Andrew Nyerere on Mwalimu humble children!

Andrew Nyerere on Mwalimu humble children!

Ingawa sikubaliani na wewe kwenye kusema Mwalimu hakuchangia HATA KIDOGO hatima ya watoto wake,

- Mkuu Fundi with all due respect, wazazi wako wamechangia vipi kwenye hatima ya maisha yako sasa hivi?

- Mwalimu alijitahidi kuwa kama mzazi yoyote mwingine wa wakati ule Tanzania, tizama mfano wa Freeman Mbowe, sio kweli kwamba kimaisha ndugu zake wote ni successful kama yeye, ingawa sio kwamba wana shida sasa how do you explain that, kwamba Mzee Mbowe RIP, alimlea Free tofauti na watoto wake wengine?

- Toka nimewafahamu watoto wa Mwalimu na Mwalimu mwenyewe, sikuwahi kusikia kwamba kuna mtoto wa Mwalimu ametaka kusoma nje yeye akamkatalia kama sisi wengine waazi wetu walivyokuwa, kwamba ametaka kuanzisha kampuni Mwalimu akakataa kumsaidia, watoto wa Mwalimu sio watu wanaopenda makuu, sio watu wa kujiweka kimbele mbele, sio wenye majivuno, sio waombaji na cha muhimu zaidi ni kwamba wako very close to each other, mmoja anapokuwa na shida huenda kwa mwingine na wote husaidiana, nakumbuka one time nyumbani kwa Madaraka, alipokuwa akiishi pale kwenye magorofa karibu na Zanaki Hostel, palikuwa pamejaa ndugu zake kibao toka Butiama na huku baba yakle akiwa ni rais,

- Kwa hiyo ni clear kwamba Mwalimu aliwafundisha umoja, kama Mwalimu anahusika na hatma ya watoto wake ni so minimum kama vile wazazi wetu wanavyohusika na hatma zetu, meaning kwamba he did kama ambavyo wazazi wengine walivyotulea, and I do not see anything to be wrong, ya maisha ya sasa ya watoto wake ni wao wenyewe ndio wameamua, Mwalimu hahusiki kabisaa.

FMES
 
- Mkuu Fundi with all due respect, wazazi wako wamechangia vipi kwenye hatima ya maisha yako sasa hivi?

- Mwalimu alijitahidi kuwa kama mzazi yoyote mwingine wa wakati ule Tanzania, tizama mfano wa Freeman Mbowe, sio kweli kwamba kimaisha ndugu zake wote ni successful kama yeye, ingawa sio kwamba wana shida sasa how do you explain that, kwamba Mzee Mbowe RIP, alimlea Free tofauti na watoto wake wengine?

- Toka nimewafahamu watoto wa Mwalimu na Mwalimu mwenyewe, sikuwahi kusikia kwamba kuna mtoto wa Mwalimu ametaka kusoma nje yeye akamkatalia kama sisi wengine waazi wetu walivyokuwa, kwamba ametaka kuanzisha kampuni Mwalimu akakataa kumsaidia, watoto wa Mwalimu sio watu wanaopenda makuu, sio watu wa kujiweka kimbele mbele, sio wenye majivuno, sio waombaji na cha muhimu zaidi ni kwamba wako very close to each other, mmoja anapokuwa na shida huenda kwa mwingine na wote husaidiana, nakumbuka one time nyumbani kwa Madaraka, alipokuwa akiishi pale kwenye magorofa karibu na Zanaki Hostel, palikuwa pamejaa ndugu zake kibao toka Butiama na huku baba yakle akiwa ni rais,

- Kwa hiyo ni clear kwamba Mwalimu aliwafundisha umoja, kama Mwalimu anahusika na hatma ya watoto wake ni so minimum kama vile wazazi wetu wanavyohusika na hatma zetu, meaning kwamba he did kama ambavyo wazazi wengine walivyotulea, and I do not see anything to be wrong, ya maisha ya sasa ya watoto wake ni wao wenyewe ndio wameamua, Mwalimu hahusiki kabisaa.

