Ananunua ndege wakati hiki na kile hatuna...

Ananunua ndege wakati hiki na kile hatuna...

Mkuu kuna kipanga mmoja yuko UDOM anaingia mwaka wa 3 alipata daraja la 4 na pointi 30. Kwahiyo na wewe ni mmoja wa vipanga hapa nchini.

Hapana kaka.

Vipanga ni hao waliosomaga 'spesho skulz'.

Mi mbeba maboksi tu.
 
Nyani ngabu sijajua kabisa nia ya maswali yako!maana kila anayekujibu bado unapingana naye na kuuliza maswali zaidi!!utapata wapi jibu litakaloridhisha nafsi yako!?
Naomba nikuulize!Nini kipaumbele ya serikali yetu!?
Watanzania wangapi wenye uhitaji wa maisha bora kuliko hao wenye uwezo wa kupanda ndege!?
Nakubaliana kwa mkuu kununua ndege,but ni muda mwafaka kwa kutekeleza hivyo ilhali maisha yanazidi kudidimia?
Any way!!Kila kitu ni njema machoni pa bwana wetu wa mbinguni!na tutiini mamlaka.
 
Kwa hiyo hatuwezi kununua ndege zetu wenyewe kwa sababu hospitali hazina vifaa vya kutosha?
Halafu unakuta anayelalamika hivyo anaenda kununua vocha ajiunge bundle kuchat na marafiki wakati nyumbani hajaacha hela ya chakula,au yuko bar anaagiza bia kwa vimada lakini ada ya shule ya mtoto hajalipa lakini yeye wala hajikosoi ila akiona ndege imenunuliwa ndio anajifannya hodari wa kusort priorities.
 
Tunategemea kufanya biashara ya usafiri kwa ndege hizo, nchi ina wananchi zaidi ya 45m tumejiandaaje kuwatumia raia wetu waliotapakaa across the country kuhakikisha hizo ndege wananchi hawa wanazitumia as a results tuna earn alot of money.
Ili iwe hivyo lazima ndege iwahudumie wote kutoka nyakanazi mpaka Tunduru, Olmotonyi mpaka mbambabay
Huyu jamaa si dhani kama yupo serous na nchi yake. Leo kuna baadhi ya vijiji bado wamekuwa watu wa mlo moja, huduma ya afya wanaifaya si chini kilomita 20, idadi ya watu wasio na ajira inazidi kuongezeka, sasa sijui anawaza nini?
Bora basi hata imgenunuliwa moja kwanza.
 
Nyani Ngabu mbona unalitaja taja jina langu!

Lekaga gete nkoyi!

Kuna baadhi ya watu hawafahamu kuwa wakati ndege za ATC zinapishana kwenye anga la Ulaya, sisi hapa Ng'wamapalala hatukuwa hata na uwanja wa mpira achilia mbali uwanja wa ndege.

Shuleni tulikuwa tunakaa kwenye mawe tuliyoenda kutafuta na kuyapata mlimani achilia mbali madawati.

Angalau huduma ya afya tulikuwa tunapata kwenye dispensary ya kanisa katoliki ambayo ilikuwa inahudumia zaidi ya kata nzima ya Ng'wamapalala.

Unga tulikuwa tunanunua kwenye duka la kijiji kwa kupanga foleni.

Basi la kutoka Bariadi kwenda Shinyanga lilikuwa linapita mara moja baada ya siku mbili au wiki.

Usafiri wa uhakika wa kwenda Bariadi ilikuwa ni baiskeli.

Kupanga ni kuchagua!
 
Unavyo vijisenti vya kukufanya usinzie mapema mayb. Ndege zinatufaa nini wakati huu hospitali hazina panadol?
 
Umeshikiwa ubongo na akili? Huwezi kufikiria mwenyewe ukiwa independent? Jaji hakosei? Anajua kila kitu??

Hebu changanya na zako kidogo tu za lasaba B
Ndio mkuu, nimeshikiwa na mbaya zaidi aliyevishika ni "Juma Pombe Maharagwe".
Sijaongelea ukamilifu wa Jaji Warioba, ila nimependa usome alichoongelea kuhusu Taifa kukosa dira katika uongozi.
Kama ambavyo anakosea, na ndivyo hivyo ambavyo na wewe unatakiwa kuchanganya na zako katika kusoma ilani ya Magufuli.
Sasa kama Taifa halina Sera ya kuliongoza, na inategemea ilani ya Chama, tutafika?
Maana kama ndio hivyo kila chama au uongozi utakaokuwa unaingia madaraka ni utakuwa unaingia na mdundo wake, yule kama aliacha hajamaliza ujenzi wa barabara, basi atakayefuata hawezi kumalizia, vile tu halipo kwenye ilani yake. Na ndio haya tunayoyaona.
 
Na kuweka kumbukumbu sahihi sasa hivi shirika la simu linamilikiwa na serikali kwa asilimia 100. Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni, kama kuna mahali waliotangulia walijakwaa na waliofuata wakabaini makosa na sehemu walizojikwaa na wakaanza kurekebisha kasoro zilizotufanya turudi nyuma au tusipige hatua ya kimaendeleo hatuna budi kuwapongeza na kuwaunga mkono ili tusonge mbele. Changamoto hazikosekani mahali popote, kama katika ngazi ya familia tu tunakumbwa na changamoto na kushindwa kuzitafutia suluhisho kwa wakati, iwe ajabu katika ngazi ya taifa
 
Nyani ngabu sijajua kabisa nia ya maswali yako!

Nisome vizuri na kwa utulivu na pengine utaweza kung'amua walau kidogo.

maana kila anayekujibu bado unapingana naye na kuuliza maswali zaidi!!

Huu ni uongo. Si kila anayenijibu napingana naye. Kama si uongo, basi nionyeshe kila nilipopingana na kila aliyenijibu.

utapata wapi jibu litakaloridhisha nafsi yako!?

Binadamu haridhiki na ukweli huu ni kwa wengi, ikiwemo hao wanaoponda ununuzi wa ndege.

Naomba nikuulize!

Kuniuliza si hisani yangu kwako. Wewe uliza tu. Huna haja ya kuniuliza juu ya kuniuliza.

Nini kipaumbele ya serikali yetu!?

Serikali haiwezi kuwa na kipaumbele. Serikali ina vipaumbele. Unaelewa tofauti yake?

Watanzania wangapi wenye uhitaji wa maisha bora kuliko hao wenye uwezo wa kupanda ndege!?

Kwani kusafiri kwa ndege nako si maisha bora?

Kufanya kazi kwenye shirika la ndege nako si maisha bora?

Unajua ni watu wangapi wanaishi au wataishi maisha yenye nafuu kutokana na hizo ajira za shirika la ndege?

Nakubaliana kwa mkuu kununua ndege,but ni muda mwafaka kwa kutekeleza hivyo ilhali maisha yanazidi kudidimia?

Maisha yanazidi kudidimia kivipi? Kuna watu wanakufa njaa Tanzania hii?

Any way!!Kila kitu ni njema machoni pa bwana wetu wa mbinguni!na tutiini mamlaka.

Huko sasa mi sipo.
 
Ndio mkuu, nimeshikiwa na mbaya zaidi aliyevishika ni "Juma Pombe Maharagwe".
Sijaongelea ukamilifu wa Jaji Warioba, ila nimependa usome alichoongelea kuhusu Taifa kukosa dira katika uongozi.
Kama ambavyo anakosea, na ndivyo hivyo ambavyo na wewe unatakiwa kuchanganya na zako katika kusoma ilani ya Magufuli.
Sasa kama Taifa halina Sera ya kuliongoza, na inategemea ilani ya Chama, tutafika?
Maana kama ndio hivyo kila chama au uongozi utakaokuwa unaingia madaraka ni utakuwa unaingia na mdundo wake, yule kama aliacha hajamaliza ujenzi wa barabara, basi atakayefuata hawezi kumalizia, vile tu halipo kwenye ilani yake. Na ndio haya tunayoyaona.
Hapo sasa umegusa point kubwa ambayo nami siku zote nataka nione kama nchi tunaifuata... DIRA YA NCHI .

