Andrew Nyerere on Mwalimu humble children!

Andrew Nyerere on Mwalimu humble children!

I hope "wenzetu" hao sio hawa wenye nursery schools toka mtoto ana mwezi mmoja! mama huyo anarudi kazini!

Binadamu wanatofautiana. Wako wanaompeleka mtoto nursey akiwa na mwezi mmoja na wako wanaoacha kazi ili wawe na watoto wao. Na si wakina mama peke yao. Nawajua wanaume wengi waliopunguza saa zao za kufanya kazi ili wawe na muda zaidi na watoto wao. Pamoja na hayo, hata huko ughaibuni sijasikia boarding za nursery! Hao wanaopelekwa wakiwa na mwezi mmoja bado wanarudi nyumbani kwa wazazi wao kila siku. Lakini baadhi yetu hata kama hatuwapeleki watoto nursery bali mtoto anaachiwa hausgel 24/7! Go figure.
 
Nyinyi wote kama sio watoto wa Nyerere mtakuwa mna speculate tu jinsi watoto wa Nyerere walivyolelewa.

Halafu kama wao hawamlaumu baba na mama yao kwa malezi waliyowapatia, nyie mnaomlaumu Nyerere tatizo lenu nini?

Unajuaje kuwa kati yetu hamna mtoto wa Nyerere?

Nionyeshe niliposema najua kuwa kati yenu "hamna mtoto wa Nyerere?"
 

Halafu kama wao hawamlaumu baba na mama yao kwa malezi waliyowapatia, nyie mnaomlaumu Nyerere tatizo lenu nini?

Hatuwezi kuulizwa sisi tatizo letu nini, mpaka tuwe na uhakika kwamba na wao hawamo humu.

Katika "sisi tunaomlaumu" inawezekana na "wao" wamo humu wanalaumu.

Mimi na wewe hatujui.
 
Hatuwezi kuulizwa sisi tatizo letu nini, mpaka tuwe na uhakika kwamba na wao hawamo humu.

Newsflash..I just did!!!!

Katika "sisi tunaomlaumu" inawezekana na "wao" wamo humu wanalaumu.

Kweli inawezekana.....

Mimi na wewe hatujui.

Jiongelee mwenyewe. Ninachokijua na nisichokijua kuhusu familia ya Nyerere pamoja na kama watoto wake, baadhi au wote, wamo humu, wewe hukijui.
 
Last edited by a moderator:
Jiongelee mwenyewe. Ninachokijua na nisichokijua kuhusu familia ya Nyerere wewe hukijui.

Tunaongelea kujua kama na wao wamo humu.

Umesema "Nyinyi wote kama sio watoto wa Nyerere..."

Ina maana na wewe huna hakika, hujui, kama wamo humu.

Sijui, na hujui.
 
Tunaongelea kujua kama na wao wamo humu.

Umesema "Nyinyi wote kama sio watoto wa Nyerere..."

Ina maana na wewe huna hakika, hujui, kama wamo humu.

Sijui, na hujui.

Unajuaje sijui? Je, unajua mimi ni mtoto wa nani?
 
Nimejua kwa sababu, tofauti na wewe, watoto wote wa Mwalimu ni Watanzania wazawa.

Wewe umewahi kututaarifu, huhitaji makaratasi kupitia ndoa za mabwanyenye maana "mimi nimezaliwa hapa."

Kama nilikuwa nadanganya je? Wewe unaamini kila kitu kinachoandikwa na unachokisoma humu? Wee vipi wewe? Na hapo "hapa" ni wapi?

Ina maana kweli wewe ni "bwenga"?
 
Kama nilikuwa nadanganya je?

Wewe unaamini kila kitu kinachoandikwa humu?

Kama ulidanganya ina maana unamuonea aibu bwanyenye aliyekusaidia uhalali wa uwepo.

Kwani wewe unaamini kila kitu, ikiwemo kuamini kwamba mimi naamini kweli wewe ni "mzaliwa wa hapa"?
 
Kama ulidanganya ina maana unamuonea aibu bwanyenye aliyekusaidia uhalali wa uwepo.

Kwani wewe unaamini kila kitu, ikiwemo kuamini kwamba mimi naamini kweli wewe ni "mzaliwa wa hapa"?

Nini kilichokufanya uhitimishe kuwa uwepo wangu hapa ni wa kihalali hadi useme kuwa namwonea aibu "bwanyenye" aliyenisaidia? Kwani kuna njia moja tu ya kupata uhalali wa kuishi hapa? Na hapo "hapa" ni wapi?...maana hujui nilipo...

Na siamini kila kitu vikiwemo unavyoamini wewe. Kwanza sivijui unavyoviamini na ndio maana nikauliza...Nikuulize tena, wewe unaamini kila kitu kinachoandikwa humu?
 
Nini kilichokufanya uhitimishe kuwa uwepo wangu hapa ni wa kihalali hadi useme kuwa namwonea aibu "bwanyenye" aliyenisaidia? Kwani kuna njia moja tu ya kupata uhalali wa kuishi hapa?

Na hapo "hapa" ni wapi?...maana hujui nilipo...

Nimehitimisha kwamba unamuonea aibu bwanyenye aliyekusaidia kwa sababu ulivyoambiwa inakuwaje wewe mpaka leo bado unaongelea mahangaiko ya kuhalisha makazi na matipwatipwa ya sehemu ya nane ukajitetea kwamba wewe ulizaliwa hapa. Sasa kama ulidanganya ina maana ulimwonea aibu bwanyenye aliyekusaidia.

Hapo "hapa" inaweza kuwa sehemu yeyote ile duniani ambapo mpaka leo unajadili jinsi ya kujihalalishia makazi.
 
Nimehitimisha kwamba unamuonea aibu bwanyenye aliyekusaidia kwa sababu ulivyoambiwa inakuwaje wewe mpaka leo bado unaongelea mahangaiko ya kuhalisha makazi na matipwatipwa ya sehemu ya nane ukajitetea kwamba wewe ulizaliwa hapa. Sasa kama ulidanganya ina maana ulimwonea aibu bwanyenye aliyekusaidia.

Hapo "hapa" inaweza kuwa sehemu yeyote ile duniani ambapo mpaka leo unajadili jinsi ya kujihalalishia makazi.

Hujui mimi mtoto wa nani. Hiyo ndio bottom line. Asante na usiku mwema.
 
Lakini kweli Mwalimu aliamini kuwa wakati ule wa chama kimoja na hicho hicho kimeshika hatamu kuna mtu aliyekuwa na ubavu wa kunyang'anya nyumba yake? Au ilikuwa danganya toto tuu akijua kuwa watamsamehe tu?

Nakubaliana na wewe kabisa, hivi ni benki ofisa gani ambaye angediriki kumnyag'anya Rais Nyerere nyumba? Mwenyekiti wa Benki na mkurugenzi Mkuu ambao amewateua yeye wangekubali?

Hii inanikumbusha hekaya za Abunuwas alipotaka kuuza sehemu ya chini ya nyumba yake iliyopo kwenye jengo la ghorofa, alileta mafundi wakubomoa nyumba ya chini na kumuamuru mwenye nyumba ya juu ashikilie kwani anataka kuondoa nyumba yake iliyopo chini. ilichofuatia ni kwa mwenye nyumba ya juu kununua sehemu ya Abunuwas bila ya kupenda.

Practically, Nyerere asingerudisha ile nyumba isipokuwa alitumia 'hekima' ya kutaka kumalizana na benki kiaina
 
- Hata hao wazuingu hawan bond yoyote na watoto wao ni maneno tu, wangekua wasingekua wanalala Nursing home, wazungu wanajitahidi kujifanya ku-bond ili kujikomba kwa watoto wao wasiwatupe Nursing Home wakizeeka lakini watoto wao wanaishia kuwatupa anyways bila kuwajali,

- Mimi siwezi kuwatupa wazazi wangu Nursing Home hata siku moja, ya wazun gu tuwaachie wazungu sio kila kitu cha wazungu ni kizuri, unafikiri ni kwa nini Marvin Gaye alipigwa risasi na baba yake mzazi na ni huko uzunguni na wao ni mabingwa wa ku-bond? Lini uliwahi kusikia bongo baba kapiga mtoto wake risasi?

Respect.

FMES!

Mbona mara nyingi tunasikia watoto wameua mzazi bongo? Mara ngapi watoto wameua mama yao au shangazi yao kwa imani za kishirikina? Mara ngapi vijana wamewapiga panga au jembe wazazi yao kwa kutaka mali? Mama Liundi aliyewanywesha watoto wake sumu nae alikuwa mzungu?

Marvin Gaye alikuwa mteja. Alikuwa mtumiaji mzuri wa unga na siku ya tukio alikuwa amepandisha. Baba yake alimpiga risasi katika hatua za kujitetea. Alichofanya baba yake Marvin kama alivyofanya mama Liundi hakimaanishi kuwa jamii zao zote ziko kama wao.

Si heri hao wazungu wanaopeleka wazazi wao na vikongwe kwenye nursing home kuliko sisi tunaowapiga nondo kichwani kwa dhana za ushirikina? Tunavyowatendea vikongwe wenye Alzheimer (hao tunaowaita wanga ) na yenyewe unaona ni sifa? Vikongwe wangapi wametelekezwa na watoto wao hawana msaada wa mtoto, mjukuu wala serikali? Wangapi tunawaona wakiomba omba mitaani? Basi nasi sote tuhukumiwe kuwa hatujali wazazi wetu? Kipi bora, kumpeleka mzazi wako aliyepatwa na Alzheimer kwenye nursing home au kumwachia azurure mitaani ambako siku akijisahau na kuvua nguo atauawa kwa kuitwa mwanga?

Sio wote wanatupwa nursing home kwa sababu watoto hawawapendi. Kuna wakati unafika, mzazi anahitaji matunzo na nafasi ambayo ni mara chache inawezekana kumpatia nyumbani. Kama mwenzetu una nafasi ya kutosha ya kuweza kukaa na wazazi wako na kuwahudumia basi unastahili pongezi. Kukaa mbali nao na kupeleka vijisenti hakuna tofauti na wanao wapeleka nursing home maana nyote mna outsource majukumu yenu!

Amandla.......
 
Last edited:
Asubuhi njema, sio usiku mwema.

Ni takriban saa moja asubuhi Tanzania saa hizi, kama ungekuwa ni mtoto wa Mwalimu. Wametoka kuamka!

Umejuaje wote wako Tanzania sasa hivi? Na kama wote wako Tanzania, umejuaje kama wote wanaamka kwa wakati mmoja?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom