Wakati sisi na wanafunzi wengine wa Mkwawa tuliongeza hela ili tupande basi kutoka Iringa kwenda Dar moja kwa moja (mwaka 1970) wakati wa likizo ya shule, Andrew Nyerere aliendelea kutumia safari warrant ya shule ambaye ililazimisha wanafunzi kwenda na basi mpaka Dodoma na kuendelea na safari ya treni katika 3rd class kwenda Dar.
Pitapita,
Nataka kuhakikisha nimekuelewa vizuri. Unasema kwamba Andrew Nyerere alikuwa mwanafunzi Mkwawa High School, Iringa, mwaka 1970? Na kwamba ulikuwa naye shuleni Mkwawa?
Ilikuwaje hivyo?
Andrew Nyerere alikuwa mwanafunzi Tambaza High School mwaka huo wa sabini. Mimi pia nilikuwa Tambaza High School 1969 - 1970. Na niliishi katika H.H. The Aga Khan Hostel pamoja na Andrew Nyerere miaka hiyo. Tuliishi pamoja miaka miwili na tulionana kila siku.
H.H. The Aga Khan Hostel likuwa ni hosteli ya Kihindi, au niseme pia ya wanafunzi wa Kihindi pamoja na sisi Wafrika weusi.
Wanafunzi weusi tulikuwa ni wachache tu na tulifahimiana sote. Tuliishi pamoja na tulikula pamoja. Andrew Nyerere alikuwa nasi kila siku, kila asubuhi, kila mchana, na kila jioni tulipokwenda kula downstairs, on the ground floor, katika hosteli hiyo. Nilimwona kila siku mwaka huo 1970 tulipokuwa pamoja Tambaza High School na pia kabla ya mwaka huo, yaani tangu 1969. Pia nakumbuka sana alipenda kuvaa shati ya kijani na kaptura nyeusi nyakati mbali mbali kwa sababu alikuwa ni mwanachama wa TANU Youth League (TYL). Wengine walikuwa ni kina Mohmmed Chande Othman (now Tanzania's High Court Judge), Msafiri Abdallah, Balinagwe Mwambungu (mwandishi wa habari aliyestaafu), James Maugo (now a prominent advocate in Dar), na wengineo ambao pia walipenda kuvaa mavazi hayo kama members wa TYL. I throw this in to jog the memory of my schoolmates and classmates at Tambaza High School who are also members of JamiiForums. Na wote niliowataja wanamfahamu sana na wanamkumbuka sana Andrew Nyerere alipokuwa mwanafunzi na sisi sote pale Tambaza High School mwaka huo wa sabini (1970).
Swali kwako Pitapita ni hili: Angekuwaje na wewe kule Mkwawa High School mwaka huo wa sabini wakati alikuwa na sisi Tambaza High School na katika hosteli ya Aga Khan?
Na kama nilivyosema, wanafunzi weusi tulikuwa wachache katika shule hiyo na katika hosteli ya Aga Khan, Upanga. Na ninakumbuka sana kulikwa wanafunzi wawili tu wa Kihindi waliokuwa wana "socialize" na sisi. Mmoja alikuwa Hassanali kutoka Tanga ambaye alikuwa ni classmate wangu Form V na Form VI, Arts 1969 - 1970. Mwingine alikuwa ni Nizar, kijana mdogo mwenye umri kama miaka kumi na nne au kumi na tano. Kulikuwa na mwanafunzi mwingine, mmoja tu kati yetu sisi Wafrika weusi, ambaye alikuwa mwenye umri huo mdogo: Swai. Nakumbuka yeye pia, Swai, alipenda sana kuvaa shati ya kijani na kaptura nyeusi kwa sababu alikuwa ni member wa TANU Youth League. I was not.
Nizar, yule kijana mdogo wa Kihindi, alipenda sana kutembea na sisi kwenda mjini na kwenye beach karibu na Selandar Bridge. Muulize Balinagwe Mwambingu. Namkumbuka sana mwanafunzi huyo, Balinagwe, ambaye pia alikuwa ni classmate wangu, kwa sababu kijana yule wa Kihindi, Nizar, alipenda sana kumshika mkono kama kaka yake mkubwa nyakati za matembezi yetu. Hassanali pia alikwenda matembezini na sisi kwenye beach mara nyingi. Pia we spent hours on the roof of the hostel every evening, hasa sisi wanafunzi weusi pamoja na Andrew Nyerere, na mara nyingi pamoja na wanafunzi hao wawili wa Kihindi: Bwana mdogo Nizar na Hassanali.
Andrew Nyerere pia alifahamiana sana na kijana huyo mdogo wa Kihindi, Nizar, na alikuwa anatembea naye mara nyingi pamoja na mimi na wanafunzi wengine weusi. Nizar pia alikuwa member wa TANU Youth League na alikuwa anavaa shati ya kijani na kaptura nyeusi mara nyingi hata matembezin na sisi kama Andrew, Chande na wengineo. Mohammed Chande Othman (now the Judge) tulikuwa tunamwita kwa kifupi tu: Chande. Wanafunzi wenzangu wanakumbuka hayo yote. Pia Chande alikuwa ni rafiki ya Andrew - rafiki wa karibu sana.
Pia mara nyingi kila jioni kabla ya supper, in fact almost everyday, tulikuwa tunakwenda beach karibu na Selandar Bridge kupunga hewa. Na mwanafunzi mwenzetu mmoja, Msafiri Abdallah ambaye alikuwa ni classmate wangu kama Chande na Mwabungu na Hassanali, alikuwa na redio ambayo alikuwa anaichukua kwenda beach na sisi kila jioni. Pia nakumbuka alipenda sana - pamoja na sisi - kusikiliza taarifa ya habari saa zile za jioni kutoka Radio South Africa, Johannesburg. Naukumbuka hata wimbo (the bird was chirping really nice) wa ndege "chiriku" kabla ya taarifa kuanza kutangazwa. Mtangazaji wa habari ambaye alikuwa ni wa kiume - alikuwa ni wa kiume kila siku - alikuwa anaanzia hivi: "This is Radio South Africa, Johannesburg." Na Andrew Nyerere alikuwa na sisi nyakati zote hizo matembezini kwenda kwenye beach.
Pia kuna nyakati kabla ya kuvuka barabara pale karibu na Selandar Bridge, tulimwona Mwalimu Nyerere akirudi nyumbani Msasani. Tuliwahi kumpungia mikono na yeye alitupungia mkono akitabasamu. Tulimwona mara nyingi pale darajani ingawa hatukumpungia mikono kila tulipomwona. Mbele yake kulikuwa gari la polisi (shaped like a VW station wagon and blue in colour with an orange flashing light on top) na nyuma yake kulikuwa gari moja nyeupe (Peugeot 404) ya maofisa wa usalama waliokuwa wanamsindikiza Mwalimu kila jioni. Andrew Nyerere alikuwa na sisi nyakati hizo mara nyingi. Pia mahali pale ambapo tulikuwa tunavuka barabara kila siku karibu na Selandar Brdge ndiyo hapo ambapo ndege ya jeshi letu la anga (then called Tanzania Air Wing) ilianguka ikiendeshwa na Captain Mwaitebele (kutoka Kyela) na instructor wake kutoka Canada. Walifariki papo hapo. Ilikuwa ni mchana na tulikwenda kuiona ajali hiyo. Andrew Nyerere pia alikuwepo.
Halafu sasa, wewe Pitapita (mpita njia?), unasema Andrew Nyerere alikuwa Mkwawa High School kule Iringa - wakati najua kwa hakika, na wanafunzi wenzangu pale Tambaza pia wanajua kwa hakika, kwamba tulikuwa shuleni pamoja Tambaza mwaka huo wa sabini na kabla ya hapo?
Wanafunzi wengine pale Tambaza High School na H.H. The Aga Khan Hostel miaka ile pamoja na Andrew Nyerere walikuwa kina George Mazula (Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi), Nkya, Celestine Mwinula, Mlozi, Chinja, Godfrey Mwakikagile, Mukama, Jacob Msaki (daktari) na wale ambao nimeisha wataja - kina Mwambungu, Judge Mohammed Chande Othman na wengineo.
Na kuna wanafunzi wenzangu pale Tambaza (1969 - 1970 ) ambao ni members wa JF wanaojua nasema ukweli. Waulize kama Andrew Nyerere hakuwa Tambaza High School na H.H. The Aga Khan Hostel na sisi miaka hiyo. Na, wewe Pitapita, tueleze alikuwaje katika shule mbili - hundreds of miles apart at the same time.
Uongo huu unatokana na nini? Kisa ni nini? Chuki? Sababu ni kumchukia Mwalimu na watoto wake? Au nini?
Pia watu wengi katika JF, badala ya kuzumgumzia na kujadili issues muhimu kwa taifa, wanataka kuwa personal na wanapenda kuzungumzia mambo binafsi ya familia za watu na maisha yao pamoja na mambo mengine mengi ambayo hayatuhusu.
Show some respect. Pia mnapoteza muda.