Ama kweli ndoa ndoano

Ama kweli ndoa ndoano

Asie sikia la mkuu huvunjika guu
Hiyo ndio hali halisi au tabia halisi ya huyo mke,kipato cha mumewe kilikua tu kinaificha hiyo tabia yake,

Mshukuru Mungu amekupa mtihani ili ugundue kua huyo sio mke,sikuombei mabaya ila siku ikitokea ukaugua na kushindwa hata kujitafutia riziki,huyo mwanamke atakunyanyasa sana au hata kukuacha ukiwa katika hali hiyo,

Huyo sio Mke,hakufai kabisa coz huo ndio ulikua mtihani wa kumtambua jinsi alivyo,achana nae mara moja kabla hayajakufika makubwa zaidi,na kitendo cha kukutangaza mpaka kwa ndugu zake nacho hakivumiliki,

Yangu ni hayo tu,the rest it's up to you.
 
Mwambie jamaa yako aachane na maneno ya huyo mke wake aangalie matendo zaidi, wanawake ndivyo walivyo, akiona matendo ya mkewe hayaridhishi aangalie namna nzuri ya kisaikolojia ya kumuweka sawa na akishindwa kabisa amfanyie mkewe figisu mpaka hahakikishe kaachishwa kazi .

Nb.Mwanamke anaye omba hela za matumizi kwa mwanaume ni bora zaidi kuliko mwanamke anayejiweza kiuchumi
NB imekaa poa
 
Rafiki yangu wa karibu alikuwa ananisimulia changamoto anazokutana nazo kwenye ndoa yake ambayo ina umri wa miaka mitatu anasema hivi karibuni mambo yake ya kiuchumi yameenda mraba sasa imepelekea dharau kubwa kuibuka kutoka kwa mke wake ambaye yeye ana kipato cha uhakika kwakuwa ni muajiriwa ,

Anasema wakigombana kidogo anamtolea kauli za kukera " sio bure nilikubalije kuolewa na mwanaume kama wewe lazma uliniroga haikuwa akili yangu halafu mwanamke anaanika habari zao kwa ndugu zake.

Jamaa anasema alikuwa tu anasikia ndoa ni ndoano lakini amejionea mwenyewe na pia anaona utofauti akilinganisha na kipindi cha uchumba jinsi mahaba yalivyokuwa mazito.
Avumilie tu.....
 
Tatizo hili linatibika Kwa kuoa mwanamke anayekupenda
Shika, kamata na ujue, upendo ni hisia. Huyeyuka wakati wowote ule, sikwamwanaume wala mwanamke. Wanachokosea wenzetu ni kutokuwa na empathy au hekima mwenzao akienda kamba huku wakiwa wote wanavumiliana. Kilicho bora, kuishi kama tulivyoagizwa na mtume Paulo ni vyema sana, ngono ukikosa hufi na mke sio lango la uzima wa mafanikio.
 
Shida kivipi mkuu.. ? Ulitaka niseme waachane?? MUNGU anachukia Talaka
Mungu pia anachukia dharau, kebehi na kutofuata maandiko yake kwamba mke atamtii mume wake, so usimtaje jina lake bure. Kila mtu achukue hamsini zake, amani ni bora kuliko kukaa na mwanamke mkorofi. Akikubali kumrudia nitamshangaa sana. Bora kuishi mwenyewe bila mke au mwanamke. Haufi!
 
Kuwa mwanamke ni ngumu sana sjui kwann tuliekewa hiki kitabia chakupenda pesa. Hakuna mwanamke asopenda pesa ya kupewa ni vile tunazidiana utashi wa kudhibiti tamaa zetu.

Huyo dada bila shaka alirogwa na ukwasi wa mshkaji akakubali kuolewa Sasa sahvi mapesa yameondoka na yeye upendo umetoka. Rafiki ako atafute Hela tu hakunaga upendo bila pesa bhana
 
Rafiki yangu wa karibu alikuwa ananisimulia changamoto anazokutana nazo kwenye ndoa yake ambayo ina umri wa miaka mitatu anasema hivi karibuni mambo yake ya kiuchumi yameenda mraba sasa imepelekea dharau kubwa kuibuka kutoka kwa mke wake ambaye yeye ana kipato cha uhakika kwakuwa ni muajiriwa ,

Anasema wakigombana kidogo anamtolea kauli za kukera " sio bure nilikubalije kuolewa na mwanaume kama wewe lazma uliniroga haikuwa akili yangu halafu mwanamke anaanika habari zao kwa ndugu zake.

Jamaa anasema alikuwa tu anasikia ndoa ni ndoano lakini amejionea mwenyewe na pia anaona utofauti akilinganisha na kipindi cha uchumba jinsi mahaba yalivyokuwa mazito.
Avumilie yana mwisho yatapita atasimama tena

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nahisi hii inakuhusu wewe
Rafiki yangu wa karibu alikuwa ananisimulia changamoto anazokutana nazo kwenye ndoa yake ambayo ina umri wa miaka mitatu anasema hivi karibuni mambo yake ya kiuchumi yameenda mraba sasa imepelekea dharau kubwa kuibuka kutoka kwa mke wake ambaye yeye ana kipato cha uhakika kwakuwa ni muajiriwa ,

Anasema wakigombana kidogo anamtolea kauli za kukera " sio bure nilikubalije kuolewa na mwanaume kama wewe lazma uliniroga haikuwa akili yangu halafu mwanamke anaanika habari zao kwa ndugu zake.

Jamaa anasema alikuwa tu anasikia ndoa ni ndoano lakini amejionea mwenyewe na pia anaona utofauti akilinganisha na kipindi cha uchumba jinsi mahaba yalivyokuwa mazito.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom