Ama kweli ndoa ndoano

Ama kweli ndoa ndoano

Rafiki yangu wa karibu alikuwa ananisimulia changamoto anazokutana nazo kwenye ndoa yake ambayo ina umri wa miaka mitatu anasema hivi karibuni mambo yake ya kiuchumi yameenda mraba sasa imepelekea dharau kubwa kuibuka kutoka kwa mke wake ambaye yeye ana kipato cha uhakika kwakuwa ni muajiriwa ,

Anasema wakigombana kidogo anamtolea kauli za kukera " sio bure nilikubalije kuolewa na mwanaume kama wewe lazma uliniroga haikuwa akili yangu halafu mwanamke anaanika habari zao kwa ndugu zake.

Jamaa anasema alikuwa tu anasikia ndoa ni ndoano lakini amejionea mwenyewe na pia anaona utofauti akilinganisha na kipindi cha uchumba jinsi mahaba yalivyokuwa mazito.
Pole yake,sio kwamba alikosea kuoa ila asilimia 95 ya wanawake ukishakwama kwenye uchumi au akikuzidi kipato cha moto utakiona,though wapo wengine wanaojielewa sana...
 
Mwambie jamaa yako aachane na maneno ya huyo mke wake aangalie matendo zaidi, wanawake ndivyo walivyo, akiona matendo ya mkewe hayaridhishi aangalie namna nzuri ya kisaikolojia ya kumuweka sawa na akishindwa kabisa amfanyie mkewe figisu mpaka hahakikishe kaachishwa kazi .

Nb.Mwanamke anaye omba hela za matumizi kwa mwanaume ni bora zaidi kuliko mwanamke anayejiweza kiuchumi
🤣 Hii mbinu ya kijasusi ni ya kikatili na nzuri kwa upande mwengine. Kumpooza makali akiachishwa kazi lazma watakaa meza ya maridhiano.
 
Hayo mawazo ni finyu sababu kuna mwanamke wa kila mtu mzee. Ukipenda madanga unapata, ukipenda independent women wapo, ukipenda corporate women wapo. Inategemea wewe unaji position vipi.

Uamuzi ni wako sasa. Kama mhanga aliamua kuoa danga yeye apambane.
Hawezi kukupenda bila sababu , na kila mtu anasababu zake kama ambavyo pesa ni sababu mojawapo , kikubwa tujue mbinu za kuishinao

Sent from my SM-A032F using JamiiForums mobile
 
Hayo mawazo ni finyu sababu kuna mwanamke wa kila mtu mzee. Ukipenda madanga unapata, ukipenda independent women wapo, ukipenda corporate women wapo. Inategemea wewe unaji position vipi.

Uamuzi ni wako sasa. Kama mhanga aliamua kuoa danga yeye apambane.
Tuhitimishe kwa kusema kupanga ni kuchagua

Sent from my SM-A032F using JamiiForums mobile app
 
😄
Kuna ndugu yangu alioa muhindi yule mmama R.I.P alikua very humble to the earth..
Yule mama alikua na elimu ya juu ya hotel management so alikua anasimamia hotel Moja kubwa katika jiji Moja mashuhuri..
Ndugu yetu alikua anamsumbua sana kula sana mtaji mavituko mengi kedekede lakini yule mmama alikua anaupendo wa dhati Kwa ndugu yetu.....
🤣 Sasa jamaa anaendeleaje huko alipo sasa
 
Nime
kunukuu,

""Anasema wakigombana kidogo anamtolea kauli za kukera " sio bure nilikubalije kuolewa na mwanaume kama wewe lazma uliniroga haikuwa akili yangu
emoji3.png
emoji3.png
emoji3.png
halafu mwanamke anaanika habari zao kwa ndugu zake""

Mwanamke utamlisha miaka 10 ila yeye akikulisha wiki Moja anakutangaza.....

NB,

Mkuu 😊 ushaur wa Bure Kwa wanaume wenzangu ukipata muda kula vizuri kabisa kunywa vinywaji unavyo penda jitoe outing mwenyewe.
Siku nilipo gundua najibana nasaidia sana watu alafu pesa yangu inaliwa Bata ☺️😊
🤣 🤣 🤣 🤣 🤣 Week 1 kakuvumilia sana siku 3 tu lazma mabango yaanze 🤣
 
Shika, kamata na ujue, upendo ni hisia. Huyeyuka wakati wowote ule, sikwamwanaume wala mwanamke. Wanachokosea wenzetu ni kutokuwa na empathy au hekima mwenzao akienda kamba huku wakiwa wote wanavumiliana. Kilicho bora, kuishi kama tulivyoagizwa na mtume Paulo ni vyema sana, ngono ukikosa hufi na mke sio lango la uzima wa mafanikio.
Upendo ni hisia ila kiini cha upendo ndio kita determine hisia hizo zitaisha lini. Kama kiini ni pesa basi tambua siku pesa zikiisha zitaondoka na ile hisia. Kama chanzo ni umaarufu basi tambua siku umaarufu wa mwanaume ukiisha ndio itakuwa mwisho wa hisia. Kama kiini cha upendo ni utu wa mtu basi jua hautakaa uishe unless utu wa mtu umebadilika.

Theres always a spark that ignites the affection between two souls. Grave mistake ndoa nyingi za sikuhizi upendo wake umeshikiliwa na ajira ya mume na pesa za michongo anazopiga ofisini. Ikitokea hela hizo zimekata basi penzi linakata na migogoro kuanza straight away.
 
Kuwa mwanamke ni ngumu sana sjui kwann tuliekewa hiki kitabia chakupenda pesa. Hakuna mwanamke asopenda pesa ya kupewa ni vile tunazidiana utashi wa kudhibiti tamaa zetu.

Huyo dada bila shaka alirogwa na ukwasi wa mshkaji akakubali kuolewa Sasa sahvi mapesa yameondoka na yeye upendo umetoka. Rafiki ako atafute Hela tu hakunaga upendo bila pesa bhana
Ndio ufunguo aliotumia kuingia kwenye moyo wa mkewe. Atafte hela hamna namna ingine.
 
Nadhani tuanze kuwaelimiaha watu kwamba ndoa ikikushinda sio lazima ung'ang'anie, unaweza kuiacha kwa amani.
Halafu labda ndoa za mkataba kwa dunia ya sasa ndo zinazofaa, tuachane na mambo ya kizamani.
Sawa Sawa Madam umesomeka , nahitaji muongozo kutoka kwako nitawezaje kumpata mtu mwenye kujielewa kama wewe ?

Sent from my SM-A032F using JamiiForums mobile app
 
Hio ndio Tabia halisi ya mke wake, inatakiwa muelewe neno uchumba ni maisha feki ndoa ni Maisha halisi.
Oa yeyeto umpendae ukimpatia utamshukuru Mungu ukikosea utakuwa mshauri wa ndoa
 
Mwambie awe mpole meli itakaa sawa tu ikishatulia kwenye maji.
Utaacha wa ngapi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom