Dada kama mambo ya kuvumilika baki kwenye ndoa yako huku kwenye usingle sio kuzuri ......
Hiyo hali ya maumivu mpaka kuhisi kufa kufa ni hali iliyopo kwenye mapenz mengi cjui mume amecheat,sijui Kazaa nje vumilia dada , unaweza kudai muachane afu ndani ya usingle unaanza date mume wa mtu au ben10 ambae nae anakigf
Vumilia na usali sana, mkabidhi mungu mumeo na ndoa yako
Finest umesema neno la maana sana! kuna rafiki yangu wa kike yeye kila akipata mtu ni mume wa mtu!
Mi naamini hakuna lisiloshindikana,amani haiji kwa njia ya mtutu,ndio maana hata mataifa yakigombana only vikoa vya upatanishi na usuluhishi.
Shida ktk ndoa kuna wanaume mabwege sana,kuna wanawake mabwege pia,kuna wanume welevu na wanawake welevu pia, usipokubali kujishusha ktk migogoro na mkaongea kwa lugha nyepesi basi ujue ngoma nzito.
Sio wazazi wetu walikuwa bora zaidi ila walivumiliana sana na kubebana,kwa mfano kumkuta mama anapambana na baba kwa maneno makali ni nadra sana.
Kumkuta baba anampa kipigo mama hata mtaani huoni kabisa.
Tumeacha maadili yetu,haki sawa,we unitishi mwanume utakuwa wewe,we mwanamke gani sura huna nk.
Vipigo maneno na dharau vinazoofisha sana ndoa zetu.
Alafu bahati nzuri kizazi chetu sio ndio tunapeleka wenzetu kuwatambulisha kwa wazazi kuwa tumependana lkn enzi za wazee wetu walikuwa wanachaguliwa mke,ndoa zilidumu mnooo sijui tunakwama wapi kizazi hiki?
Kudharauliana,kutoheshimiana,kutovumiliana,jeuri ya fedha,kunyima unyumba nk ni moja ya matatizo makubwa sana ktk ndoa zetu.
Ukitaka umuone mwanaume mbaya mnyime unyumba na umdharau aisee ndoa iko hatarini.
Mwanamke ukitaka umtake ubaya kwa kizazi hiki umnyanyase,umletee umalaya,umdharau kisa pesa,umpige means mfume dume. wa sasa ni 50 50 japo ngumu sana kuipata dada zangu chukueni +ve vibes tu huko kwenye makongomano,mnafundwa vzr kwenye kitchen party mkija ndani mnasahau kila nafikiri huwa mnataka zawadi tu na makabati tu...!
Mwayego utampoteza mke kizazi hiki cha kike akipigwi wazee....ongea nae kwa busara.
Nina mengi ya kuwajuza mwezi November 2020 natimiza 10years ktk hii sector.
Nimeshuhudia mengi ya kwangu nawenzangu,nishauri tu mdada kama jamaa kazingua embu omba uende kwende kwenu upumzike kdg...
Ntaendelee next time, kuna mambo mengi sana ktk ndoa mazuri na mengine ya kuchosha na kukatisha tamaaa.
Kikubwa me tuishi kwa akili na ke,...! tuwapende,watatuheshimu au mtuheshimu tutwapenda..... mwanaume acha kuomba kupendwa na mkeo we kwani ni demu? embu kila mtu aplay part yake ktk maisha...
Alafu wanume mke jukumu la kulisha familia sio lake ni msaada tu wanatupa....sijui nataja mke mwenye kazi ili akusaidie kulisha si ndio?
Mie huwa nakopa kwake, nikichoka utasikia mzee huna hela we chukua laki hii nenda kwa wenzio upate mawazo mapya!
Ohooooo men tuishi nao kwa IQ