Nchi inatakiwa iwe na dira ambayo yeyote atakayeunda serikali atafuata dira hiyo...... Suala hili litasaidia sana taifa kusonga mbele no matter chama gani kitakamata dola.
 
Nampongeza Rais JPM kwamaana anafanya sasa kupanda ndege isiwe ndoto tena kwa watz.
 
SAMAHANI MH RAIS
SAMAHANI MAMLAKA HUSIKA
SAMAHANI WASHAURI WA RAIS

Mh Rais leo umesema kuwa unazo hela za kununua ndege zingine mbili (NAOMBA NILIE KIDOGO hiiii hiiii hiii ng'aaa ng'aaa ng'aaa)

ni muda sasa umepita msd wanasema hawana hela za kuagiza Madawa (nalia tena hiiii hiii hiii hiii hiiii)

mwanangu wakambo hajachomwa sindano ya chanjo ile hospitali yetu ya kata haina (nalia tena hiii hiii hiii hiii)

kule kigoma kumetokea tetemeko
(KILA SIKU WAHANGA WANALALAMA KUWA HAWAJALIWI) (nalia tena hiii hiii hiii hiii)

KWANI MH HIZO NDEGE MPYA ZITAKUWA ZINABEBA MAITI AMA WAGONJWA WALIOKOSA MADAWA MAHOSPITALINI?

ama je kipaombele cha serikali hii ni ndege tu??

WAHESHIMIWA INAWEZEKANA NIMEWAZA VIBAYA HIVYO NISAMEHEWE BILA KUADHIBIWA
Tumpe muda.
 
Nyani Ngabu mbona unalitaja taja jina langu!

Lekaga gete nkoyi!

Kuna baadhi ya watu hawafahamu kuwa wakati ndege za ATC zinapishana kwenye anga la Ulaya, sisi hapa Ng'wamapalala hatukuwa hata na uwanja wa mpira achilia mbali uwanja wa ndege.

Shuleni tulikuwa tunakaa kwenye mawe tuliyoenda kutafuta na kuyapata mlimani achilia mbali madawati.

Angalau huduma ya afya tulikuwa tunapata kwenye dispensary ya kanisa katoliki ambayo ilikuwa inahudumia zaidi ya kata nzima ya Ng'wamapalala.

Unga tulikuwa tunanunua kwenye duka la kijiji kwa kupanga foleni.

Basi la kutoka Bariadi kwenda Shinyanga lilikuwa linapita mara moja baada ya siku mbili au wiki.

Usafiri wa uhakika wa kwenda Bariadi ilikuwa ni baiskeli.

Kupanga ni kuchagua!

Chuuu...hene nkoi ule ujimelile hei?

Gabhita makanza malipu natenagubhona ung'wenumu.

Mhola mhola ahene?
 
Jibu ni kwamba matatizo kwa mwanadamu hayaishi.
Shida aina mwisho mpaka siku ya kufa.
Mwalimu wangu wa Form5 Economics siku ya kwanza anaanza kunifundisha economics alisema mahitaji hapa duniani yapo mengi sana na malighafi ni chache kutatua hayo matatizo kwa hiyo inabidi kuyapanga hayo matatizo ili utumie hiyo malighafi uliyonayo kuyatatua.....hata siku moja hakuna Raisi atakaye kuja kumaliza haya matatizo ya mwanadamu....na tatizo kubwa tulilonalo sasa hivi ni kila mtu kujua kila kitu na kuhisi gvt ipo kutatua kila matatizo yetu kazi sana
 
Back
Top Bottom