Ananunua ndege wakati hiki na kile hatuna...

Ananunua ndege wakati hiki na kile hatuna...

Ubaya unaongezeka pale vipaumbele vyenyewe anaamua mtu mmoja!! Kwa ubora gani aliokuwa nao? (ni rahisi kuhoji hivyo)
Mkuu, ebu fikiria vizuri. OK, umeongelea kwa kipindi kile, je unakumbuka idadi ya watu na uwiano wa mahitaji yao ya msingi.?
Leo Tanzania ina watu si chini ya milioni 45, je unahisi kuna uwiano wa mahitaji yao ya msingi, mfano kupata huduma bora za Afya, Malazi bora na Elimu bora.
Watu wanapanga foleni kila mahali siku hizi, sio hospital, kwenye mabenki, barabrani, baadhi ya maofisi ya umma.
Tuna matatizo mengi, sana na makubwa kuliko hata hilo la ndege.
Kwa mwando huu wa kuchagua vipaumbele vya maendeleo pasipo kufanya tafiti za kina na kutosha, tutabaki tunaruka sarakasi wakati bado tupo kwenye vazi la kanzu na msuli, kufaidisha wengine.
 
Huyu jamaa si dhani kama yupo serous na nchi yake. Leo kuna baadhi ya vijiji bado wamekuwa watu wa mlo moja, huduma ya afya wanaifaya si chini kilomita 20, idadi ya watu wasio na ajira inazidi kuongezeka, sasa sijui anawaza nini?
Bora basi hata imgenunuliwa moja kwanza.

Kwani wakati wa ATC hakukuwepo na vijiji ambavyo watu walikuwa wanashindia mlo mmoja?

Hakukuwepo na hivyo vijiji ambavyo watu kupata huduma ya afya ilibidi waende umbali si chini ya hizo kilomita 20?

Wakati wa ATC hakukuwepo kabisa na changamoto zingine?
 
SAMAHANI MH RAIS
SAMAHANI MAMLAKA HUSIKA
SAMAHANI WASHAURI WA RAIS

Mh Rais leo umesema kuwa unazo hela za kununua ndege zingine mbili (NAOMBA NILIE KIDOGO hiiii hiiii hiii ng'aaa ng'aaa ng'aaa)

ni muda sasa umepita msd wanasema hawana hela za kuagiza Madawa (nalia tena hiiii hiii hiii hiii hiiii)

mwanangu wakambo hajachomwa sindano ya chanjo ile hospitali yetu ya kata haina (nalia tena hiii hiii hiii hiii)

kule kigoma kumetokea tetemeko
(KILA SIKU WAHANGA WANALALAMA KUWA HAWAJALIWI) (nalia tena hiii hiii hiii hiii)

KWANI MH HIZO NDEGE MPYA ZITAKUWA ZINABEBA MAITI AMA WAGONJWA WALIOKOSA MADAWA MAHOSPITALINI?

ama je kipaombele cha serikali hii ni ndege tu??

WAHESHIMIWA INAWEZEKANA NIMEWAZA VIBAYA HIVYO NISAMEHEWE BILA KUADHIBIWA
Nakuunga miguu,mikono na vyote kwa kweli nimesikitika sana.
 
SAMAHANI MH RAIS
SAMAHANI MAMLAKA HUSIKA
SAMAHANI WASHAURI WA RAIS

Mh Rais leo umesema kuwa unazo hela za kununua ndege zingine mbili (NAOMBA NILIE KIDOGO hiiii hiiii hiii ng'aaa ng'aaa ng'aaa)

ni muda sasa umepita msd wanasema hawana hela za kuagiza Madawa (nalia tena hiiii hiii hiii hiii hiiii)

mwanangu wakambo hajachomwa sindano ya chanjo ile hospitali yetu ya kata haina (nalia tena hiii hiii hiii hiii)

kule kigoma kumetokea tetemeko
(KILA SIKU WAHANGA WANALALAMA KUWA HAWAJALIWI) (nalia tena hiii hiii hiii hiii)

KWANI MH HIZO NDEGE MPYA ZITAKUWA ZINABEBA MAITI AMA WAGONJWA WALIOKOSA MADAWA MAHOSPITALINI?

ama je kipaombele cha serikali hii ni ndege tu??

WAHESHIMIWA INAWEZEKANA NIMEWAZA VIBAYA HIVYO NISAMEHEWE BILA KUADHIBIWA
Kazungumza hbr ya ndege kwa kua alikua ktk shughuli hyo.ikifika wakati wa kuzungumzia afya atatoa maneno ya kile kilichopo ktk idara hyo ya afya juu ya hzo sindano za kinga.wahanga Bukoba pia mbona kuna watu wanashughulika na kinachoendelea huko na maelekezo yake binafsi alishatoa
 
Kinachohuzunisha hapa wanaobeza ununuzi wa hizo ndege hapa jukwaani,ndio wale waliokuwa wakidhaniwa ni ma 'great thinkers'. Je kapuku?

Na wengine ndo hao hao walokuwa mstari wa mbele kuiponda serikali kwa kushindwa kuliendeleza shirika la ndege la taifa!

Mara ooh hata Kenya wametuzidi....mara ooh ona Rwanda walipo sasa...licha ya vita lakini wana ndege zao tena kali sana...mara ooh Ethiopia licha ya baa la njaa ya mwaka sijui '85 ule lakini shirika lao la ndege ndo inasemekana ni shirika bora la ndege barani Afrika.

Halafu leo hii serikali inafanya kweli katika jitihada za kulirudishia uhai shirika la ndege, watu wanaponda!
 
Kwani wakati wa ATC hakukuwepo na vijiji ambavyo watu walikuwa wanashindia mlo mmoja?

Hakukuwepo na hivyo vijiji ambavyo watu kupata huduma ya afya ilibidi waende umbali si chini ya hizo kilomita 20?

Wakati wa ATC hakukuwepo kabisa na changamoto zingine?
Kwahiyo kwa upande wako unaona ni bora, tatizo hilo liendelee kuwepo badala ya kulitatua kwanza.?
Naomba nikuulize Swali kwako neno "maendeleo" ni nini?
 
SAMAHANI MH RAIS
SAMAHANI MAMLAKA HUSIKA
SAMAHANI WASHAURI WA RAIS

Mh Rais leo umesema kuwa unazo hela za kununua ndege zingine mbili (NAOMBA NILIE KIDOGO hiiii hiiii hiii ng'aaa ng'aaa ng'aaa)

ni muda sasa umepita msd wanasema hawana hela za kuagiza Madawa (nalia tena hiiii hiii hiii hiii hiiii)

mwanangu wakambo hajachomwa sindano ya chanjo ile hospitali yetu ya kata haina (nalia tena hiii hiii hiii hiii)

kule kigoma kumetokea tetemeko
(KILA SIKU WAHANGA WANALALAMA KUWA HAWAJALIWI) (nalia tena hiii hiii hiii hiii)

KWANI MH HIZO NDEGE MPYA ZITAKUWA ZINABEBA MAITI AMA WAGONJWA WALIOKOSA MADAWA MAHOSPITALINI?

ama je kipaombele cha serikali hii ni ndege tu??

WAHESHIMIWA INAWEZEKANA NIMEWAZA VIBAYA HIVYO NISAMEHEWE BILA KUADHIBIWA
Kuna ukweli fulani kwenye hilo andiko lako ila na wewe uache uongo kwa kusema Kigoma kuna wahanga wa tetemeko wanaolalamika hawajaliwi!
 
Kwani usafiri wa ndege na afya,elimu bora,maji safi na salama kipi cha muhimu?
Au hiyo ilikuwa kipaumbele kwa wakati.

Vyote vina umuhimu wake katika muktadha wake.

Ni sawa na machungwa, matufaha, mahindi, nyama, na maziwa.

Vyote ni vyakula na vyote vina umuhimu wake katika uhai wa mwanadamu.

Ndo maana ni muhimu kula vyote kwa viwango vyenye uwiano na wastani mzuri.
 
Mkuu utalia sana zama hizi, kila kitu na wakati wake, muda ukifika msd itajaa madawa, hata hivyo tumieni miti shamba mbona mapori kibao mkuu
 
Bado tuna safari ndefu mimi nadhani hilo la ndege limekaa vema sasa tuangalie lingine na pia kupongeza maana kwa vipaumbele kila mtu atataka kipaumbele chake na pia watanzania sijui tumekopi wapi khulka ya kuponda tu bila ya kuonyesha njia japo kwa michango ya mawazo.
 
SAMAHANI MH RAIS
SAMAHANI MAMLAKA HUSIKA
SAMAHANI WASHAURI WA RAIS

Mh Rais leo umesema kuwa unazo hela za kununua ndege zingine mbili (NAOMBA NILIE KIDOGO hiiii hiiii hiii ng'aaa ng'aaa ng'aaa)

ni muda sasa umepita msd wanasema hawana hela za kuagiza Madawa (nalia tena hiiii hiii hiii hiii hiiii)

mwanangu wakambo hajachomwa sindano ya chanjo ile hospitali yetu ya kata haina (nalia tena hiii hiii hiii hiii)

kule kigoma kumetokea tetemeko
(KILA SIKU WAHANGA WANALALAMA KUWA HAWAJALIWI) (nalia tena hiii hiii hiii hiii)

KWANI MH HIZO NDEGE MPYA ZITAKUWA ZINABEBA MAITI AMA WAGONJWA WALIOKOSA MADAWA MAHOSPITALINI?

ama je kipaombele cha serikali hii ni ndege tu??

WAHESHIMIWA INAWEZEKANA NIMEWAZA VIBAYA HIVYO NISAMEHEWE BILA KUADHIBIWA
False start in Africa by Walter Rodney, false priorities in Tanzania by me.
 
Kutokuridhika kwa binadamu ni jambo la kiasili.

Kunung'unika nako ni ada ya mja.

Bila ya kupoteza sana muda ngoja nizame moja kwa moja kwenye hoja.

Baada ya ununuzi wa hizi ndege za shirika letu la ndege, kumekuwepo na hoja kadha wa kadha zinazohoji eti kwa nini mheshimiwa MTUKUFU rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dokta John Pombe Joseph Magufuli pamoja na serikali yake wananunua ndege ilhali sehemu nyingi za Tanzania hazina viwanja vya ndege, eti hatuna sukari ya kutosha, hatuna sijui mashine gani mahospitalini, na kadhalika na kadhalika.

Sasa nami hebu ngoja niulize [maswali] yangu:

Hivi, kwani wakati ule tulipokuwa na zile ndege zetu za ATC, tulikuwa na viwanja vingapi vya ndege huko mikoani na wilayani?

Je, wakati ule hospitali zetu za serikali zilikuwa na kila kitu? Bugando ilikuwa na mashine zote zilizokuwa zinahitajika? Muhimbili nayo ilikuwa imejitosheleza kwa kila kitu?

Sukari, unga, sabuni, na mahitaji mengine nayo tulikuwa tumejitosheleza nayo vizuri tu?

Hizo Fokker Friendship [nadhani walikuwa nazo mbili au zaidi] za ATC ziliweza kutua hata huku kwetu Ikungulyabashashi, Ng'wamapalala, Lamadi, Madale, na Nyangokolwa?

Nchi zingine zilizo na mashirika yao ya ndege zenyewe zimetatua matatizo yake yote kabla ya kuamua kuwa na ndege zake zenyewe?

Huko Kenya kwa mfano, wao kila hospitali yao ina kila kifaa kilicho cha muhimu?

Sasa labda mimi kwa vile ni mbeba maboksi tu nisiye na elimu yoyote ile kubwa [niliishia kidato cha nne ambapo nilipata daraja la nne na pointi 30] ndo maana labda kwa kiasi fulani sizielewi hizo hoja za baadhi ya hao vipanga wanaozitoa.

Lakini nadhani mtu unaweza ukawa unatafuna jojo huku ukitembea na kuongea kwenye simu yako ukiwa unaelekea kwa Joji kwenda kula kiti moto au chipsi vumbi.

Nyani wakifanya makosa wenzako siyo warrant ya wewe kufanya makosa
 
Back
Top Bottom