Aliyewahi kufanya mchakato wa talaka msaada

Aliyewahi kufanya mchakato wa talaka msaada

Nashukuru nimepata visa vyako

Kuna uzi zimepandishwa poa kabisa hapo.
amu katag story ya nyuma poa kabisa.

Sasa nikushauri hivi.

Huyo jamaa si chaguo lako.

Ondoka. Kwanza una uvumilivu uliotukuka.
Sepa. Usitafute talaka mapema. Akibadilika badae mkayajenga it's Ok. Ila kwa sasa. SEPA.
 
  • Thanks
Reactions: amu
Hehehehe, ukiwa na mke anatumia jf hapo hakuna kitu.

Watu wa jf mna nn? Mmeolewa na kuoa kweli? Mbona hakuna hata anaeshauri kusuluhisha?
Kila mmoja hapa anataka ndoa ivunjike. Mna nn nyinyi wana wa jf?
Miaka siyo, mmoja hapo kimara kafa kifo cha kutatanisha hata hajazikwa bado


Wanawake wanaogopa kusemwa au wanawaza mali na hivyo ndo vinakufanya unabaki ukilia lia hadi umauti unakukuta ndani.

Mwanaume anakuambia ...nitakuua nikafungwe..
na wewe uko tu, mara ulale jikoni mara chumba cha watoto mara car parking unatesekea hapo hapo.

Niliondoka na watoto tu vingine vyote hadi nguo niliacha.

Mungu hakuniacha, leo hii ninaweza kusema .. Mungu kwangu ni Bwana, amenitendea makubwa.

Don't afraid, laiti ungekuwa bongo au pwani ningekupa hifadhi ya kuanzia maisha.
 
Umesema una mpenda Soma hichi kitabu, kitakusaidia then hutaki kumwacha just ignore him maisha yaendelee
Screenshot_20200625-092053_1593066138929.jpg
 
Muone mwanasheria
Talaka inategemea aina ya ndoa na dini zenu
Well said mkuu. Anaweza kuanzia kwangu. Sijui nawezaje kumuita kwenye hii comment, bilashaka utanisaidia.

Kimsingi, maombi ya talaka yanaweza kufunguliwa mahakama ya mwanzo, mahakama ya wilaya/mahakama ya hakimu mkazi au mahakama kuu. Ila busara inatutaka tuanzie mahakama ya chini, mathalani, mahakama ya mwanzo, ili asiporidhika na maamuzi asipoteze haki ya kukata rufaa kwenda mahakama za juu zaidi.

Kabla ya kupelekea maombi ahakikishe amepitia baraza la usuluhishi, mabaraza haya yanapatikana kwenye kila kata na kwenye makanisa/misikiti. Baraza hili litawaita na kujaribu kuwasuluhisha. Likishindwa litaandika 'hati' ambayo ni lazima iambatanishwe kwenye maombi ya talaka. Hati hii haitakuwa ya lazima kama mwenza wake hataki kwenda, hapatikani n.k.

Vilevile, ili ndoa ifike ukingoni lzm kuwe na sababu za msingi kama vile ugoni, mwenza mmoja kuwa kichaa;na kwa uthibitisho wa daktari bingwa ni kwamba mwenza huyo hawezi kupona ndani ya kipindi cha miaka mitano, vipigo vilivyokithiri (lakini lazima kuwe na ushahidi) kama PF3 au ushahidi wa majirani, n.k.

Akishafuata taratibu hizo hapo juu amuone mwanasheria kwa ajili ya kuandaliwa maombi maalumu ya kuwasilishwa mahakamani, isipokuwa kama anafungua maombi haya mahakama ya mwanzo, ambapo atakwenda moja kwa moja mahakamani na kuwaeleza makarani wa mahakama adhma hii.

Aidha, nampa pole sana. Nimeandika Kitabu chenye title hii; "DONDOO MUHIMU ZA NAMNA YA KUKABILIANA NA KESI ZA ARDHI, JINAI, MADAI, MIRATHI NA NDOA HASA KWA WASOMAJI WASIO WANASHERIA NA WANASHERIA WACHANGA (SOMO FUPI LA SHERIA KWA VITENDO)". Kinaweza kuwa msaada kwake na kwa wengine pia. Bei ni shilingi elfu kumi tu za Kitanzania. Napatikana Dodoma ila mikoani natuma.

Aksanteni!
 
Well said mkuu. Anaweza kuanzia kwangu. Sijui nawezaje kumuita kwenye hii comment, bilashaka utanisaidia.

Kimsingi, maombi ya talaka yanaweza kufunguliwa mahakama ya mwanzo, mahakama ya wilaya/mahakama ya hakimu mkazi au mahakama kuu. Ila busara inatutaka tuanzie mahakama ya chini, mathalani, mahakama ya mwanzo, ili asiporidhika na maamuzi asipoteze haki ya kukata rufaa kwenda mahakama za juu zaidi.

