Nyani Ngabu ,kwanza nikupongeze kwa kuanzisha mada nzuri sana na wakati muafaka lakini nasikitika kuwa kwa standard ya JF ya sasa hii mada itaonekana haina maana lakini ingekuwa mada nzuri sana kama tungepunguza ushabiki wa kisiasa ambao umestawi kwenye vichwa vya watanzania wengi.
Nchi yetu ina matatizo mengi mno (yanaweza fika bilioni) sidhani kama kuna sekta ambayo tumefanikiwa tunaweza kujivunia (elimu,afya,kilimo,miundombinu,ufugaji,uvuvi,uchumi,utalii,michezo,habari,teknolojia) sidhani kama tukitatua tatizo moja watu wataunga mkono,bado tutaendelea kulalamika kwa nini hakuanza na C tumeanza na A.Kuna matatizo ambayo yapo ndani ya uwezo wetu na tunaweza kuyamaliza sisi wenyewe ndani ya muda mfupi.
Haya matatizo ni ngumu sana kuisha ndani ya miaka 10/20 na hakuna mwanasiasa ambaye anaweza kuyamaliza ndani ya miaka 20 kama viongozi wetu na wananchi kwa ujumla hatutabadilika.Kibaya zaidi mambo yanabadilika kwa kasi sana tukiendelea kuzubaa tunazidi kuachwa nyuma licha ya rasilimali tulizonazo,kwa sasa hatuna kipaumbele .Tatizo kubwa lilitufikisha hapa lilikuwa ni rushwa na ufisadi tukijitahidi kulipunguza/kulimaliza hili una haja ya kuhamia kwenye vipaumbele kwenye sekta ya afya,elimu,kilimo,ufugaji,utalii na teknolojia