Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 370,954
- 858,881
Jioni ya tarehe 25 Mei 2003, uwanja wa ndege wa Quatro de Fevereiro huko Luanda, nchini Angola, ulikuwa kimya kama kawaida.
Lakini kimya hicho kilivunjika ghafla pale ndege kubwa aina ya Boeing 727-223, yenye usajili N844AA, ilipoanza kujisogeza polepole kwenye njia ya kuruka bila kibali chochote kutoka kwa waongoza ndege.
Ilikuwa ni ndege ambayo miaka 25 iliwahi kubeba abiria kwa shirika la American Airlines, lakini wakati huo imebadilishwa kuwa ya kubeba mizigo kwa kuweka ndani yake matangi makubwa ya kubeba mafuta ya dizeli.
Kwa zaidi ya mwaka mzima ilikuwa imetulia hapo Luanda, imefungiwa kwa sababu ya madeni na migogoro ya ukodishaji.
Watu waliokuwa kwenye mnara walishangaa tu kuiona ndege hiyo ikitembea kwenye barabara za mchepuko (taxiway) kwa namna isiyo ya kawaida, bila taa, bila sauti ya mawasiliano, na transponder yake ikiwa imezimwa kabisa, na baadae ikaanza kukimbia njia ya kuruka na kupaa angani.
Ndege hiyo haikuonekana kabisa na rada za kibiashara. Ikaruka moja kwa moja kuelekea kusini magharibi, ikazama juu ya giza la Bahari ya Atlantiki na tangu siku hiyo haikuwahi kuonekana tena.
Hakuna mabaki, hakuna alama, hakuna hata mtu aliyedai kuiona.
Ndani yake kuliaminika kuwa na wanaume wawili tu.
Mmoja alikuwa Ben Charles Padilla, Mmarekani aliyekuwa fundi wa ndege na rubani binafsi.
Mwingine alikuwa John Mikel Mutantu, fundi aliyetoka Jamhuri ya Kongo ambaye aliajiriwa tu.
Tatizo ni kwamba Boeing 727 haiwezi kurushwa na mtu mmoja au wawili wasio na mafunzo kamili.
Inahitaji rubani, rubani msaidizi na mhandisi wa ndege wenye sifa.
Lakini wale wawili waliondoka nayo jioni ile, na siri yao ikazama pamoja na ndege kubwa zaidi kuwahi kutoweka kabisa katika historia ya anga.
Hadi leo, baada ya miaka zaidi ya ishirini, hakuna aliyejua ndege hiyo iliishia wapi, wala ilitokea nini kwa wanaume wawili waliokwenda nayo gizani.
Lakini kimya hicho kilivunjika ghafla pale ndege kubwa aina ya Boeing 727-223, yenye usajili N844AA, ilipoanza kujisogeza polepole kwenye njia ya kuruka bila kibali chochote kutoka kwa waongoza ndege.
Ilikuwa ni ndege ambayo miaka 25 iliwahi kubeba abiria kwa shirika la American Airlines, lakini wakati huo imebadilishwa kuwa ya kubeba mizigo kwa kuweka ndani yake matangi makubwa ya kubeba mafuta ya dizeli.
Kwa zaidi ya mwaka mzima ilikuwa imetulia hapo Luanda, imefungiwa kwa sababu ya madeni na migogoro ya ukodishaji.
Watu waliokuwa kwenye mnara walishangaa tu kuiona ndege hiyo ikitembea kwenye barabara za mchepuko (taxiway) kwa namna isiyo ya kawaida, bila taa, bila sauti ya mawasiliano, na transponder yake ikiwa imezimwa kabisa, na baadae ikaanza kukimbia njia ya kuruka na kupaa angani.
Ndege hiyo haikuonekana kabisa na rada za kibiashara. Ikaruka moja kwa moja kuelekea kusini magharibi, ikazama juu ya giza la Bahari ya Atlantiki na tangu siku hiyo haikuwahi kuonekana tena.
Hakuna mabaki, hakuna alama, hakuna hata mtu aliyedai kuiona.
Ndani yake kuliaminika kuwa na wanaume wawili tu.
Mmoja alikuwa Ben Charles Padilla, Mmarekani aliyekuwa fundi wa ndege na rubani binafsi.
Mwingine alikuwa John Mikel Mutantu, fundi aliyetoka Jamhuri ya Kongo ambaye aliajiriwa tu.
Tatizo ni kwamba Boeing 727 haiwezi kurushwa na mtu mmoja au wawili wasio na mafunzo kamili.
Inahitaji rubani, rubani msaidizi na mhandisi wa ndege wenye sifa.
Lakini wale wawili waliondoka nayo jioni ile, na siri yao ikazama pamoja na ndege kubwa zaidi kuwahi kutoweka kabisa katika historia ya anga.
Hadi leo, baada ya miaka zaidi ya ishirini, hakuna aliyejua ndege hiyo iliishia wapi, wala ilitokea nini kwa wanaume wawili waliokwenda nayo gizani.