Brown73
JF-Expert Member
- Aug 24, 2010
- 1,100
- 683
Kutokuridhika kwa binadamu ni jambo la kiasili.
Kunung'unika nako ni ada ya mja.
Bila ya kupoteza sana muda ngoja nizame moja kwa moja kwenye hoja.
Baada ya ununuzi wa hizi ndege za shirika letu la ndege, kumekuwepo na hoja kadha wa kadha zinazohoji eti kwa nini mheshimiwa MTUKUFU rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dokta John Pombe Joseph Magufuli pamoja na serikali yake wananunua ndege ilhali sehemu nyingi za Tanzania hazina viwanja vya ndege, eti hatuna sukari ya kutosha, hatuna sijui mashine gani mahospitalini, na kadhalika na kadhalika.
Sasa nami hebu ngoja niulize [maswali] yangu:
Hivi, kwani wakati ule tulipokuwa na zile ndege zetu za ATC, tulikuwa na viwanja vingapi vya ndege huko mikoani na wilayani?
Je, wakati ule hospitali zetu za serikali zilikuwa na kila kitu? Bugando ilikuwa na mashine zote zilizokuwa zinahitajika? Muhimbili nayo ilikuwa imejitosheleza kwa kila kitu?
Sukari, unga, sabuni, na mahitaji mengine nayo tulikuwa tumejitosheleza nayo vizuri tu?
Hizo Fokker Friendship [nadhani walikuwa nazo mbili au zaidi] za ATC ziliweza kutua hata huku kwetu Ikungulyabashashi, Ng'wamapalala, Lamadi, Madale, na Nyangokolwa?
Nchi zingine zilizo na mashirika yao ya ndege zenyewe zimetatua matatizo yake yote kabla ya kuamua kuwa na ndege zake zenyewe?
Huko Kenya kwa mfano, wao kila hospitali yao ina kila kifaa kilicho cha muhimu?
Sasa labda mimi kwa vile ni mbeba maboksi tu nisiye na elimu yoyote ile kubwa [niliishia kidato cha nne ambapo nilipata daraja la nne na pointi 30] ndo maana labda kwa kiasi fulani sizielewi hizo hoja za baadhi ya hao vipanga wanaozitoa.
Lakini nadhani mtu unaweza ukawa unatafuna jojo huku ukitembea na kuongea kwenye simu yako ukiwa unaelekea kwa Joji kwenda kula kiti moto au chipsi vumbi.
Mimi binafsi nafikiria hivi,
Badhi ya wizara hazina kipato maalum cha kujiendesha kwa hiyo asilimia kubwa ya budget yao anategemea kodi zetu, mfano elimu, afya, ulinzi na jeshi lapolisi na kadhalikia. Ili hela za serikali au hazina ziongezeke inabidi serikali itafute njia nyinyi za kuongeza kipato. Utalii ni mmoja yapo ya kipato hapa nchini, kwa hiyo ili ili kuboresha Utalii inabidi kuboresha na usafiri. Na pia wafanya biashara wanahitaji usafiri bora ili biashara zao ziende kiurahisi. Kwa hiyo usafiri wa anga ni muhimu sana kwa wafanya biashara.
Kwa hiyo kufufuliwa hili shirika ni muhimu sana. Si lazima tuwe na ndege zinazo kwenda international. Mbona hapa Sweden hawana ndege za nje na hakuna anayepiga kelele na kukashifu kwamba hawana hizo ndege kubwa za kwenda nje.