Andrew Nyerere on Mwalimu humble children!

Andrew Nyerere on Mwalimu humble children!



Na Mwalimu asingeweza kuwaomba wajerumani maana alizaliwa baada ya utawala wao kuisha.

Source zangu ni humu humu kwenye mtandao. Google utapata habari zote.



Amandla..............

- Kumbe Mwalimu alipokataa masharti ya misaada ya wajerumani na kuwataka waondoke haraka sana bongo, tulikuwa bado hatujawa huru?

- Ahsante sana Mkuu Fundi, na huu ushahidi kutoka google na kushangiliwa na kidenge flani, Bwa! ha! ha! ha! again ahsante sana kwa elimu nzito sana hii kutoka google.

Respect.

FMES

 
The Treaty of Versailles (of 28 June 1919) broke up the colony, giving the western area to Belgium as Ruanda-Urundi, the small Kionga Triangle south of the Rovuma River to Portugal to become part of Mozambique, and the remainder to Britain, which named it Tanganyika.

Nyerere alizaliwa 1922, Nyerere alizaliwa baada ya Mjerumani kuondoka na hajawahi kushindana na Wajerumani katika ukombozi wa Tanganyika.
 
Nyerere alizaliwa 1922, Nyerere alizaliwa baada ya Mjerumani kuondoka na hajawahi kushindana na Wajerumani katika ukombozi wa Tanganyika.

- Kama vile ambavyo hakuwahi kushindana nao kuhusu masharti ya misaada na The West, au?

FMES
 
Dilunga,
Ile nyumba ya Magomeni TANU iliinunua kutoka kwa balozi Tibandebage. Bado ipo pale kama mali ya CCM. Nadhani wanataka kuifanya kama ukumbusho. Ile ya Msasani, ingawa serikali ilimrudishia, Mwalimu aliasa kuwa ataitumia mama Maria and when she is gone it will revert to govt ownership. Kuna mpango wa kuifanya museum of some sort.

- Jasusi darasa safi, hivi ndani kuna anyemjua Mwalimu kuliko wewe? Mimi nawashangaa jamaa wanavyoupanda mkenge!

Weka darasa mkuu tunakula elimu ya bure!

Respect.

FMES!
 
- Kama vile ambavyo hakuwahi kushindana nao kuhusu masharti ya misaada na The West, au?

FMES

Sikusema hivyo mkuu, the operating part ni hapo katika ukombozi wa Tanganyika, nafikiri si pagumu kueleweka.

Baada ya uhuru najua Nyerere aling'oa nyaya za simu za msaada zilizokwishatandikwa na Wajerumani huko Tanga kwa sababu ya tofauti za kisiasa mshashi yule asivyo na akili nzuri.
 
Sikusema hivyo mkuu, the operating part ni hapo katika ukombozi wa Tanganyika, nafikiri si pagumu kueleweka.

Baada ya uhuru najua Nyerere aling'oa nyaya za simu za msaada zilizokwishatandikwa na Wajerumani huko Tanga kwa sababu ya tofauti za kisiasa mshashi yule asivyo na akili nzuri.

- Ohh Finally, ahsante mkuu kwa kukubali ukweli ingawa mwishoni sana kwamba Mwalimu aliwafukuza wajerumani baada ya kutaka kumpa masharti ya misaada, na hii ilikuwa baada ya uhuru, ni hilo ndio hoja yangu ya msingi hapa kuhusu wajerumani, ahsante tena.

Respect.

FMES
 
Tusipotoshe mambo,kuna eneo Butiama linaitwa Mwitongo,kama mmelitafuta kwenye google earth,shauri zenu hamtaliona,ni kitongoji na ni mlimani hivi.
Mwalimu alijenga nyumba Butiama na wala sio Mwitongo,iko mbali kidogo na Mwitongo,mama yake,dada yke walikuwa wanakaa eneo hilohilo,na mbele kidogo ni mji wa chief Wanzagi ambaye ni kaka yake na ndiye aliyekuwa mkuu wa ukoo wa Nyerere.
Kwenye hio picha hapo wawili sio watoto wake...mmoja ni mtoto wa mdogo wake na mwingine ni mdogo wa Mama Maria.Mengine yanatia hata uvivu kuchangia.
 
