Ennie
JF-Expert Member
- Jan 15, 2011
- 7,137
- 4,139
Dah unamtetea kwa udi na uvumba aisee angekuwepo humu nadhani hata vocha ungepata aisee
Haha haaaaaaaaa!
Sitaki hata like yake,ila ukweli lazima usemwe
Dah unamtetea kwa udi na uvumba aisee angekuwepo humu nadhani hata vocha ungepata aisee
hata ningekuwa mimi nisingekurudishia
Wana jamii wenzangu mimi ni mwanaume wa miaka 29 nimekuwa na uhusiano na msichana kwa miaka 3 mwishoni mwa mwaka niligundua kuwa ana uhusiano na mtu mwingine na nilipombana kwa maswali alikubali na kusema wamekuwa pamoja kwa miezi 8 ila wameachana wiki mbili zilizopita nimeumia sana maaana nilimwamini mno, nimeamua kuachana nae ila nilimpa laptop yangu ya gharama sana ya laki 9 kwa makubaliano nitamnunulia ya kwake ila baaada ya usaliti aliofanya nimeona anipe mali yangu .Cha ajabu anang'ang'ania kwa kusema anaitumia na kwa sasa hawezi kunipa,kipekee sipendi fujo nafikiria kutumia nguvu ila naona ni utoto na naweza kusababisha matatizo.Naombeni ushauri nifanyeje?
Best jamaa aliahidi huyu kuwa bint atumie laptop ya jamaa mpaka atakaponunuliwa yake na jamaa,sasa jamaa hajatimiza ahadi ati!!!
Hajatuambia lakini ndani ya miaka hiyo mitatu naye amepewa vingapi na bint na amerejesha vingapi baada ya kuachana!!!!
ibakie kama ukumbusho tu wa usaliti!?
Kwa hiyo unamuona yuko sahihi kuwa na mchumba ambaye amemvalisha pete huku akiwa na mwingne wa pembeni? au wewe umebase kwenye laptop peke yake?Haha haaaaaaaaa!
Sitaki hata like yake,ila ukweli lazima usemwe
Ukisoma vizuri utaona kuwa hayo makubaliano ya kununuliwa laptop yalitegemea status ya relationship yao!!
Usikimbilie kutaka kujua mengine ikiwa hili la laptop bado hujafanya hukumu ya haki...
Katika mahusiano ya ndoa, mtu hupaswi kubinafsisha mali za mpenzi mliyetengana...kesi kama hizi za dhuluma zimeshawaweka wengi matatizoni na huwa zipo sana mahakama za mwanzo
Hayo makosa mengine jamaa alishahukumu kwa kumuacha,mimi niko hapooo kwenye la laptop hapoKwa hiyo unamuona yuko sahihi kuwa na mchumba ambaye amemvalisha pete huku akiwa na mwingne wa pembeni? au wewe umebase kwenye laptop peke yake?
Hahahaaaa haya mama umeshinda.....kwa hiyo huo ndo mshahara wake siyoHayo makosa mengine jamaa alishahukumu kwa kumuacha,mimi niko hapooo kwenye la laptop hapo
Matatizo ya kugusa rafiki unayaona? Ukionja nyama ya mtu...... Umeniamini sasa?sasa hata kama ni mimi sikupi.... kwa sababu naachana na wewe zaidi ya migegedo na starehe na outing nimebaki na kitu gani cha kwako amna sasa... mwachie bwana miaka mitatu ujamnunulia ya kwake mwachie tu bwana.... au kama kuna kitu kingine ulimpa sema ni haali yake kung'ang'ania kabisa nampa support nipe namba yake nimpe ujanja mwingine ...
Kwani dhahabu alikuwa anachimba bila ridhaa ya mwenye mgodi?Mmechezeana miaka mi 3 leo unadai laptop kisa ya laki 9, laki tisa nini? hebu na wewe rudisha dhahabu uliyokuwa unachimba kwenye mgodi wake ndani ya miaka mitatu, ni ushamba, ni umaskini au ni nini?
kwamba mwenye hii laptop hii ni ukumbusho tosha
Happy new year
Alimuazima aitumie mpaka atakapomnunulia ya kwake,akimnunulia atarudishiwa yake!!"!!!!
Kwani hiyo laptop aliiba? si alimpa kwa makubaliano ya kumnunulia nyingine amnunulie sasa, hawezi amwachiye yeye ndo anunueKwani dhahabu alikuwa anachimba bila ridhaa ya mwenye mgodi?
Pete kitu gani Daudi1? Tena siku hizi wanazibiana rizki tu,mtu anavalishwa pete mpaka inafubaa hakuna dalili ya ndoa.
Bint angekuja akaeleza yake story inge balance,wanaume wengi wanadanganya mabint na pete then wanaanza kuwahubiria uvumilivu huku street wanaendelea kufungua wallet kama kawa!!![/QUOTE
Kwa hili chukua tano ni kweli tena style yao mpyaa wanaenda kununua pete za kavungwe wanakuja na mbwembwe nyingii wanakupotezea mdaa baadae wanakutaftia sababu baada ya kukutumia kama toilet paper. Uliona wap uchumba miaka mitatu kama sio kuzibiana rizki za ndoa... Bora hata alivyojichukulia hako ka laptop ingawa hakana thamani juu ya mda alioupoteza
Msema peke yake muongo best,natamani bint naye angekuwa member humu atupe upande wa pili wa habari.
Inawezekana hata hiyo laptop alimuuzia!!!!
Lakini si wameachana madam mbona unakuwa mkali jamani,Raisi muda wake unapoisha yale ambayo hakuyafanya atayafanya anayekuja yeye aruidishe tu hiyo laptop then atanunuliwa na mwingine atakayeshika madarakaKwani hiyo laptop aliiba? si alimpa kwa makubaliano ya kumnunulia nyingine amnunulie sasa, hawezi amwachiye yeye ndo anunue