Kabla ya kupelekea maombi ahakikishe amepitia baraza la usuluhishi, mabaraza haya yanapatikana kwenye kila kata na kwenye makanisa/misikiti. Baraza hili litawaita na kujaribu kuwasuluhisha. Likishindwa litaandika 'hati' ambayo ni lazima iambatanishwe kwenye maombi ya talaka. Hati hii haitakuwa ya lazima kama mwenza wake hataki kwenda, hapatikani n.k.

Vilevile, ili ndoa ifike ukingoni lzm kuwe na sababu za msingi kama vile ugoni, mwenza mmoja kuwa kichaa;na kwa uthibitisho wa daktari bingwa ni kwamba mwenza huyo hawezi kupona ndani ya kipindi cha miaka mitano, vipigo vilivyokithiri (lakini lazima kuwe na ushahidi) kama PF3 au ushahidi wa majirani, n.k.

Akishafuata taratibu hizo hapo juu amuone mwanasheria kwa ajili ya kuandaliwa maombi maalumu ya kuwasilishwa mahakamani.

Aidha, nampa pole sana. Nimeandika Kitabu chenye title hii; "DONDOO MUHIMU ZA NAMNA YA KUKABILIANA NA KESI ZA ARDHI, JINAI, MADAI, MIRATHI NA NDOA HASA KWA WASOMAJI WASIO WANASHERIA NA WANASHERIA WACHANGA (SOMO FUPI LA SHERIA KWA VITENDO). Kinaweza kuwa msaada kwake na kwa wengine pia. Bei ni shilingi elfu kumi tu za Kitanzania. Napatikana Dodoma ila mikoani natuma.

Aksanteni!
Hicho kitabu unacho Cha online pia au una hard copy tu.?
 
Weka online pia maana naweza kukihitaji Sasa kutuma hard copy ni gharama nyingine kikiwa online mtu anakutumia pesa wamtumia kwa email .
Ushauri mzuri sana huu mkuu. Nitaufuata. Weka email yako hapa au ni-PM kama hutojali ili kikiwa tayari online nikujuze.
 
Ushauri mzuri sana huu mkuu. Nitaufuata. Weka email yako hapa au ni-PM kama hutojali ili kikiwa tayari online nikujuze.
Siwezi weka email yangu hapa nitakuwa nimeharibu privacy yangu bure humu, Ila I need that book when ur ready kindly inform me
 
kabla ya kwenda mahakamani lazima mpitie kwenye mabaraza ya usuluhishi yanayopatikana makanisani, misikitini, au ustawi wa jamii.

Huko mtapewa cheti konesha kuwa usuluhishi umeshindikana.

Mtaenda mahakamani kuvunja ndoa, kugawana mali na malezi ya mtoto/watoto.

Sababu za kuvunja ndoa.

1. Ukatili.
2. Zinaa.
3. Kushindwa kutoa tendo la ndoa.
4. Kutengwa kwa muda mrefu.
ect.

Mahakama haitavunja ndoa bila kwanza kupitia hatua za usuluhishi.

Ndoa ikishavunjwa mtapata hati rasmi ambayo mtasajili Rita.

Tafuta wakili akuongoze.
Upo vizuri mkuu.Yalishakupata nini
 
Huoni kama ni jeuri tu fulani..anayetegemea mitandao kutatua matatizo ya ndoa yake.

Tizama anavyopewa jeuri na wachangiaji hapo juu. Akila panga tutakutana hapa kusema RIP RIP RIP.

Kumbe moto tumeuchochea sisi.

Wacha tuone.
Wewe Ndo Mbaba nini.Talaka.inakuja
 
Miaka siyo, mmoja hapo kimara kafa kifo cha kutatanisha hata hajazikwa bado


Wanawake wanaogopa kusemwa au wanawaza mali na hivyo ndo vinakufanya unabaki ukilia lia hadi umauti unakukuta ndani.

Mwanaume anakuambia ...nitakuua nikafungwe..
na wewe uko tu, mara ulale jikoni mara chumba cha watoto mara car parking unatesekea hapo hapo.

Niliondoka na watoto tu vingine vyote hadi nguo niliacha.

Mungu hakuniacha, leo hii ninaweza kusema .. Mungu kwangu ni Bwana, amenitendea makubwa.

Don't afraid, laiti ungekuwa bongo au pwani ningekupa hifadhi ya kuanzia maisha.
😃😃
Sijui kwa nini kila nikikuona nawaza ile story yako kwenye uzi wa kulana kimasihara.
wewe mwanamke sio kabisa
hahahaha
 
mhhh hivi ndoa za siku hizi zina mapepo?au mapepo ni wanandoa wenyewe?
 
Back
Top Bottom