Emmanuel Tengulaga
Member
- May 17, 2020
- 17
- 4
Ni kweliNimekuwa nikifuatilia mambo kadha wa kadha ambayo yanajitokeza katika taifa, nimeona tuna Rais anayetumia muda mrefu sana kufanya maamuzi makubwa na ya maana.
Kwa mfano hili janga la Covid-19 tangu limeanza hadi sasa hakuna hatua za msingi zilizochukuliwa kudhibiti maambukizi ya kuenea kwake.
Watu mbalimbali wamekuwa wakitoa mapendekezo mbalimbali kuhusu kulikabili jambo hili kama vile kufunga mipaka, kuifunga (lock down) Dar es salaam kwa muda, Benki kuu kuuhami uchumi, kusambaza vifaa vya kupima ugonjwa nchi nzima, n.k.
Yeye anawaza kukusanya kodi tu ndio maana hata tamko la mkuu wa mkoa wa Mbeya la kufunga baa mapema amelifutilia mbali. Hadi sasa amepumzika tu anasubiri hadi mambo yaharibike ndio achukue hatua.
Jambo pekee analoweza kulifanya kwa haraka ni KUFUKUZA WATU KAZI isipokuwa Makonda pekee.
Mlio karibu naye hata kama mnamwogopa kwenye hili pigeni moyo konde mumwambie.
Sent using Jamii Forums mobile app
BUNGE LIMEKUWA NA KAZI YA KUSIFU TU, WAKOSOAJI NA WASHAURI WANAFANYIWA VISA VINGI, KIONGOZI WAO NI WAHOVYO KABISA HUYO SPIKAWastaafu nao kimya!!
Mitandao tu ndio kwa sasa inasaidia kukosoa na kushauri vinginevyo hata baadhi ya hatua zinazochukuliwa huenda zisingekuwepo pasipo kelele za watu mitandaoni.
Bunge kwa sasa nalo msaada wake ni mdogo sana katika kuishauri na kuisimamia serikali.
Ukiona mtu anabeza kitu anachokifanya Rais wetu ukiona mtu anabeza unapata mashaka ya vinasaba vyake
Sent using Jamii Forums mobile app
Vinasaba (DNA) imekuwaje!?Kuna vinasaba (dna) ya mtanzania?
Nipe biological composition yake!
Mpumbavu ni yule ambaye hajui kuwa watu wanamjua kuwa yeye ni mpumbavuKuna mpumbavu mmoja kasema eti asiempenda Magufuli hana vinasaba vya Tanzania!
Nikaamua kumuuliza hivyo...maana sentensi yake hiyo ni the most stupidious to ever come from human basket mouth!
Mpumbavu zaidi ni yule anaeona wenzake wapumbavu kumbe yeye ndio mpumbavu zaidi!Mpumbavu ni yule ambaye hajui kuwa watu wanamjua kuwa yeye ni mpumbavu
Sent using Jamii Forums mobile app
Watu watoe nyongo wapendavyo. Ni aina mojawapo ya tiba pia !!!hua najiuliza sana uongoz wa jf, hii thread imekua pinned kana kwamba ni habari kubwa sana ...kwa lengo lipi?
Sent using Jamii Forums mobile app
kama hujui unapokwenda... basi huwezi kupotea.
Mwalimu Nyerere aliwahi kusema, "Hatuwezi kuwa na Rais ambaye hatujui kesho ataamka amefikiria nini au ameshauriwa nini na mke wake". Kwa wakati ule kilionekana ni kijembe kwa mzee Mwinyi lakini leo kauli yake inaonyesha maana.
Hatujui mwelekeo wa nchi kiukweli, hatujui kesho atafukuzwa na nani au ziara ya Rais au Waziri Mkuu itakuwa wapi. Hatujui kama tutaamka tunafagia barabara au tutaingia ofisini kwetu kama kawaida.
Hatujui tunaanza na nini, kujenga viwanda au kuboresha miundombinu na kuimarisha kilimo ili tupate malighafi.
Hatujui tatizo la sukari kwa mfano linaondoka kwa kurekebisha viwanda vyetu na kuongeza uzalishaji wa miwa au kuruhusu sukari ya nje au tuvamie magodauni ya watu.
Ukimuangalia usoni na ukasikia anachotamka unakiri ana nia kabisa ya kututoa hapa. Swali ni je, anajua jinsi ya kututoa?! Anajua anakotupeleka?
Nimejitahidi kuangalia Bunge ili nione labda Mawaziri wake wanaweza kuonyesha mwelekeo, huko nikachanganyikiwa zaidi.
Mwanamtandao mmoja alisema unaweza kuwa na dereva mzuri anayefuata sheria zote za barabarani lakini hajui anaenda wapi!
[/QUO
Anatupeleka kwenye nchi ya viwanda