Itoshe kusema kada ya walimu imeingiliwa na mamluki!
Zamani ilikuwa rahisi sana kuwachambua walimu kwenye kundi la watu pasipo hata kujitambulisha, lakini sasa hivi kwenye kikundi cha watu mtaani wakichanganyika wa kike na kiume huwezi kutofauti uvaaji wa mwalimu na muimba singeli, wote utawaona wameshikilia dera, kofia za kitozi, mavazi ya kitozi, maongezi ya kihuni huni, umbeya ndio usiseme n.k. Hapo zamani mwalimu alitambulika kuanzia staha ya mavazi hadi uongeaji wa hekima.
Tabia za ajabu mashuleni
1. Ni kawaida sana sasa hivi kuambiwa mwalimu fulani huwa anatuuzia visheti na vipipi wakati wa vipindi darasani. Tabia kama hizi mwalimu anapozifanya darasani wakati wa vipindi zinadhihilisha, hajali tena heshima yake, hajali tena taaluma ya watoto n.k.
2. Tabia za kumsengenya mwalimu mwenzake darasani au kuwaonyesha watoto kwamba walimu fulani na fulani hawapatani, ni moja ya tabia ya ajabu sana.
3. Upigaji wa hovyo wa watoto wadogo pasipo kuzingatia utaratibu wa utoaji adhabu. Watoto wadogo wanapigwa kila sehemu ya mwili hadi kichwani wakati mwingine hata kwa mateke na ngumi. Huu siyo ufindishaji ni uuaji.
4. Utongozaji wa kishamba wa watoto na ubakaji, yaani takwimu za makadirio kwasasa katika walimu 100, asilimia 5% wanajihusisha kimapenzi na wanafunzi. Hivyo tukiamua kupiga kura ya siri shuleni ni aibu tupu kwa walimu, tena wengine ni walimu wakuu.
5. Kushiriki kuiba mali za shule, vitendea kazi, vifaa vya usafi au mali iliyopo kwenye himaya ya shule.
6. Michezo ya upatu na makundi yasiyoeleweka n.k.
Kiufupi shuleni imekuwa ni biashara na mapenzi halafu taaluma bora liende. Anaewadhalilisha walimu ni matendo yao, Serikali isichoke kuwafanyia semina walimu mara kwa mara.
Pia kwa wale walimu wanaofanya vizuri wapongezwe, siyo kila siku taarifa mbaya tu mwalimu kaua, kabaka n.k.
Zamani ilikuwa rahisi sana kuwachambua walimu kwenye kundi la watu pasipo hata kujitambulisha, lakini sasa hivi kwenye kikundi cha watu mtaani wakichanganyika wa kike na kiume huwezi kutofauti uvaaji wa mwalimu na muimba singeli, wote utawaona wameshikilia dera, kofia za kitozi, mavazi ya kitozi, maongezi ya kihuni huni, umbeya ndio usiseme n.k. Hapo zamani mwalimu alitambulika kuanzia staha ya mavazi hadi uongeaji wa hekima.
Tabia za ajabu mashuleni
1. Ni kawaida sana sasa hivi kuambiwa mwalimu fulani huwa anatuuzia visheti na vipipi wakati wa vipindi darasani. Tabia kama hizi mwalimu anapozifanya darasani wakati wa vipindi zinadhihilisha, hajali tena heshima yake, hajali tena taaluma ya watoto n.k.
2. Tabia za kumsengenya mwalimu mwenzake darasani au kuwaonyesha watoto kwamba walimu fulani na fulani hawapatani, ni moja ya tabia ya ajabu sana.
3. Upigaji wa hovyo wa watoto wadogo pasipo kuzingatia utaratibu wa utoaji adhabu. Watoto wadogo wanapigwa kila sehemu ya mwili hadi kichwani wakati mwingine hata kwa mateke na ngumi. Huu siyo ufindishaji ni uuaji.
4. Utongozaji wa kishamba wa watoto na ubakaji, yaani takwimu za makadirio kwasasa katika walimu 100, asilimia 5% wanajihusisha kimapenzi na wanafunzi. Hivyo tukiamua kupiga kura ya siri shuleni ni aibu tupu kwa walimu, tena wengine ni walimu wakuu.
5. Kushiriki kuiba mali za shule, vitendea kazi, vifaa vya usafi au mali iliyopo kwenye himaya ya shule.
6. Michezo ya upatu na makundi yasiyoeleweka n.k.
Kiufupi shuleni imekuwa ni biashara na mapenzi halafu taaluma bora liende. Anaewadhalilisha walimu ni matendo yao, Serikali isichoke kuwafanyia semina walimu mara kwa mara.
Pia kwa wale walimu wanaofanya vizuri wapongezwe, siyo kila siku taarifa mbaya tu mwalimu kaua, kabaka n.k.