Andrew Nyerere on Mwalimu humble children!

Andrew Nyerere on Mwalimu humble children!

Samahani kama nimekosa jina, lakini nazungumza mtoto wa Mwalimu. Sikuwa darasa moja, lakini tulikuwa shule moja na nilimjua kwa sababu alikuwa mtoto wa Rais. Nahakikisha yeye hanijui mimi binafsi. Samahani for this oversight.
 
Nyani Ngabu said:
Joka...hata mimi nina maoni hayo hayo. Malezi ya watoto wa Nyerere kwa kweli, kwa mtazamo wangu mimi, hayatuhusu. Hayo ni mambo ya kifamilia.

Tunavuka mno mstari na kuanza kumkosoa Mwalimu kwa mambo binafsi. Malezi ya watoto wake sisi yanatuhusu vipi? Oooh eti mmoja wa watoto wake mlevi..so what? Kuna walevi wangapi dunia hii?

Lawama lawama lawama ad infinitum...and then what?

NN,

..karibu tena jamvini.

..i am 100% with you. kwa mtizamo wangu, mtoto hulelewa na wazazi wake, pamoja na jumuiya inayomzunguka.

..kwamba mtoto atakuja kuwa mtu wa maana atakayewaenzi na kuwatunza wazazi kwangu mimi ni suala la majaaliwa kama bahati ya kuwa na mtoto. you just try your very best, lakini matokeo ni kazi ya MUNGU.
 
Heheheheheee....nilikuwepo kama sipo......habari njema kabisa. Karibu nachoma nyama hapa na kuna bonge la keg la Heineken na kama unapenda Stella Hatoi pouwa tu...naye anapatikana

Nafurahi kukuona mazee, Heineken is OK najua umezimiss sana kule behind the bars! Stella huku wanaziita bit my wife hahahah Enjoy man....mimi ninaahadi na Sungura tope sitaki leo nitaharibu!!
 
Mwalimu is probably the greatest figure to appear in the history of our country to date. Kwa hali hiyo, ni lazima itafika wakati watu watataka kujua ni nini kilichomsukuma kufikia pale alipofikia. Watataka kumjua Mwalimu kama binadamu wa flesh and blood na sio huyu two-dimensional larger than life figure ambae tunataka kumfanya. Kwa hali hiyo mahusiano yake na watu walio karibu nae (pamoja na familia yake) vitachinguzwa na kujadiliwa ili kutafuta kujua ukweli wa yale ambayo anadaiwa kuyafanya na nini hasa kilichomfanya a-click. Hivi kweli mnadhani kama watakuja kutayarisha documentary ya maisha yake itajaa clips za yeye akisaini mikataba, kutembea kuunga Azimio la Arusha, kutangaza vita na Uganda, n.k. tu? Producer yeyote anajua kuwa ili kuifanya hiyo documentary credible itabidi kuingiza haya ambayo baadhi yetu tunadai ni personal issues.

Watoto wa Mwalimu kuwa na kile tunachokiona ni matatizo hakiamuondolea heshima ya mambo aliyoyafanya. Mbona kwenye ukoo wa Kennedys kuna drug addicts, alcoholics, watu walioshutumiwa kubaka n.k.? Yote haya hayajawaongolea J.F.K na mdogo wake heshima katika macho ya wamarekani. Martin Luther King, kama alivyokuwa JFK, alijulikana kama mtu wa warembo lakini bado stature yake ipo pale pale. Mimi naamini kuwa ni refreshing kama mijadala kama hii ikiwepo wakati watu waliomfahamu Mwalimu wangali hai. Wakiondoka wao, mengi yatakuwa speculated na si yote yatamweka Mwalimu katika mwanga mzuri. Watoto wa Mwalimu ni sehemu ya historia yetu na kwa hali hiyo hawawezi kuepuka kuwa katika public eye. Pengine si chaguo lao lakini fate ndiyo imewafikisha hapo.

Amandla......
 
Mwalimu is probably the greatest figure to appear in the history of our country to date. Kwa hali hiyo, ni lazima itafika wakati watu watataka kujua ni nini kilichomsukuma kufikia pale alipofikia. Watataka kumjua Mwalimu kama binadamu wa flesh and blood na sio huyu two-dimensional larger than life figure ambae tunataka kumfanya. Kwa hali hiyo mahusiano yake na watu walio karibu nae (pamoja na familia yake) vitachinguzwa na kujadiliwa ili kutafuta kujua ukweli wa yale ambayo anadaiwa kuyafanya na nini hasa kilichomfanya a-click. Hivi kweli mnadhani kama watakuja kutayarisha documentary ya maisha yake itajaa clips za yeye akisaini mikataba, kutembea kuunga Azimio la Arusha, kutangaza vita na Uganda, n.k. tu? Producer yeyote anajua kuwa ili kuifanya hiyo documentary credible itabidi kuingiza haya ambayo baadhi yetu tunadai ni personal issues.......

Kwa hiyo wewe kujua Andrew amedata na anavalishwa straight jacket na sijui Madaraka au Makongoro ni walevi wa mapombe machafu kutakusaidia nini?

Halafu kuharibikiwa kwao mnamlaumu Nyerere....ni haki kweli hiyo? Hivi kila anayeharibikwa maishani wa kulaumiwa ni wazazi na malezi waliyowapa?

Mwishowe mtaanza kuuliza Nyerere alikuwa anavaa briefs au boxers......endeleeni....
 
Nyani Ngabu,
Mkuu karibu...duh kulipooza kichizi mkuu wangu pamoja na yote hayo umerudi na makali mapya!..
 
Kwa hiyo wewe kujua Andrew amedata na anavalishwa straight jacket na sijui Madaraka au Makongoro ni walevi wa mapombe machafu kutakusaidia nini?

Halafu kuharibikiwa kwao mnamlaumu Nyerere....ni haki kweli hiyo? Hivi kila anayeharibikwa maishani wa kulaumiwa ni wazazi na malezi waliyowapa?

Mwishowe mtaanza kuuliza Nyerere alikuwa anavaa briefs au boxers......endeleeni....

Si kila kitu ninachoulizia lazima kinisaidie.

Hivi mnataka kusema kuwa kama wangekuwa na mafanikio makubwa, watu wasingewasifia wazazi wao kwa malezi waliowapa watoto wao? Tunapojadili mafanikio na kutofanikiwa katika maisha kwa mtu hatuwezi kukwepa kujadili malezi yake na nafasi yake katika hatma ya maisha yake. Tupende, tusipende malezi tunayopata utotoni yana sehemu kubwa katika maisha yetu ya baadae.

Hayo maswali mengine ni yako. Sisi huko hatumo.

Amandla....
 
Fundi Mchundo,
Mkuu ebu nambie kuna mtoto gani kasifiwa au anaweza kusifiwa na Wadanganyika kwa malezi ya wazazi wake..Acheni wakuu zangu kwa mbongo kila kitu ni nuksi tupu hata ukimsema Karume au Mwinyi bado watakuja na matusi ya nguoni...hasifiwi wala hapendwi mtu hata siku moja, ndio tulivyo..
Ktk mkusanyiko wa hoja nyingi humu inadhihirisha wazi NDIVYO TULIVYO!...
 

Mwalimu is probably the greatest figure to appear in the history of our country to date. Kwa hali hiyo, ni lazima itafika wakati watu watataka kujua ni nini kilichomsukuma kufikia pale alipofikia. Watataka kumjua Mwalimu kama binadamu wa flesh and blood na sio huyu two-dimensional larger than life figure ambae tunataka kumfanya. Kwa hali hiyo mahusiano yake na watu walio karibu nae (pamoja na familia yake) vitachinguzwa na kujadiliwa ili kutafuta kujua ukweli wa yale ambayo anadaiwa kuyafanya na nini hasa kilichomfanya a-click. Hivi kweli mnadhani kama watakuja kutayarisha documentary ya maisha yake itajaa clips za yeye akisaini mikataba, kutembea kuunga Azimio la Arusha, kutangaza vita na Uganda, n.k. tu? Producer yeyote anajua kuwa ili kuifanya hiyo documentary credible itabidi kuingiza haya ambayo baadhi yetu tunadai ni personal issues.

Watoto wa Mwalimu kuwa na kile tunachokiona ni matatizo hakiamuondolea heshima ya mambo aliyoyafanya. Mbona kwenye ukoo wa Kennedys kuna drug addicts, alcoholics, watu walioshutumiwa kubaka n.k.? Yote haya hayajawaongolea J.F.K na mdogo wake heshima katika macho ya wamarekani. Martin Luther King, kama alivyokuwa JFK, alijulikana kama mtu wa warembo lakini bado stature yake ipo pale pale. Mimi naamini kuwa ni refreshing kama mijadala kama hii ikiwepo wakati watu waliomfahamu Mwalimu wangali hai. Wakiondoka wao, mengi yatakuwa speculated na si yote yatamweka Mwalimu katika mwanga mzuri. Watoto wa Mwalimu ni sehemu ya historia yetu na kwa hali hiyo hawawezi kuepuka kuwa katika public eye. Pengine si chaguo lao lakini fate ndiyo imewafikisha hapo.

Amandla......

Wewe jamaa siku nikikutana na wewe in person nitacheka ile mbaya siku hiyo. Unanifurahisha sana. Najaribu kukuchora akilini, jamaa mmoja focused ile mbaya, private sana, mpole mpole, lakini hunyenyekei mtu, mwenye misimamo mikali sana, halafu knowledgeable ile mbaya. Ha aha aaaaaaa

Hayo mambo ulosema hapo nimewahi kumwambia mtu hiiiivyo hiiiiivyo.... karibu neno kwa neno. Kwamba Nyerere yule ndio ametupa identity Watanzania, ubunifu wa kuanzisha siasa zake, na kujenga mfungamano wa Watanzania na mpaka leo tuna aina fulani ya ujamaa ujamaa umetukaa vichwani. Ni sehemu kubwa sana ya historia ya maisha ya Mtanzania, ni lazima tumchambue kwa undani.

Juzi nimemwangalia Warioba anahojiwa kifupi chuo kikuu, waandishi wakawa wanakubaliana nae mpaka wanamalizia sentensi za Warioba. Nikamuuliza mshkaji mmoja, e bana eeh unaona hawa waandishi wanauliza swali halafu wanamalizia wenyewe kauli za warioba kama watoto wa darasani? Jamaa akanijibu hiyo ni sehemu ya urithi wetu wa Ujamaa. Kukubaliana, mshikamano, undugu. Hakuna kubananana mbavu. Kwa faida au hasara, lakini ndivyo ilivyo. Yote haya ni Nyerere. Ametupa identity, national personality, if you will.

Sasa mtu aliyetupa personality ya Taifa, kwa nini msimsome kwa undani iwezekanavyo?
 
Mwalimu is probably the greatest figure to appear in the history of our country to date. Kwa hali hiyo, ni lazima itafika wakati watu watataka kujua ni nini kilichomsukuma kufikia pale alipofikia. Watataka kumjua Mwalimu kama binadamu wa flesh and blood na sio huyu two-dimensional larger than life figure ambae tunataka kumfanya. Kwa hali hiyo mahusiano yake na watu walio karibu nae (pamoja na familia yake) vitachinguzwa na kujadiliwa ili kutafuta kujua ukweli wa yale ambayo anadaiwa kuyafanya na nini hasa kilichomfanya a-click. Hivi kweli mnadhani kama watakuja kutayarisha documentary ya maisha yake itajaa clips za yeye akisaini mikataba, kutembea kuunga Azimio la Arusha, kutangaza vita na Uganda, n.k. tu? Producer yeyote anajua kuwa ili kuifanya hiyo documentary credible itabidi kuingiza haya ambayo baadhi yetu tunadai ni personal issues.