Aliyepakatwa na Mwalimu ni Madaraka,waliokaa chini,kutoka kushoto ni mtoto wa Joseph Nyerere,Magige,Rose na Makongoro.
Waliosimama kuanzia kushoto ni John,Anna,Andrew na huyo mwingine ni mdogo wa mama Maria
 
Dilunga,
Kama alivyosema FMES tupo hapa kuelimishana. Tuendelee kumkona nyani giladi.
Ila kwa wale ambao hawajafika Butiama ningewashauri mkipata nafasi na uwezo mtembelee kile kijiji. Waambie wenyeji wawaonyeshe nyumba ya kwanza aliyojenga Mwalimu alipokuwa anajitayarisha kumwoa mama Maria. Yaani huwezi ku-imagine mtu amerudi na degree ya Edinburgh anajenga such a simple house. But that was Mwalimu.
 
Tusipotoshe mambo,kuna eneo Butiama linaitwa Mwitongo,kama mmelitafuta kwenye google earth,shauri zenu hamtaliona,ni kitongoji na ni mlimani hivi.
Mwalimu alijenga nyumba Butiama na wala sio Mwitongo,iko mbali kidogo na Mwitongo,mama yake,dada yke walikuwa wanakaa eneo hilohilo,na mbele kidogo ni mji wa chief Wanzagi ambaye ni kaka yake na ndiye aliyekuwa mkuu wa ukoo wa Nyerere.
Kwenye hio picha hapo wawili sio watoto wake...mmoja ni mtoto wa mdogo wake na mwingine ni mdogo wa Mama Maria.Mengine yanatia hata uvivu kuchangia
.

- Sasa unaona Zanaki, safi sana lete darasa kumbe sasa waliosema kwamba Mwitongo sio anything ila ni pango kumbe zilikuwa ni kamba?

FMES!
 
Dilunga,
Kama alivyosema FMES tupo hapa kuelimishana. Tuendelee kumkona nyani giladi.
Ila kwa wale ambao hawajafika Butiama ningewashauri mkipata nafasi na uwezo mtembelee kile kijiji. Waambie wenyeji wawaonyeshe nyumba ya kwanza aliyojenga Mwalimu alipokuwa anajitayarisha kumwoa mama Maria. Yaani huwezi ku-imagine mtu amerudi na degree ya Edinburgh anajenga such a simple house. But that was Mwalimu.

- Mkuu Jasusi, saafi sana mimi nimefika sana pale Butiam na Kung'ombe, wakati ule tunafanya biashara ya siagi na kina Koi, Elamu, Matare na Milton, kutoka Musoma,

- Sikumbuki vizuri kila kitu, lakini ninajua one thing kwamba wewe na Zanaki, mna make a lot of sense na mnayo authority nzito sana kuhusu somo la Butiama sasa endeleeni kutuelimisha wakuu na hii elimu ya bure.

Respect.

FMES
 
- Mkuu Fundi ahsante sana kwa ufahamisho wako kwamba source yako ni humu humu Google, sina la kuongeza zaidi mkuu, labda kidogo tu!.

FMES!

Mkuu FMES. Mimi sina ubavu wa kudai watoto wa Marehemu Dossa Aziz walikuwa rafiki zangu. Siwajui, Mkuu, kama vile ambavyo siwajui watoto wa wale tunaowaita wakubwa wote. Sources zangu zote ziko kwenye public fora na wala si anecdotes nilizobahatika kusikia.

Tofauti na unavyotaka kusema, Mwalimu hakusita kuomba. Hao wajerumani aliwaomba watujengee reli kwenda Zambia, wakamtolea nje. Alichokuwa akipinga yeye ni masharti ya kipuuzi. Alikataa kuwabembeleza Ujerumani Magharibi pale walipompa sharti la kutoitambua Ujerumani Mashariki. Kuomba kwake halikuwa tatizo maana alijua hali ya nchi yake. Alichokataa ni kudhalilishwa kutokana na umaskini wake.

Amandla..........
 
Dilunga,
Kama alivyosema FMES tupo hapa kuelimishana. Tuendelee kumkona nyani giladi.
Ila kwa wale ambao hawajafika Butiama ningewashauri mkipata nafasi na uwezo mtembelee kile kijiji. Waambie wenyeji wawaonyeshe nyumba ya kwanza aliyojenga Mwalimu alipokuwa anajitayarisha kumwoa mama Maria. Yaani huwezi ku-imagine mtu amerudi na degree ya Edinburgh anajenga such a simple house. But that was Mwalimu.

Lakini si aliporudi alikuwa Mwalimu wa kawaida tu? Sidhani kama angekuwa na ubavu wa kujenga nyumba ya kifahari kutokana na mshahara wake. Wakati ule watu waliishi kwa mishahara yao si kama siku hizi. Nadhani tuzungumzie zaidi mambo aliyoyafanya alipokuwa Waziri Mkuu halafu Rais. Nyumba alizojenga wakati huo, ingawa zilikuwa nzuri, lakini hazikuwa za kifahari!

Amandla..........
 
Fundi Mchundo,
Mkuu uenifanya nijiulize maswali!..
Hivi wazee wetu walijenga vipi nyumba za kifahari wakati wa Mkoloni?..Na hizo za kifahari zilifanana vipi wakati ule maanake tusije changanya ufahari wa miaka ya 1950.

Nakumbuka Magomeni Mikumi ndio ilikuwa O'bay ya wakati ule kwa waswahili.
Wasomi wote walijenga Mikumi na kama ukifuatilia list ya waasisi wa chama wengi wao walikuwa wakiishi Magomeni Mikumi..Kwa kipato gani waliweza jenga nyumba kama makarani wa mkoloni, wakati leo hii tukiwa huru graduate wa Mlimani hawezi jenga hata kibanda cha uwani bila kuiba!..
 
Fundi Mchundo,
Mkuu uenifanya nijiulize maswali!..
Hivi wazee wetu walijenga vipi nyumba za kifahari wakati wa Mkoloni?..Na hizo za kifahari zilifanana vipi wakati ule maanake tusije changanya ufahari wa miaka ya 1950.

Nakumbuka Magomeni Mikumi ndio ilikuwa O'bay ya wakati ule kwa waswahili.
Wasomi wote walijenga Mikumi na kama ukifuatilia list ya waasisi wa chama wengi wao walikuwa wakiishi Magomeni Mikumi..Kwa kipato gani waliweza jenga nyumba kama makarani wa mkoloni, wakati leo hii tukiwa huru graduate wa Mlimani hawezi jenga hata kibanda cha uwani bila kuiba!..

Sidhani kama walikuwa na nyumba za kifahari wakati wa ukoloni. Walijenga nyumba zilizoendana na staha zao. Nyumba nzuri, za kudumu, zenye umeme ndani na maji. Hata Magomeni Mikumi nyumba zilizokuwepo, vijana wa leo wangeziona mapagala. Nyingi zilikuwa hazina hata self container! Lakini ndiyo hizo ambazo makarani, walimu n.k walijenga, walijivunia na kulelea watoto wao.

Ukiangalia hata nyumba za wakoloni hazikuwa chochote kitu. Vyumba viwili, sebule, jiko na bafu la kushirikiana. Nje walikuwa na gereji na chumba cha hausiboi. Mchezo umekwisha!

Siku hizi kipato chetu hakiendani na gharama za ujenzi pamoja na matarajio yetu. Wengi wetu si wavumilivu na tunataka maksri yasiyoendana na nafasi yetu. Utakuta maofisini wasomi hawajengi lakini matypist na walinzi wana vibanda vyao! Hao wanakusanya kidogo kidogo, wanapiga matofali taratibu, wanajenga bila sakafu wala siling bodi, madirisha, maji wala umeme. Halafu wanaanza na chumba kimoja. Lakini baada ya miaka wana kibanda cha kuwahifadhi wakati wasomi wanasubiri dili ili wajenge kasri!

Amandla.......
 
Sidhani kama walikuwa na nyumba za kifahari wakati wa ukoloni. Walijenga nyumba zilizoendana na staha zao. Nyumba nzuri, za kudumu, zenye umeme ndani na maji. Hata Magomeni Mikumi nyumba zilizokuwepo, vijana wa leo wangeziona mapagala. Nyingi zilikuwa hazina hata self container! Lakini ndiyo hizo ambazo makarani, walimu n.k walijenga, walijivunia na kulelea watoto wao.

Ukiangalia hata nyumba za wakoloni hazikuwa chochote kitu. Vyumba viwili, sebule, jiko na bafu la kushirikiana. Nje walikuwa na gereji na chumba cha hausiboi. Mchezo umekwisha!

Siku hizi kipato chetu hakiendani na gharama za ujenzi pamoja na matarajio yetu. Wengi wetu si wavumilivu na tunataka maksri yasiyoendana na nafasi yetu. Utakuta maofisini wasomi hawajengi lakini matypist na walinzi wana vibanda vyao! Hao wanakusanya kidogo kidogo, wanapiga matofali taratibu, wanajenga bila sakafu wala siling bodi, madirisha, maji wala umeme. Halafu wanaanza na chumba kimoja. Lakini baada ya miaka wana kibanda cha kuwahifadhi wakati wasomi wanasubiri dili ili wajenge kasri!

Amandla.......

Fundi Mchundo:

Wewe hutaki kujenga kwa sababu tunakokaa watu aveleji unakuita uswazi. Mnataka kubanana Osterbay.
 
Fundi Mchundo,
Mkuu uenifanya nijiulize maswali!..
Hivi wazee wetu walijenga vipi nyumba za kifahari wakati wa Mkoloni?..Na hizo za kifahari zilifanana vipi wakati ule maanake tusije changanya ufahari wa miaka ya 1950.

Nakumbuka Magomeni Mikumi ndio ilikuwa O'bay ya wakati ule kwa waswahili.
Wasomi wote walijenga Mikumi na kama ukifuatilia list ya waasisi wa chama wengi wao walikuwa wakiishi Magomeni Mikumi..Kwa kipato gani waliweza jenga nyumba kama makarani wa mkoloni, wakati leo hii tukiwa huru graduate wa Mlimani hawezi jenga hata kibanda cha uwani bila kuiba!..

Mkandara:

Takwimu zinaonyesha kuwa kipato cha civil servant mpaka 1979 kilikuwa kimepungua kwa zaidi ya 90%. Najua utalalamika kuwa nanukuu wazungu, lakini that's is the way it's.
 
Mkandara:

Takwimu zinaonyesha kuwa kipato cha civil servant mpaka 1979 kilikuwa kimepungua kwa zaidi ya 90%. Najua utalalamika kuwa nanukuu wazungu, lakini that's is the way it's.

Duh! hapa nipe ufahamu zaidi!
 
1.
Fundi Mchundo;

Mkuu FMES. Mimi sina ubavu wa kudai watoto wa Marehemu Dossa Aziz walikuwa rafiki zangu. Siwajui, Mkuu, kama vile ambavyo siwajui watoto wa wale tunaowaita wakubwa wote. Sources zangu zote ziko kwenye public fora na wala si anecdotes nilizobahatika kusikia.

- Mkuu Fundi, watoto wa Mwalimu, na Mwalimu mwenyewe ninawafahamu vizuri sana, ndio maana haikuwa taabu kuchangia hii mada na kuuweka ukweli kwamba Mwalimu hana makosa kabisaa katika maisha ya watoto wake, kuwajua watu wa aina flani ni mambo ya territory tulizotoka, wala sio crime kama unavyotaka kuiweka, ulianza vizuri vipi nini kimekusibu sasa mwishoni?

2.
Tofauti na unavyotaka kusema, Mwalimu hakusita kuomba. Hao wajerumani aliwaomba watujengee reli kwenda Zambia, wakamtolea nje. Alichokuwa akipinga yeye ni masharti ya kipuuzi. Alikataa kuwabembeleza Ujerumani Magharibi pale walipompa sharti la kutoitambua Ujerumani Mashariki. Kuomba kwake halikuwa tatizo maana alijua hali ya nchi yake. Alichokataa ni kudhalilishwa kutokana na umaskini wake.

Amandla..........

- Point ilikwa kama Mwalimu na watoto wake ni waombaji, nikasema sio kweli hawana hiyo tabia, nikasema Mwalimu hawezi kujidhalilisha na kuomba omba kwa sababu ya maisha yake binafsi, naona sasa umeikubali hoja yangu, na kwamba Mwalimu alipopambana na wajerumani tulikuwa huru tayari kama nilivyosema, ahsante sana mkuu.

FMES
 
- Mkuu Fundi, watoto wa Mwalimu, na Mwalimu mwenyewe ninawafahamu vizuri sana, ndio maana haikuwa taabu kuchangia hii mada na kuuweka ukweli kwamba Mwalimu hana makosa kabisaa katika maisha ya watoto wake, kuwajua watu wa aina flani ni mambo ya territory tulizotoka, wala sio crime kama unavyotaka kuiweka, ulianza vizuri vipi nini kimekusibu sasa mwishoni?

Ingawa sikubaliani na wewe kwenye kusema Mwalimu hakuchangia HATA KIDOGO hatima ya watoto wake, I apologise kwa lugha niliyoitumia!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom