili za darasani ndio wanakuwa matajiri,matajiri wengi sana hapo bongo na hata duniani kwa ujumla hawajasoma...Na kwahiyo basi upambanaji wa kutafuta mali haukutegemea sana elimu.

- Elimu kubwa inatakiwa kuku-guarantee maisha mazuri au utajiri, sasa kama huna akili za darasani basi uwe na akili za maisha, kama huna zote hakuna msaaada na hakuna wa kulaumiwa, wewe ulitaka Mwalimu afanye nini hasa? Achukue hela hazina awape ndio ungefurahi? Kama hawana akili ya kuzitunza then what?

4.
Hata hivyo nafasi za uongozi zilipatikana base on uwezo wa kielimu,na kwa jinsi mwalimu alivyokuwa kimsingi kutokana na imani zake,hasingeweza kamwe kumpa mtoto wake madaraka yoyote yale hata kama angekuwa na elimu...Na kwahiyo sasa wewe unataka kusema yote hayo yametokea bahati mbaya?

- Ulitaka Mwalimu awape madaraka watoto wake are you serious au unatania? Mkapa si aliwapa then what happened? Yaani mkuu kilio chako chote hapa ni kwa sababu ulitaka Mwalimu awape madaraka watoto wake bila sababu kwa kuwa yeye ni rais tu?

5.
Turudi kwenye issue ya pesa za matumizi kupewa Butiku nk....Malezi ya kijamaa unayajua? Ama labda na wewe ni sapota? Watoto watakapolaumiwa sambamba na malezi nayo yatakuwa questioned,ama kwasababu mnataka kumpa mwalimu utakatifu?

- Hapa unasema nini eti watoto wa Mwalimu walikuwa hawapewi hela za matumizi ndio maana leo hawana maisha mazuri? I s that so? Hela za matuimizi kwa watoto ndio guarantee ya maisha mazuri wakikua? Hebu rudia tena hii point mkuu!


6.
Kama unavyoelewa hapa JF tutajadili pande zote,hayo maneno uliyosema hapo juu ni stories za watanzania kibao tu...Ila cha ajabu hujui source yake na hivyo unabakia kusema eti sijui kuhusu yule mtoto wa Mageni na yeye miguu juu! What is that mkuu?!

- Wewe mkuu ndio hujui source ya unachokiongea, je unawafahamu vizuri hawa watoto wa Mwalimu, au na wewe unarukia tu habari za mtaani? Madaraka alioa mtoto wa waziri mmoja then Mageni, ambaye alikua Hotel Manager pale Twiga Hotel huyu demu alikua opportunists na wote pale mjini tulikuwa tunamshitukia jamaa yangu akaupanda mkenge akaishia kuachwa malori yote miguu juu, sasa wewe unasema ninaongea habari za mtaani wakati ninaongea habari nilizozionai, sasa kama huyajui si uulize, hao kina Magambo, Steven Kiboko, Milton na Matare wanaokula kuku sasa hivi kwa jina la Mwalimu wewe unawafahamu mkuu? Huna hoja hapa mkuu!


7.
Unachotakiwa uelewe ni kuwa hayo yote ni matokeo misingi ya malezi period.

- Sasa eti unasema kwamba watoto wote waliopewa malezi mazuri na wazazi wao duniani ndio peke yao wanaokula kuku? Una maana wananchi wote walioko kwenye majela ni kwa sababu hawakupewa malezi mazuri na wazazi wao? Mbona mkuu huna hoja?

8.
Mambo ya kwenye ujasiariamali wa dunia ya sasa unaona hata mbumbumbu wana opportunity simply because theyre born eith a silver spoon in their mouth....Mfano rahisi ni Bush,ambaye amekuja mpaka kuwa rais...Mifano ni mingi.

- Good point, sasa ilikuwaje ndugu wa pembeni wa Mwalimu wakalitumia jina na kutajirika wakati watoto wenyewe wakishindwa? Unasema hili ni kosa la Mwalimu? Utamlinganisha Bush aliyekua akimiliki timu ya Baseball ya Texas Rangers na watoto wa Mwalimu aliyekua hamiliki anything? Watoto wa Mwalimu walikwua na kila kitu on their hands ni matatizo yao wenyewe wakashindwa kutumia nafasi, DK. Hussein asingesota Turkey leo asingekua waziri period.

Respect.

FMES
 
FMES:

Mtu akisoma posti zako mbili za mwisho, humble ya watoto wa Mwalimu ambayo mwanzilishi wa thread aliyotaka kuonyesha, haionekani. Kama kuna failure haitokani na wao kuwa humble bali kwenye miti hakuna wajenzi.

Vilevile Mwalimu yeye ni nusu tu ya watoto wake. Mama pia ana mchango wake. Tena mchango wa mama ni mkubwa.

Kwa maoni yangu binafsi, familia za watu hazitakiwi kuwa kwenye majadiliano. Lakini mtu akizileta zinakuwa fair game.

- Usichanganye mambo, watoto wa Mwalimu hawana tatizo na mtu, ni humble, ni wastaarabu, wenye heshima zao hawana makuu, wana matatizo ndani ya familia yao na siku zote hukaa chini na kuyatatua kifamilia, bila kuingiza mtu wa nje, sio waombaji wa hela au mali, wametulia na umasikini wao.

- Kama kuna a proven principle hapa kwamba wao ni life failures, basi ni mapungufu yao wenyewe lakini sio tatizo la Mwalimu, that is my point.

FMES
 
- Usichanganye mambo, watoto wa Mwalimu hawana tatizo na mtu, ni humble, ni wastaarabu, wenye heshima zao hawana makuu, wana matatizo ndani ya familia yao na siku zote hukaa chini na kuyatatua kifamilia, bila kuingiza mtu wa nje, sio waombaji wa hela au mali, wametulia na umasikini wao.

- Kama kuna a proven principle hapa kwamba wao ni life failures, basi ni mapungufu yao wenyewe lakini sio tatizo la Mwalimu, that is my point.

FMES

Lakini hii thread nzima si mtu ame-dedicate kwa ajiri yao. Inakuwa fair game watu wakiunganisha dots.

Ukiangalia thread imeanzishwa na mtu aliyetegemea information ya ku-google bila kuwajua kiundani na hapo ndipo matatizo yanapoanza.

Mtu akija hapa na kusema Makongoro alifanya hivi au vile, nitaunganisha dots tu.

Mtu akisema huyu jamaa anakula mihogo wakati wa breakfast kwa sababu yupo humble kula mikate ni lazima niunganishe dots tu
 
FMES,
Mkuu wangu unapoteza pumzi zako kwa sababu hawa watu wanachotaka ni LAWAMA zao kwa Nyerere kama kiongozi na baba wa watoto hawa, wakati hakuna kati yao anayefahamu maisha ya hawa watoto.
Yaani kila siku matatizo yetu hutafuta mchawi hakuna hata siku moja tumekubali hata makosa yetu wenyewe....
Kibaya zaidi ni kwamba hakuna mtu anayesema Nyerere angefanya nini cha maana, kwani tumeona tofauti za watoto mbali mbali toka Karume, Mwinyi hadi Mkapa na wote hawa bado wanalaumiwa kwa njia moja ama nyingine....
Jamani kwa nini tunapenda sana kuzungumzia maisha ya watu wengine wakati yetu sisi yanatushinda..
Na inasikitisha sana kuona tunapenda sana kumzungumzia marehemu sijui kwa sababu hayupo duniani, hutasikia wakisema kuhusu Karume, Mwinyi, wala Mkapa ambao wapo hai..
Mkuu nakuomba achana na hawa watu, U're bigger than this nonsense!
 


...wana matatizo ndani ya familia yao na siku zote hukaa chini na kuyatatua kifamilia, bila kuingiza mtu wa nje, sio waombaji wa hela au mali, wametulia na umasikini wao.
Hii si kweli kwamba siku zote huwa wanatatua matatizo yao bila kuingiza mtu wa nje. Wakati familia inafarakana kuhusu mahala pa kumzika marehemu Mwalimu, ilibidi Waziri Kimiti ndio aingilie kati kuwasuluhisha, na Nyerere akazikwa mahala ambapo hakuna aliyetaka baina ya pande zilizogawanyika katika mvutano.

Na si kweli kwamba hawaombi misaada. Andrew hukimbilia ubalozini kupewa misaada na pia kutunzwa kwenye majengo ya serikali, Usalama. Na sitashangaa familia kupokea misaada maana hata Mwalimu alifanya. Alisaidiwa nyumba mpya na TANU mwaka 1974, alisaidiwa nyumba mpya na Jeshi mwaka 1999, alisaidiwa rehani ya nyumba ya Msasani na ukarabati na utunzaji wake kuanzia mwaka 1985. Tuseme yote, sio kuwasafisha tu.
 
1.
Dilunga;Hii si kweli kwamba siku zote huwa wanatatua matatizo yao bila kuingiza mtu wa nje. Wakati familia inafarakana kuhusu mahala pa kumzika marehemu Mwalimu, ilibidi Waziri Kimiti ndio aingilie kati kuwasuluhisha, na Nyerere akazikwa mahala ambapo hakuna aliyetaka baina ya pande zilizogawanyika katika mvutano.

- Sasa unaona unavyoharibu yaani hujui kwamba Kimiti alikubaliwa na familia kuwasimamia masilahi yao katika yale mazishi, kwa hiyo alikua anamuwakilisha Mkapa, ambaye ni part ya familia yao, kwa hiyo Kimiti alikuwa within the family lines, yaani hata dogo hivi ulikuwa hujui mkuu?

2.
Na si kweli kwamba hawaombi misaada. Andrew hukimbilia ubalozini kupewa misaada na pia kutunzwa kwenye majengo ya serikali, Usalama.

- Wapi huko mkuu? Bwa! ha! ha! ha! Yule ni mtoto wa rais mstaafu, popote pale penye serikali anatakiwa kupewa msaada hata sipoomba mkuu vipi mkuu mbona protokali zinakupa taabu sana Bwa! ha! ha! ah! huyu ni mtoto wa rais mstaafu sio sawa na raia wa kawaida bro! Sasa kupewa haki yake sio kuomba mkuu!

3.
Na sitashangaa familia kupokea misaada

- Hii nayo ni hoja inayoanza na sintoshangaa?

4.
maana hata Mwalimu alifanya. Alisaidiwa nyumba mpya na TANU mwaka 1974, alisaidiwa nyumba mpya na Jeshi mwaka 1999, alisaidiwa rehani ya nyumba ya Msasani na ukarabati na utunzaji wake kuanzia mwaka 1985. Tuseme yote, sio kuwasafisha tu.

- Dosa Azizi aliyekuwa muanzilishi wa TAA ndiye aliyemuomba Mwalimu kushika usukani w a chama, na priviledges zake zikawa ni pamoja na kupewa nyumba, sasa unaona unachanganya priviledges za uongozi na kuomba ni vitu viwili tofauti, nyumba ya Mkapa kule Lushoto amejengewa na serikali kwa muijbu wa sheria sio ameomba.

Respect.

FMES!

 
FMES,
Mkuu wangu unapoteza pumzi zako kwa sababu hawa watu wanachotaka ni LAWAMA zao kwa Nyerere kama kiongozi na baba wa watoto hawa, wakati hakuna kati yao anayefahamu maisha ya hawa watoto.
Yaani kila siku matatizo yetu hutafuta mchawi hakuna hata siku moja tumekubali hata makosa yetu wenyewe....
Kibaya zaidi ni kwamba hakuna mtu anayesema Nyerere angefanya nini cha maana, kwani tumeona tofauti za watoto mbali mbali toka Karume, Mwinyi hadi Mkapa na wote hawa bado wanalaumiwa kwa njia moja ama nyingine....
Jamani kwa nini tunapenda sana kuzungumzia maisha ya watu wengine wakati yetu sisi yanatushinda..
Na inasikitisha sana kuona tunapenda sana kumzungumzia marehemu sijui kwa sababu hayupo duniani, hutasikia wakisema kuhusu Karume, Mwinyi, wala Mkapa ambao wapo hai..
Mkuu nakuomba achana na hawa watu, U're bigger than this nonsense!

- Ngoja tutoe darasa kwanza mkuu, hakuna noma!

Respect.

FMES!
 
Back
Top Bottom