Watoto wa Mwalimu kuwa na kile tunachokiona ni matatizo hakiamuondolea heshima ya mambo aliyoyafanya. Mbona kwenye ukoo wa Kennedys kuna drug addicts, alcoholics, watu walioshutumiwa kubaka n.k.? Yote haya hayajawaongolea J.F.K na mdogo wake heshima katika macho ya wamarekani. Martin Luther King, kama alivyokuwa JFK, alijulikana kama mtu wa warembo lakini bado stature yake ipo pale pale. Mimi naamini kuwa ni refreshing kama mijadala kama hii ikiwepo wakati watu waliomfahamu Mwalimu wangali hai. Wakiondoka wao, mengi yatakuwa speculated na si yote yatamweka Mwalimu katika mwanga mzuri. Watoto wa Mwalimu ni sehemu ya historia yetu na kwa hali hiyo hawawezi kuepuka kuwa katika public eye. Pengine si chaguo lao lakini fate ndiyo imewafikisha hapo.

Amandla......

Documentary ya mwalimu imeshatoka, go to mwalimu chair university of dar utaipata!
 
Jamani mlio Dar tuarifuni tunaweza kuipata vipi. How much does it cost?

Jasusi:

Wewe ni living documentary ya mwalimu na bado unataka zaidi ya hapo. Afu usanii wa shule ya Tambaza mliuanzisha zamani sana.

Yaani yule member anayeitwa Swari ana posti tano tu na anakuja moja kwa moja kujibu posti moja na kupotea.
 
kwi!kwi!kwi!
Mwakikagile is a friend of mine ingawa tumepoteana muda mrefu sasa. Kama unazo contacts zake nitapenda kuwasiliana naye.

Jasusi,

Kama ulivyosema, ulisoma shule H.H. The Aga Khan (Tambaza) kabla ya mimi na wanafunzi wenzangu kama kina George Mazula (marehemu), Andrew Nyerere, Mohammed Chande Othman (High Court Judge), Msafiri Abdallah, Godfrey Mwakikagile, Celestine Mwinula, Walter Mallya (kaka ya High Court Judge Willie Mallya), Rashid Hemed (mwanasheria)i, James Maugo (pia mwanasheria), Balinagwe Mwambungu, Hamisi Kasanga, Abdallah Yakuti, Geoffrey Mbogo, Suleiman Kazema, Mlozi, Chinja, Omari Mangosongo, Dodo Dafi, Swai, Nkya, wasichana na classmate wangu Pili (kutoka Tabora) na Flora (kutoka Handeni), msichana mwingine Tecla Chando (kutoka Moshi) na wengineo hatujaenda hapo.

Kwa sababu ulitutangulia pale Tambaza, unawafahamu kina Juma Penza na Reginald Mhango? Wao pia wlisoma shule Aga Khan (Tambaza) kabla ya sisi, na nimeambiwa kwamba ni marafiki sana wa Godfrey Mwakikagile. Pia walifanya kazi pamoja na Godfrey Mwakikagile kama waandishi wa habari pale Daily News kati ya 1969 na 1972 mwaka ambao Mwakikagile aliondoka kwenda shule USA. Kama wanavyojua, Godfrey alianza kufanya kazi pale gazetini alipokuwa bado mwanafunzi Tambaza, Form V, wakati wa likizo, mwezi wa June. Namkumbuka sana kwa sababu alikuwa ni classmate wangu na tuliishi pamoja pale H.H. The Aga Khan Hostel 1969 - 1970.

Nimewataja hao wawili, Juma Penza ambaye baadaye akawa national publicity secretary wa chama cha utawala CCM (pamoja na Paul Sozigwa), halafu director wa Radio Uhuru, na Reginald Mhango ambaye alikuwa editor wa Daily News na baadaye managing editor wa Guardian (na kazi zingine serikalini) kwa sababu wanaweza kukusaidia kuwasiliana na Godfrey Mwakikagile.

Pia muulize Charles Kizigha, Daily News, na Kassim Mpenda, Director of Information Services, Ministry of Information, ambao walifanya kazi pamoja na Mwakikagile kama news reporters pale Daily News pamoja na Juma Penza na Reginald Mhango na wengineo. Hao wawili, Kizigha na Mpenda, walikuwa na mawasiliano na Mwakikagile kupitia kwa Andrew Nyerere miaka ya karibuni. Unaweza kuwauliza kuthibitisha jambo hilo. Nina uhakika kwa sababu nilikuwa na Andrew Nyerere kwa muda mrefu Dar es Salaam Godfrey Mwakikagile alipokuwa anaandika kitabu kuhusu Mwalimu, "Nyerere and Africa: End of an Era." Andrew aliwasiliana na Mwakikagile kwa muda mrefu kati ya 1999 na 2004 alipokuwa anaandika kitabu hicho na kabla ya second edition kuchapishwa mwanzoni mwa 2005. Edition ya kwanza ilichapishwa 2002, ya pili 2005, ya tatu 2006, na ya nne 2008.

Godfrey alimwambia Andrew aende kwa Kizigha na Mpenda ili wamtafutie picha anazohitaji kitabuni. Andrew alikwenda kuonana na Kizigha na Mpenda kwa niaba ya Mwakikagile kuhusu project hiyo ili wamtumie Godfrey picha mbali mbali za Mwalimu. Andrew alipewa picha hizo kutoka kwenye archives na alimtumia Godfrey pamoja na picha chache kutoka nyumbani kwa Mwalimu ili azitumie katika kitabu alichokuwa anaandika na ambamo amemtaja Kizigha na Mpenda na kuwapa shukrani kwa msaada wao ingawa amesema pia hakuweza kuzitumia picha zote katika kitabu hicho. Na Andrew aliwahi kuniambia kwamba anawasiliana na Godfrey Mwakikagile kwa email na simu nyakati hizo. Pia barua za mawasiliano hayo ziko katika kitabu hicho ambacho kwa sasa kimesomwa na watu mbali mbali pamoja na Watanzania kama Mzee Butiku na Salim Ahmed Salim kama inavyoelezwa kitabuni kutokana na mawasiliano kati ya Andrew na Godfrey. Hivi sasa nasoma Fourth Edition ya kitabu hicho, 740 pages, and I'm really plodding through since it's a tome with small print (font size 10). Ingekuwa print ya kawaida ( 12 point font size), kitabu hicho kingekuwa zaidi ya 1,000 pages.

Ningeweza kumuuliza Andrew kama anaweza kukupa contact za Mwakikagile lakini kutokana na hali yake, haiwezekani. Na sijamwona Dar kwa muda mrefu. Kwahiyo jaribu kuwauliza kina Juma Penza, Reginald Mhango, Charles Kizigha na Kassim Mpenda. Inawezekana watakusaidia kuwasiliana na rafiki yako huyo.

Kwa upande wangu, nitajaribu kukusaidia kwa sababu Mwakikagile na mimi tuna mutual friend, Professor Emmanuel Sendezera, Physics, kule Afrika Kusini. Amewasiliana na Mwakikagile kwa miaka mingi tangu walipokuwa pamoja USA - walisoma shule pamoja USA - na ninadhani bado anawasiliana naye hata sasa. Kuna wakati aliniambia kuna Mtanzania anayemfahamu sana ambaye ameandika vitabu, na aliponiambia jina, nilimwambia kwamba Godfrey Mwakikagile alikuwa ni classmate wangu Tanzania. Mimi pia bado nawasiliana na Sendezera. Alikuwa head of Physics Department, University of Malawi, na pia alifundisha Wits (University of Witwatersrand) na vyuo vikuu vingine kule South Africa. Na bado anafundisha huko. Yuko KwaZulu/Natal sasa. Nitamuuliza kama anaweza kunipa contact hizo na nitakujilisha kwa njia ya private message.
 
Hii Thred ni Nzuri , inatukumbusha JULIUS KAMBARAGE NYERERE, It is Good to know that he has not FORGOTEN, as long as the History of our country STANDS, Najua tunapomzungumzia Nyerere kuna mambo mengi sana ya kuyaangalia, Kwa mfano :Ujamaa, Hotuba zake, mitazamo yake,mavazi yake(hususani zile suti na Kile kifimbo ambacho mengi yameongelea juu yake hata kufikia mmoja wa wanafamilia kukimiliki akiwa na imani fulani), lakini katika yote Watoto wake ni kiwakilishi kizuri kwa watu wote. Wamefanikiwa au kutofanikiwa hii inatokana na mitizamo ya watu.Lakini ilifaa sana tuwapate wenyewe waseme Ni changamoto gani walikumbana nazo kulelewa na baba kama Julius?Na nini yalikuwa matarajio ya Nyerere kwao?

Ninahisi Jasusi ni Nyerere Damu, Kama alivyo Zanaki. Hawa wanayoyakusema.
 
Shwari,
You too must be a teacher. Una memory nzuri sana. Hata Zakumi amekuwa impressed. Ndio, nawafahamu wengi wa uliowataja, including Penza, Mhango na Kizigha. Umenirahisishia sana kazi ya kumtafuta Mwakikagile. Thank you, thank you!
 
garnesh ...naona upo hewani....watu wanataka kujuwa kama ndie wewe yule au tuendelee kumsubiri....
 
Currently Active Users Viewing This Thread: 4 (3 members and 1 guests)
Phillemon Mikael, ganesh, Nyani Ngabu
 
..yes garnesh ...[andrew nyerere]- as you said ...

i have concluded ...your article on budhism was such goood....and the other you wanted dalai to visit tanzania...

we want now you to get more involved with issues ..just like willium j..... together we can shape the history and influence the future....you are such a bright fellow!

ganesh
ganesh has no status.
Senior Member Join Date: Mon Nov 2008
Posts: 117
Thanks: 0
Thanked 23 Times in 15 Posts
Rep Power: 21

Credits: 1

dalai lama akaribishwe tanzania

--------------------------------------------------------------------------------

Mkutano wa amani uliopangwa kufanyika SA ,umefutwa,kwa ajili Serkali ya SA haitaki Dalai Lama aende kule. Kwa nini SerIkali ya Tanzania isipendekeze kwamba huu mkutano ufanyike hapa Dar es Salaam? Ni ajabu kuona kwamba SA ambayo inaongoza Afrika kwa ujambazi,na labda pia kwa ukimwi,inaweza kumfukuza kiongozi wa dini. Afrika ina matatizo mengi ya vita,kwa hiyo siyo vizuri kuwazuia viongozi wa dini kuja hapa. Afrika pia ina matatizo ya mmong'onyoko wa maadili. Tuko tayari kumsikiliza kiongozi yoyote wa kidini,kama anao ushauri wowote. Benedict XVI alikuwepo hapa wiki iliyopita. Vatican inasikitika kwamba maneno aliyosema kuhusu Afrika hayakusikilizwa,badala yake umetokea ubishi mkubwa kuhusu maneno yake aliyosema kuhusu condom. Pope Benedict aliongea kuhusu matatizo ya Afrika. Serikali ya SA inasema kwamba Dalai Lama akienda kule,basi watu wataongea kuhusu Tibet,na hiyo ni makosa,kwa sababu watu wakiwa Afrika,wanapaswa kuongea kuhusu Afrika. Hawa Waaafrika Kusini walipokuwa wanapigania uhuru,matatizo yao yalikuwa yanazungumzwa Duniani kote. Hivyo ndivyo walivyopata ushindi,pamoja na juhudi zao wenyewe. Dalai Lama pia anaweza kuzungumzia kuhusu Darfur na Somalia,lakini kama nchi yake haiko huru,matatizo yake lazima yaje kwanza. Miaka yote hapa Tanzania tulikuwa tunapinga udhalimu uliokuwa unafanyika Vietnam. Ile vita ilipokwisha tulikuwa na furaha kubwa.Nakumbuka Ndugu Kawawa aliitisha mkutano wa hadhara Jengo la Umoja wa Vijana wa CCM[TANU],kuwaeleza vijana kwamba,''Vietnam,vita imekwisha jana."'
Kwa hiyo itakuwa vizuri kama Rais Kikwete atamuagiza Waziri Membe amualike Dalai Lama na hawa watu wengine watukufu waje hapa Dar es Salaa wafanye huo mkutano,wasitafute refund ya ticket zao,badala yake waje Dar es Salaam. Labda pia tunahitaji kumwomba Balozi wa China ili tuweze kumualika Dalai Lama. Kuna mambo mengi sana kuhusu China ambayo hatuyafahamu.Tunaambiwa kwamba watu 35 milioni wamekihama Chama cha Kikomunisti. Watu wana manung'uniko mengi sana kule China.
Halafu mafundisho ya Dalai Lama yanaweza kuisaidia Afrika. Kwa sababu yule Guru Padmasambava,aliyeipeleka dini ya Budha Tibet,alipofika kule alikuwa na kazi kubwa ya kuzikabili imani za kishirikina. Kulikuwa na matatizo makubwa ya ushirikina,na Padmasambava aliitwa aende kule. Alikuwa anaishi India au Burma. Ninaposema ushirikina nina maana ushirikina. Huyu Padmasambava alikuwa ni mtu ambaye makazi yake ni makaburini. Akichoka kuishi katika makaburi sehemu fulani,anaenda kuishi katika makaburi sehemu nyingine. Kwa hiyo watu wa Tibet walipokuwa na matatizo na uchawi,wakamwita,kuona kama anaweza kuwasaidia. Dini yao ya Tibet,ambayo inaitwa ''Lamaism'',sasa hivi ni mchanganyiko wa dini ya Budha na dini ya asili. Halafu pia inafaa kueleza Dalai Lama ni mtu gani. Dalai Lama ni kiongozi wa Tibet ambaye habadiliki. Hakuna kura za kumchagua Dalai Lama. Hakuna Palace Coups. Dalai Lama peke yake ndiye anayeiongoza Tibet. Hiyo ndiyo Katiba yao. Dalai Lama anaongoza mpaka siku ya kufa kwake. Akifa mwili wake unahifadhiwa. Halafu imani yao ni kwamba roho yake inaingia katika mwili wa mtoto mdogo. Kwa hiyo wale Lama,ambao ndio mapadre wa Tibet,wanazunguka nchi nzima kutafuta Dalai Lama ametua wapi. Wakimpata huyo mtoto,ndie wanampeleka Potala,ambayo ndiyo Ikulu yao,kuwa Dalai Lama. Huyu ni mtoto bado,inabidi aende shule,halafu baadaye anakuwa Dalai Lama. Ndiyo maana huyu Dalai Lama wa sasa,anaitwa Dalai Lama wa 14,ina maana mabadiliko ya uongozi yamefanyika mara 14. Hata hivyo,inaaminiwa na Watibeti wengi kwamba Dalai huyu siyo reincarnation ya Dalai Lama wa 13. Hata yeye mwenyewe amesema hivyo,kwamba siyo reincarnation wa ''Chenrezi'',ambalo ndilo jina la Dali Lama wa 13. Huyu Dalai Lama alichaguliwa bila kujali usahihi wa chaguo. Alichaguliwa kuwafurahisha Wachina. Ina maana huyu Dalai Lama wanayempinga Wachina,alichaguliwa kuwafurahisha wao.
Kwa hiyo nadhani huu mkutano ni bora uletwe hapa Kempiski,wale Waskandinavia,waambiwe waulete huu mkutano hapa. They should be given alternative venues,if they should choose so. Huu ni mkutano wa amani. Wars cost money. Na hawa Wachina tumewaona jana wanaomboleza kifo cha mmoja wao aliyeuawa kikatili na majambazi. Hayo ndioy maadili tunayozungumzia.. Wars cost money,na sasa hivi kuna Financial Crsis Duniani. Pia siyo rahisi kuziuza kwa wananchi vita ya nchi moja ya Afrika kupigana na nchi nyingine ya Afrika.Nilikuwa nasoma jana katika gazeti moja la Marekani,kwamba kesi za litigation Marekani siku hizi zimekwenda out of fashion kwa ajili ya hii Financial Crisis,na walikuwa wanauliza lawyers wale wanaozitegema hizi kesi watafanya nini. Kwa hiyo inashangaza kuona Bw. Reginald Mengi na waandishi wa habari wanadaiana hela,wakati huu wa Financial crisis.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom