Ama kweli ndoa ndoano

Ama kweli ndoa ndoano

Upendo ni hisia ila kiini cha upendo ndio kita determine hisia hizo zitaisha lini. Kama kiini ni pesa basi tambua siku pesa zikiisha zitaondoka na ile hisia. Kama chanzo ni umaarufu basi tambua siku umaarufu wa mwanaume ukiisha ndio itakuwa mwisho wa hisia. Kama kiini cha upendo ni utu wa mtu basi jua hautakaa uishe unless utu wa mtu umebadilika.

Theres always a spark that ignites the affection between two souls. Grave mistake ndoa nyingi za sikuhizi upendo wake umeshikiliwa na ajira ya mume na pesa za michongo anazopiga ofisini. Ikitokea hela hizo zimekata basi penzi linakata na migogoro kuanza straight away.
Katika yote hapa nakupa asilimia elfu moja

Sent from my SM-A032F using JamiiForums mobile app
 
Rafiki yangu wa karibu alikuwa ananisimulia changamoto anazokutana nazo kwenye ndoa yake ambayo ina umri wa miaka mitatu anasema hivi karibuni mambo yake ya kiuchumi yameenda mraba sasa imepelekea dharau kubwa kuibuka kutoka kwa mke wake ambaye yeye ana kipato cha uhakika kwakuwa ni muajiriwa ,

Anasema wakigombana kidogo anamtolea kauli za kukera " sio bure nilikubalije kuolewa na mwanaume kama wewe lazma uliniroga haikuwa akili yangu halafu mwanamke anaanika habari zao kwa ndugu zake.

Jamaa anasema alikuwa tu anasikia ndoa ni ndoano lakini amejionea mwenyewe na pia anaona utofauti akilinganisha na kipindi cha uchumba jinsi mahaba yalivyokuwa mazito.
Acha tuwaombee (kidumu chama cha kataa ndoa) "CHAKANDO"
 
Big noo , jamaa yako hajakosa hela , amepungukiwa tuu Kwa kiwango ambacho huyo slayqeen wake kinamtoa kwenye mudi, mwanamke akikupenda acha kabisa , atakutia moyo Sana na atafanya kila liwezalo uinuke...na kabla ya kuoa wanaume wote huwa tunapitia kwenye uamuz wa makundi hayo mawili , demu unayemfukuzia na demu anayekupenda , mara nyingi huwa tunaangukia Kwa demu unayemfukuzia na kumtosa anayekupenda , shughuli huanza ukiishiwa mtaji
You nailed it bro! Maelezo yako yanafikirisha sana na ndio hali halisi ilivyo
 
Utu ndio kila kitu, tushaongea sana sasa wacha waendelee kuoa matako huku wakidhani maisha huwa ni kitonga milele daima.🤣 Oh siwezi kuoa mwanamke wa kawaida bora nioe mzuri tutarekebishana.
Usioe au kuolewa na mtu kwa kuangalia mambo ya nje ie sura, umbile,sijui elimu, au hali yake ya uchumi, ingawa sikatai kuna preference au features ambazo kila mtu anazipenda lakini ni muhimu kuangalia utu, background ya muhusika especially aina ya familia alnayotoka na malezi aliyopewa, historia ya familia yao na imani yake

Utu wa ndani, upendo, uvumilivu na kubebana katika kila hali, vitu ambavyo unaweza kuvipima wakati wa uchumba, umewahi hata kupretend umefukuzwa kazi au umefunga biashara japo kwa mweI mmoja au miwili uone mchumba wako atachukulia vipi hilo swala?
 
Wosia wa shida na Raha Huwa unaishaia kwenye mlango wa kanisa,shida na Raha ni ya mwanaume pekee Raha ni wote.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom