Jana majira ya saa tisa Alasiiri mchana nilipokea ujumbe kwenye PM juu ya mtu aliyekuwa kapoteza pochi yenye pesa. Ujumbe ule uliambatanishwa na namba ya simu, na jina halisi la mwenye pesa kama tu lilivyokuwa kwenye driving license na akataja kiasi halisi cha pesa. Wanajamvi mlinitaka akipatikana mwenye mali nilete feedback, nami nimefanya hivyo.
Ilivyokuwa;
Mwenye pesa si mwana JF mwenzetu, ila rafiki yake ndo mwana JF ambaye alikuwa na taarifa za rafiki yake kupoteza pesa, alipoteza pesa hizo katika ugomvi na mpenzi wake walipokuwa wakitokea bar ya Afri center, nimekutana nao wote jana na wakakubali majina yao niyaweke humu na pesa alizokuwa kapoteza ilikuwa sh 635,000 zikiwa kwenye mkoba mdogo wa kike. Mpotezaji anaitwa Herieth Kanakaitwa mrembo wa haja, rafiki yake ambaye ndo mwana JF mwenzetu anaitwa Zuhura saidi, amegoma nisiweke ID yake.
Walinipa laki mbili kama shukrani, dada huyu katokea kunipenda sana tena sana, amelia sana machozi ya furaha, alijua ndo basi tena, anasema mimi sasa nimekuwa ndugu yake, bravo JF.