FMES

Mkuu. Wazazi wangu wamechangia kwa kiasi kikubwa sana mafanikio nyeyote niliyo nayo. Bila wazazi wangu kunikazia shurubu nisome , huu ufundi mchundo ningeusikia tu. Bila wazazi wangu kuniuliza KILA jioni kama nimefanya homework zangu, nisingefika hapa. Bila wazazi wangu kuhakikisha kila mwisho wa term wanasoma report yangu na kutaka kujua kulikoni kwenye masomo niliyofanya vibaya, nisingefika hapa. Bila wazazi wangu kuwa karibu na walimu kutaka kujua maendeleo yangu shuleni, nisingefika hapa. Bila wazazi wangu kunikatalia nilipotaka kuwaiga wenzangu ambao niliona ni mabitozi, nisingefika hapa. Bila wazazi wangu kuhakikisha kuwa nyumbani napata chakula, nina mahali pa kulala na nguo za kunisetitiri, nisingefika hapa. Bila wazazi wangu kunionyesha kwa mifano yao, faida ya elimu, nisingefika hapa. Vitu vyote hivi vinapaswa kufanywa na wazazi wenyewe kama wapo na si vinginevyo.

Mwalimu mwenyewe amewahi kukiri kuwa moja ya vitu anavyojutia ni kutokuwa karibu na watoto wake. Alitoa mfano wa Madaraka kuwa alienda Canada kwa juhudi zake mwenyewe na si kwa msaada wake. sasa kama mwenyewe aliona kuwa alipungukiwa kwenye duty yake ya ubaba, sisi ni nani tuseme otherwise. Mapenzi ya mzazi kwa mtoto yanahitaji kuonyeshwa kwa vitendo na si kwa remote control kama alivyofanya. Ndiyo maana Obama ameapa kuwa atahakikisha kuwa kila iwezekanavyo atakula chakula cha jioni na familia yake, atawafunika mashuka mabinti zake na kuwapeleka shule. Uwezo wa kukodi watu wa kumfanyia vyote hivyo anao lakini anajua hakuna kinachoweza ku-replace presence ya mzazi mwenyewe! Hakuna faraja kwa mtoto kama kujua wazazi wake wanamjali! Mzazi atakiwa ku-preempt matatizo ya mwanae. Mzazi haungoji kuombwa bali unamshauri mtoto wako. Kama unaona anastahili kuendelea na masomo, mnamshauri hata kabla yeye mwenyewe hajafikiria. Kama unaona anataka kuanzisha biashara, unamshauri hata bila yeye kukuomba. Mzazi anayengoja mtoto wake amuombe ndio amsaidie, basi ana walakin!

Amandla.........
 
Mkuu. Wazazi wangu wamechangia kwa kiasi kikubwa sana mafanikio nyeyote niliyo nayo. Bila wazazi wangu kunikazia shurubu nisome , huu ufundi mchundo ningeusikia tu. Bila wazazi wangu kuniuliza KILA jioni kama nimefanya homework zangu, nisingefika hapa. Bila wazazi wangu kuhakikisha kila mwisho wa term wanasoma report yangu na kutaka kujua kulikoni kwenye masomo niliyofanya vibaya, nisingefika hapa. Bila wazazi wangu kuwa karibu na walimu kutaka kujua maendeleo yangu shuleni, nisingefika hapa. Bila wazazi wangu kunikatalia nilipotaka kuwaiga wenzangu ambao niliona ni mabitozi, nisingefika hapa. Bila wazazi wangu kuhakikisha kuwa nyumbani napata chakula, nina mahali pa kulala na nguo za kunisetitiri, nisingefika hapa. Bila wazazi wangu kunionyesha kwa mifano yao, faida ya elimu, nisingefika hapa. Vitu vyote hivi vinapaswa kufanywa na wazazi wenyewe kama wapo na si vinginevyo.

Mwalimu mwenyewe amewahi kukiri kuwa moja ya vitu anavyojutia ni kutokuwa karibu na watoto wake. Alitoa mfano wa Madaraka kuwa alienda Canada kwa juhudi zake mwenyewe na si kwa msaada wake. sasa kama mwenyewe aliona kuwa alipungukiwa kwenye duty yake ya ubaba, sisi ni nani tuseme otherwise. Mapenzi ya mzazi kwa mtoto yanahitaji kuonyeshwa kwa vitendo na si kwa remote control kama alivyofanya. Ndiyo maana Obama ameapa kuwa atahakikisha kuwa kila iwezekanavyo atakula chakula cha jioni na familia yake, atawafunika mashuka mabinti zake na kuwapeleka shule. Uwezo wa kukodi watu wa kumfanyia vyote hivyo anao lakini anajua hakuna kinachoweza ku-replace presence ya mzazi mwenyewe! Hakuna faraja kwa mtoto kama kujua wazazi wake wanamjali! Mzazi atakiwa ku-preempt matatizo ya mwanae. Mzazi haungoji kuombwa bali unamshauri mtoto wako. Kama unaona anastahili kuendelea na masomo, mnamshauri hata kabla yeye mwenyewe hajafikiria. Kama unaona anataka kuanzisha biashara, unamshauri hata bila yeye kukuomba. Mzazi anayengoja mtoto wake amuombe ndio amsaidie, basi ana walakin!

Amandla.........

Fundi Mchundo:

Makuzi ya vijana yanategemea mambo mengi moja wapo ni mazingira, chakula, wazazi, genes za urithi na mambo mengi. katika yote hayo wazazi wanachangia kiasi kikubwa.

Yote uliotaja hapo ni sahihi kabisa. Kwa kuongezea tu ni wazazi wanaochagua mazingira ya mtoto wao kulelewa. Shule ya kusoma hiko kwenye mazingira. Leo hii kuna watanzania wanajinyima hili watoto wao wapelekwe kwenye shule za Saint Zakumi hili wajifunze kwa kiingereza.

Ni wazazi wanaochagua chakula cha mtoto wao. Ni wazazi wanaochagua potential mates.

Na sera za elimu ya Tanzania, kuna mafanikio madogo kwa sababu siku zote anaangaliwa mtoto bila kujali mazingira ya wazazi wake.
 
Duh,

Kuna mtu anataka ku undermine mchango wa wazazi?

Kuna watu hawajalelewa na wazazi au ni ushashi tu?
 
Duh,

Kuna mtu anataka ku undermine mchango wa wazazi?

Kuna watu hawajalelewa na wazazi au ni ushashi tu?

Kwa Tanzania kuna watu baada ya kusoma walikataa wazazi wao. Walio aibu kuwa wazazi wao ni aveleji.
 
Nyinyi wote kama sio watoto wa Nyerere mtakuwa mna speculate tu jinsi watoto wa Nyerere walivyolelewa.

Halafu kama wao hawamlaumu baba na mama yao kwa malezi waliyowapatia, nyie mnaomlaumu Nyerere tatizo lenu nini?
 
Nyinyi wote kama sio watoto wa Nyerere mtakuwa mna speculate tu jinsi watoto wa Nyerere walivyolelewa.

Halafu kama wao hawamlaumu baba na mama yao kwa malezi waliyowapatia, nyie mnaomlaumu Nyerere tatizo lenu nini?

Unajuaje kuwa kati yetu hamna mtoto wa Nyerere?
 
Hapo tutakuwa tunatoka nje ya mada. Humu tumeshakuwa na side shows nyingi na sitaki kuongezea.
Aaaaah mkuu wangu sasa hapa unayumba...nilisubiri sana kuona hizo nukuu baada ya Hapa Petu kuuliza.Sasa kama unatutolea nje itakuwa kazi mpyaa!
Dondosha nazi hizo mkuu wangu, uwe kama umekosea vile, napenda sana kujifunza!..
 
Fundi Mchundo:

Makuzi ya vijana yanategemea mambo mengi moja wapo ni mazingira, chakula, wazazi, genes za urithi na mambo mengi. katika yote hayo wazazi wanachangia kiasi kikubwa.

