Aliyewahi kufanya mchakato wa talaka msaada

Hivi mbona hankomi nyinyi.. Akina Kiria wana waharibu sana nyinyi.

Anyway. Kazi kwako.
 
Anzia baraza la kata sehemu unayoishi watawasulihisha ikishindikana watakujazia fomu maalumu utaenda nayo mahakama ya mwanzo then huko utafungua kesi ya madai ya talaka. Mtasikikizwa then at the end talaka itatoka. Hata km ndo ni ya kanisani mahama ndo chombo pekee kina mamlaka ya kuvunja ndoa kisheria
 
Nakuelewa.

Lakini vipi kama yupo kwenye ndoa inayotishia usalama wa afya na uhai wake? Anapaswa kuendelea kuvumilia?
Huoni kama ni jeuri tu fulani..anayetegemea mitandao kutatua matatizo ya ndoa yake.

Tizama anavyopewa jeuri na wachangiaji hapo juu. Akila panga tutakutana hapa kusema RIP RIP RIP.

Kumbe moto tumeuchochea sisi.

Wacha tuone.
 
Ondoka haraka talaka ukaitafufie huku umeshatoka kwake. Marehemu Mercy Mkandala inasemekana kuanza process za talaka akiwa ndani na mbaya wake. Ameishia kuuawa
Mleta mada kamata hii. Ni muhimu mno.
 
Maisha ni vile unavyopanga mwenyewe,
Uamue kujenga au kupanga ni wewe,
Kusuka au kunyoa ni wewe,
Uende kushoto au kulia ni wewe.

Linex Sunday Mjeda.
 
Pole mkuu.

Mimi sitofautiani na waliotangulia ila nitoe ushauri kidogo ama kusisitiza.

1. Ondoka haraka hapo unapoishi, process zako zote kuanzia baraza la usuluhishi ni lazima usiwe unaishi na huyo mtu.

2. Uendapo katika Baraza la usuluhishi hakikisha kuwa unapambana haswa, ikiwezekana hata vurugu, yaani wao Baraza wasitoke na suluhisho la ninyi kuwatenganisha ila watoke na suluhisho la ninyi kwenda mahakamani kwa kuwapa barua.

Kwanini nasema hivi, Baraza wanatazama huu mgogoro wenu ni wa ngapi, mshawahi kuwekwa chini na kupatanishwa, ukubwa wa mgogoro n.k

Baraza endapo likaona vurugu ni kubwa huwa siku hiyo hiyo wanatoa barua ili iende mahakamani na kwa bahati mbaya baraza la usuluhishi wanasheria hawaruhusiwi, hata kama una ndugu hawaongea chochote kile, wazungumzaji ni ninyi tu.
 
Huoni kama ni jeuri tu fulani..anayetegemea mitandao kutatua matatizo ya ndoa yake.

Tizama anavyopewa jeuri na wachangiaji hapo juu. Akila panga tutakutana hapa kusema RIP RIP RIP.

Kumbe moto tumeuchochea sisi.

Wacha tuone.

Kwahiyo kudai talaka ni ujeuri?
 
Mawazo ushauri sababu nahisi nakufa soon.
Aliyewahi pitia hili swala naomba ushauri

Japo mi sijaona kubwa la kukufanya uvunje ndoa.

Yaani umeshindwa kabisaa kukubaliana na wanavyoishi mumeo na nduguze? Umeshindwa kabisaa kufuata aina ya maisha yao?

Au Kuna mengine zaidi ya yale?

Talaka si nzuri sana kitu cha kukimbilia, watoto huteseka sana.

Hapo ukubali kutunza mtoto mwenyewe, usitegemee kupata matunzo toka kwa babake kirahisi.

Kama Kuna Mali mlichuma basi mtauza hii itawarudisha nyuma kimaendeleo.
 
Mawazo ushauri sababu nahisi nakufa soon.
Aliyewahi pitia hili swala naomba ushauri
Pole sana kwa magumu unayopitia lakini kumbuka kuwa maisha yamejaa changamoto ambazo inahitaji maombi ili kushinda matatizo yanayo kukabili, Ndoa ni mtihani mgumu pale unapokuwa na mwenza mlevi, ugomvi, uzinzi na kupelekea mahusiano yenu ndani ya nyumba kulega.
Kwa kuwa uliapa kuishi wote mpaka kifo kiwatenge basi vumilia tu hili litapita.
Kila jaribu litapita vumilia ulee mtoto wako maana hata huku utapata wanaume suruali wa kuvaa machoni na kunyoa viduku lazma wa kuumize tu.
Pole sana Mungu akujalie moyo wa uvumilivu katika magumu unayopitia.
 
Back
Top Bottom