Amini usiamini Marando ndo anabomoa CHADEMA

YEYE MBUSHI, kwa uliyoyaandika hapo juu ni kwamba humjui Mabere Nyaucho Marando, pole sana kijana. Huyo ndiye mwanamageuzi kunukuliwa akitoa kauli ya Mwalimu kufilisika kisiasa wakati upepo wa mageuzi ulipotia mguu nchini kwa mara ya kwanza. Kauli hiyo ya kushitua, iliyotolewa Mwalimu akiwa bado hajamkabidhi Raisi Mwinyi uenyekiti wa CCM, ilisababisha Mabere aogopwe na kutengwa na ndugu, marafiki na wanataaluma wenzake. Mabere Nyaucho Marando ni mzalendo wa kwanza kuukataa uteuzi wa Raisi Mwinyi kwenye tume ya eti kuwauliza Watanzania kama wanaridhia demokrasia ya vyama vingi akidai ni kufuja hela kwa jambo lililo wazi. YEYE MBUSHI, kubali kuwa ni kweli humjui Mabere Nyaucho Marando; hujui CCM ilivyohangaika na inavyozidi kuhangaika usiku na mchana kumrubuni lakini mara zote inaangukia pua. Kwa Chadema huyo jamaa ni mtaji tosha...acha kukurupuka.
 
Mie sina imani na dr slaa, huyu ndie tatizo chadema.
 

Aache kazi ya kuwabomoa watu wanaojifanya miungu watu, wanatafuna rasilimali za nchi bila kufuata taratibu na kanuni za nchi zinavyoelekeza. Aanze tu kuibomoa chadema???!!!
 
Nimesema toka mwanzo kuwa mtanipinga kwa kuwa hamjui historia ilofichwa

Yaani mkuu wewe ni mzushi wa kawaida kabisa ambaye hata ungeenda kijiwe cha kahawa ungeishiwa kuzomewa tu.Huwezi kuongea kwa hisia halafu utusgawishi tukuamini,tutakuwa wajinga kuliko wewe
 
Nadhani hawa MaCCM wamebuni mbinu mpya ya kupandikiza chuki na woga, watu waogopane na kuchukiana!!
Makamanda kuweni makini na hawa makanjanja wa Lumumba!!
 
Naunga mkono hoja. Alishasema kwa kinywa chake mwenyewe kuwa yeye ni shushushu ie usalama wa taifa na ile kazi huwa haiachwi, ni ya maisha, hawafukuzwi.

Yaani wewe bado tu hujui kuwa usalama wa taifa wengi ni CHADEMA? Kwa kukusaidia tu hata ndani ya CCM wengi wao ni CHADEMA.
 
Asante kwa taarifa, unajua kuwa hata Mrema alikuwa ni mfanyakazi wa TISS? au unajua kuwa Mbowe, Dr Slaa wote wakuwa wana CCM?....life keep changing bwana

 
Ukifikilia sana, vuguvugu la vyama vingi lilikuwa na baraka za Nyerere toka mwanzo...NCCR - nadhani ilikuwa ni kifupisho na mikutano ya kudai mabadiliko ambayo ilianza miaka ya 1991, ni kweli mabadiliko yalitokea, hata kama akina marando walikuwa Usalama wa Taifa, kuwa usalama wa taifa sio kuwa ni mwana CCM, hiyo ndio dhana potofu, walioko ndani ya TISS anaweza akawa na mapenzi na chama chochote ila haruhusiwi kuwa mwanachama kama mtumishi wa umma....kama watu waliowahi fanya kazi TISS utawaogopa, basi hata hiyo kazi yake ya sheria sidhani kama angepata wateja, maana angeweza kuwa uipande wa serikali

 
Camp05 usiogope kivuli watu wakichoka wanabadilika, hata ofisini unaweza kugeukwa!!
Marando alisha choka na mfumo
amebadilika!!
 
Last edited by a moderator:
kwani vyama vya upinzani ni maadui wa Taifa? kwani ukiwa usalama wa taifa ni kwa ajili ya kuilinda CCM?.Unadhani Usalama wa taifa wote wanafurahia kuona jinsi CCM inavyoinajisi nchi kwa ufisadi na maovu mengine.Arcado Ntagazwa alikua Mkurugenzi msaidizi wa TISS wakati wa Mwalimu na sasa yuko chadema na yeye anaihujumu CHADEMA? Nyerere alisema CCM sio baba wala mama yake angeweza kutoka wakati wowote ule kutokana na maovu yaliokua yakifanywa na CCM.Naamini Marando anaweza kuwa ni mmoja wa watanzania wanaopenda mabadiliko na ndio maana alishiriki kuanzisha kwa vuguvugu la vyama vingi na NCCR Mageuzi yake.ni maoni yangu tu lakini.
 
Nimesema toka mwanzo kuwa mtanipinga kwa kuwa hamjui historia ilofichwa

historia ipi? kufanya kazi na nyerere ikulu ndo historia yenyewe, kwa hiyo unataka tukuunge mkono kwa hicho? wacha hizo, toa hoja zenye mashiko.
 
Baada ya kugonga mwamba kuisambaratisha CHADEMA kwa kumutumia ZITTO sasa mnataka kumtumia MARANDO endeleni lakini nawaambia ukombozi huu unacheleweshwa tu lakini uko palepale muda ukifika hakuna wa kuzuia nguvu ya umma

marando atimuliwe kwenye chama haraka. lema yuko wapi ampige vitofali. msaliti huyu.
 
Camp05 usiogope kivuli watu wakichoka wanabadilika, hata ofisini unaweza kugeukwa!!
Marando alisha choka na mfumo
amebadilika!!

mkuu. mchagga na mkurya wapi na wapi. marando anatusaliti wakaskazini
 
Last edited by a moderator:
Hoja hii yaweza kuwa rahisi kama mnavyodhania,lakini si ya kupuuzia.Lets think green!
 
marando kwanza ni msomi atatusumbua sana kwenye chama. tumfukuze huyu msaliti
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…