Yote uliotaja hapo ni sahihi kabisa. Kwa kuongezea tu ni wazazi wanaochagua mazingira ya mtoto wao kulelewa. Shule ya kusoma hiko kwenye mazingira. Leo hii kuna watanzania wanajinyima hili watoto wao wapelekwe kwenye shule za Saint Zakumi hili wajifunze kwa kiingereza.

Ni wazazi wanaochagua chakula cha mtoto wao. Ni wazazi wanaochagua potential mates.

Na sera za elimu ya Tanzania, kuna mafanikio madogo kwa sababu siku zote anaangaliwa mtoto bila kujali mazingira ya wazazi wake.

Kosa lingine tunalolifanya hasa wale kati yetu wenye kanafasi kidogo ni kudhani kuwa unaweza ku-outsource majukumu ya mzazi. Tunawaachia mahausgel na watu baki jukumu la kutulelea watoto. Tunawapeleka mbali nasi ( huko kwenye skuli za Saint Zakumi) watoto wetu wakiwa katika umri ambao unahitaji mapenzi na kuwepo kwa mzazi. Wengine tunadhani kuwa karibu na watoto wetu ni kuwadekeza. Matokeo ndio hayo. Watoto wana rebel ( wanafanya fujo, wanakuwa watukutu, walevi n.k) ili tutambue kuwepo kwao. Na huo ushirikiano anaouzungumzia FMES inawezekana (si lazima) unatokana na watoto wakiwa wadogo kutambua kuwa inabidi wao waungane maana wazazi si wa kuwategemea. Katika formative years ni muhimu mno mzazi kuwepo katika maisha ya mwanae. Wenzetu wanasema huo ndiyo wakati wa ku-bond! Ukiuchezea wakati huo, ndiyo basi.
 
Mkuu. Wazazi wangu wamechangia kwa kiasi kikubwa sana mafanikio nyeyote niliyo nayo. Bila wazazi wangu kunikazia shurubu nisome , huu ufundi mchundo ningeusikia tu. Bila wazazi wangu kuniuliza KILA jioni kama nimefanya homework zangu, nisingefika hapa. Bila wazazi wangu kuhakikisha kila mwisho wa term wanasoma report yangu na kutaka kujua kulikoni kwenye masomo niliyofanya vibaya, nisingefika hapa. Bila wazazi wangu kuwa karibu na walimu kutaka kujua maendeleo yangu shuleni, nisingefika hapa. Bila wazazi wangu kunikatalia nilipotaka kuwaiga wenzangu ambao niliona ni mabitozi, nisingefika hapa. Bila wazazi wangu kuhakikisha kuwa nyumbani napata chakula, nina mahali pa kulala na nguo za kunisetitiri, nisingefika hapa. Bila wazazi wangu kunionyesha kwa mifano yao, faida ya elimu, nisingefika hapa. Vitu vyote hivi vinapaswa kufanywa na wazazi wenyewe kama wapo na si vinginevyo.

Mwalimu mwenyewe amewahi kukiri kuwa moja ya vitu anavyojutia ni kutokuwa karibu na watoto wake. Alitoa mfano wa Madaraka kuwa alienda Canada kwa juhudi zake mwenyewe na si kwa msaada wake. sasa kama mwenyewe aliona kuwa alipungukiwa kwenye duty yake ya ubaba, sisi ni nani tuseme otherwise. Mapenzi ya mzazi kwa mtoto yanahitaji kuonyeshwa kwa vitendo na si kwa remote control kama alivyofanya. Ndiyo maana Obama ameapa kuwa atahakikisha kuwa kila iwezekanavyo atakula chakula cha jioni na familia yake, atawafunika mashuka mabinti zake na kuwapeleka shule. Uwezo wa kukodi watu wa kumfanyia vyote hivyo anao lakini anajua hakuna kinachoweza ku-replace presence ya mzazi mwenyewe! Hakuna faraja kwa mtoto kama kujua wazazi wake wanamjali! Mzazi atakiwa ku-preempt matatizo ya mwanae. Mzazi haungoji kuombwa bali unamshauri mtoto wako. Kama unaona anastahili kuendelea na masomo, mnamshauri hata kabla yeye mwenyewe hajafikiria. Kama unaona anataka kuanzisha biashara, unamshauri hata bila yeye kukuomba. Mzazi anayengoja mtoto wake amuombe ndio amsaidie, basi ana walakin!

Amandla.........

- Mkuu Fundi, unasema wazazi wote wa bongo waliweza kufanya haya unayoyasema isipokuwa Mwalimu tu?

- Kwa hiyo wabongo wote walio na maisha mazuri leo ni kwa sababu wazazi wao walifanya hayo unayosema wazazi wako walikufanyia?

- Je hata ndugu zako wote uliozaliwa nao wana maisha mazuri kama wewe, maana ninataka kuamini kuwa unayo au?

FMES!
 
Aaaaah mkuu wangu sasa hapa unayumba...nilisubiri sana kuona hizo nukuu baada ya Hapa Petu kuuliza.Sasa kama unatutolea nje itakuwa kazi mpyaa!
Dondosha nazi hizo mkuu wangu, uwe kama umekosea vile, napenda sana kujifunza!..

Mkandara:

Msimamo wangu utabaki palepale kwa sababu nitatoa namba ambazo zinaweza kubadilisha sura za mjadala mzima. Uache mjadala uwe katika masuala ya familia ya mwalimu na malezi ya watoto.

Naelewa you were clearning your gun powder hili ujibu vipande vyangu. Sorry Chale.
 
Kosa lingine tunalolifanya hasa wale kati yetu wenye kanafasi kidogo ni kudhani kuwa unaweza ku-outsource majukumu ya mzazi. Tunawaachia mahausgel na watu baki jukumu la kutulelea watoto. Tunawapeleka mbali nasi ( huko kwenye skuli za Saint Zakumi) watoto wetu wakiwa katika umri ambao unahitaji mapenzi na kuwepo kwa mzazi. Wengine tunadhani kuwa karibu na watoto wetu ni kuwadekeza. Matokeo ndio hayo. Watoto wana rebel ( wanafanya fujo, wanakuwa watukutu, walevi n.k) ili tutambue kuwepo kwao. Na huo ushirikiano anaouzungumzia FMES inawezekana (si lazima) unatokana na watoto wakiwa wadogo kutambua kuwa inabidi wao waungane maana wazazi si wa kuwategemea. Katika formative years ni muhimu mno mzazi kuwepo katika maisha ya mwanae. Wenzetu wanasema huo ndiyo wakati wa ku-bond! Ukiuchezea wakati huo, ndiyo basi.

- Fundi tunamsingizia Mwalimu maneno mengi sana ambayo hayana ukweli kabisa, Mwalimu alikuwa akiwapenda sana watoto wake kinyume kabisa na tunayoambiwa kila siku na wanaomchukia, ninakumbuka siku moja askari pale Ikulu alimchapa kibao Andrew mkuu waulize walijionea kilichompata yule askari,

- Ninakumbuka onetime Mwalimu ameenda Japan, akapewa big screen TV la nchi 52 na Sony, akalichukua na kuja nalo bongo na yeye mwenyewe kumpa mtoto wake Madaraka, eti huyu ni yule Mwalimu ambaye tunaambiwa kuwa alikuwa hapendi makubwa? alikuwa hapendi TV? Alikuwa hapendi watoto wake? Alikuwa hapendi vitu vizuri? Please!

- Hivi ni wapi watoto wa Mwalimu wamelalamika kwamba baba yao hakuwa na mapenzi nao? Where? Na ni wapi hapo Mwalimu aliposema kwamba hakuwa karibu na watoto wake? Ni rais wa Nchi gani ambaye yuko karibu sana na watoto wake? Kuwafunika mablanketi watoto saa ya kulala ni kazi ya mama yao kwa sisi waa-Africa mkuu, sio baba, kuwapikia watoto ndio hasa sababu ya kuoa mke kwa sisi waa-Africa, angalieni sana jamani hizo tabia za kizungu, sisi ni wabongo yaani Africans.

Tumlaumu Mwalimu kwa mengine, labda ya siasa lakini ya watoto, hatujui ya ndani kwake yaani sisi tunaweza kujua kama Mwalimu aliwatandikia vitanda watoto wake au hapana? Sasa wewe unamuona huyu Obama ni sawa kweli wmwanaume mzima kwenda kutandikia watoto vitanda, Mkuu fundi pole pole msituambukize uzungu mkuu, sisi ni wabongo, tunaendeleza mila na desturi baba ni baba tu hawezi kuanza kutandika vitanda vya watoto, mimi sitandiki vitanda vya watoto wangu na hakuna noma mkuu!.

- Hayo ya Ku-bond waachieni wazungu, sio yetu wa-Africa.

Respect.

FMEs!
 
- Fundi tunamsingizia Mwalimu maneno mengi sana ambayo hayana ukweli kabisa, Mwalimu alikuwa akiwapenda sana watoto wake kinyume kabisa na tunayoambiwa kila siku na wanaomchukia, ninakumbuka siku moja askari pale Ikulu alimchapa kibao Andrew mkuu waulize walijionea kilichompata yule askari,

- Ninakumbuka onetime Mwalimu ameenda Japan, akapewa big screen TV la nchi 52 na Sony, akalichukua na kuja nalo bongo na yeye mwenyewe kumpa mtoto wake Madaraka, eti huyu ni yule Mwalimu ambaye tunaambiwa kuwa alikuwa hapendi makubwa? alikuwa hapendi TV? Alikuwa hapendi watoto wake? Alikuwa hapendi vitu vizuri? Please!

- Hivi ni wapi watoto wa Mwalimu wamelalamika kwamba baba yao hakuwa na mapenzi nao? Where? Na ni wapi hapo Mwalimu aliposema kwamba hakuwa karibu na watoto wake? Ni rais wa Nchi gani ambaye yuko karibu sana na watoto wake? Kuwafunika mablanketi watoto saa ya kulala ni kazi ya mama yao kwa sisi waa-Africa mkuu, sio baba, kuwapikia watoto ndio hasa sababu ya kuoa mke kwa sisi waa-Africa, angalieni sana jamani hizo tabia za kizungu, sisi ni wabongo yaani Africans.

Tumlaumu Mwalimu kwa mengine, labda ya siasa lakini ya watoto, hatujui ya ndani kwake yaani sisi tunaweza kujua kama Mwalimu aliwatandikia vitanda watoto wake au hapana? Sasa wewe unamuona huyu Obama ni sawa kweli wmwanaume mzima kwenda kutandikia watoto vitanda, Mkuu fundi pole pole msituambukize uzungu mkuu, sisi ni wabongo, tunaendeleza mila na desturi baba ni baba tu hawezi kuanza kutandika vitanda vya watoto, mimi sitandiki vitanda vya watoto wangu na hakuna noma mkuu!.

- Hayo ya Ku-bond waachieni wazungu, sio yetu wa-Africa.

Respect.

FMEs!

FMES. With all due respect, si peke yako uliyekuwa ukisikiza hotuba au mahojiano ya Nyerere. Ni uamuzi wako kuniamini au kutoniamini kuhusu haya niliyoyasema. Mbona unakuwa mwepesi sana kudai uthibitisho wakati unataka tuchukue usemayo kama gospel truth?

Hakuna mtu aliyesema kuwa Nyerere alikuwa hawapendi watoto wake. Aliwapenda sana na ndiyo maana alisema aliyoyasema. Kinachozungumziwa hapa ni involvement yake katika maisha yao ya kila siku. Ni siri iliyo wazi kuwa Butiku ndiye aliyekuwa akitatua matatizo yao madogomadogo.


Mtoto ni mtoto ni mtoto. Hakuna cha uzungu katika malezi. Ni dhana potovu na iliyopitwa na wakati kudai kuwa mtu anaepaswa kuwa karibu na watoto ni mama. Baba kazi yake ni kutafuta, kukaa kilabu na kucharaza bakora. Kama baba anataka kuwapikia watoto wake sioni kitakachoharibika. Mbona hatuoni shida ma-hausboi kutupikia? Au ndiyo uzungu uliokubalika?

Kama unaona ukitandika kitanda cha mtoto wako kitakupunguzia status yako kama mwanaume, hilo ni lako. Wengine wanajivunia kubadilisha nepi watoto wao na sijaona status yao ikishuka. Na ni waafrika kama wewe na mimi. Mbona huko ughaibuni hamlazimishi kuchapa bakora watoto wenu? Si ni sisi tuaminio kuwa bila bakora mtoto haleleki! Msitake kutulazimisha kuwa antiquated machoism yenu ndiyo yetu sote. Uafrika wako si uafrika wangu.

Amandla......
 
Mzee angalia sana usemi huu. Unawapa watoto Western Education, Western Upbringing na baadaye ku-bond ni kwa wazungu tu.

- Hata hao wazuingu hawan bond yoyote na watoto wao ni maneno tu, wangekua wasingekua wanalala Nursing home, wazungu wanajitahidi kujifanya ku-bond ili kujikomba kwa watoto wao wasiwatupe Nursing Home wakizeeka lakini watoto wao wanaishia kuwatupa anyways bila kuwajali,

- Mimi siwezi kuwatupa wazazi wangu Nursing Home hata siku moja, ya wazun gu tuwaachie wazungu sio kila kitu cha wazungu ni kizuri, unafikiri ni kwa nini Marvin Gaye alipigwa risasi na baba yake mzazi na ni huko uzunguni na wao ni mabingwa wa ku-bond? Lini uliwahi kusikia bongo baba kapiga mtoto wake risasi?

Respect.

FMES!
 
- Mkuu Fundi, unasema wazazi wote wa bongo waliweza kufanya haya unayoyasema isipokuwa Mwalimu tu?

- Kwa hiyo wabongo wote walio na maisha mazuri leo ni kwa sababu wazazi wao walifanya hayo unayosema wazazi wako walikufanyia?

- Je hata ndugu zako wote uliozaliwa nao wana maisha mazuri kama wewe, maana ninataka kuamini kuwa unayo au?

FMES!

Sijasema wazazi wote walifanya niliyofanyiwa. Sijasema kuwa Mwalimu hakufanya yote niliyofanyiwa. Umeuliza nafasi ya mzazi wangu katika maisha YANGU, nami nimekujibu. Sijaishi Ikulu, siwajui watoto wa Mwalimu kwa hiyo siwezi kuzungumzia maisha yao ya kila siku nje ya yale yaliyokuwa katika public forum.

Mbona unaleta ubishi usio na msingi? Hakuna mahali niliposema kuwa mtu akitendewa nilivyotendewa mimi basi nae maisha yake yatakuwa na neema. Hakuna guarantee katika malezi lakini kuwa karibu na watoto wetu kunasaidia kuepusha matatizo ya baadae. Wako ambao pamoja na kutendewa yote haya na wazazi wao wameishia kubaya. Wako ambao pamoja na kutelekezwa, kunyanyaswa, kuteswa na wazazi yao wamefanikiwa.

Maisha ninayoona mimi ni mazuri pengine kwako ni shida tupu. Na maisha unayoyaona wewe ni mazuri pengine kwangu mimi ni fedheha tupu. Hicho nilichonacho namshukuru Mungu na wazazi wangu. Hayo ya ndugu wengine siwezi kukujibu maana mimi ni mtoto pekee!

Amandla..............
 


1. siwajui watoto wa Mwalimu kwa hiyo siwezi kuzungumzia maisha yao ya kila siku nje ya yale yaliyokuwa katika public forum.

2. Wako ambao pamoja na kutendewa yote haya na wazazi wao wameishia kubaya. Wako ambao pamoja na kutelekezwa, kunyanyaswa, kuteswa na wazazi yao wamefanikiwa.

3. Maisha ninayoona mimi ni mazuri pengine kwako ni shida tupu. Na maisha unayoyaona wewe ni mazuri pengine kwangu mimi ni fedheha tupu.

Amandla..............



- Tuko pamoja sana hapa mkuu.

Respect.

FMES!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom