Tatizo mnakurupukia mambo bila kufikirisha akili, kabla ya kukimbilia kwenye conspiracies ulitakiwa kwanza uiache akili yako ijiulize maswali chanya na kufanya utafiti wa kitu kinachoongelewa, ungesoma kwanza historia ya kampuni ya Apple ungengamua mapema tu mahusiano ya tunda la Apple na Kampuni yenyewe!
Jobs na Wosniak wakati wanaanza ujasiriamali huu hawakuwa na kitu mfukoni zaidi ya ujuzi wao, hivyo waliamua kutafuta soko kwa kutumia prototype walokuwa nayo tayari. Duka moja la computer liitwalo Byte lilikuwa interested na hiyo computer, wakatoa offer ya kununua pc 50 kwa bei ya $500@, payment on delivery! Kisa cha mwenye duka (Bytes, siyo Jobs wala Wosniak) kuuza kwa $666.66 ni kuongeza Robo moja ya bei ya kununulia katika bei ya kuuza ndiyo ikaja hiyo $666, yaani: 500/3=166.6666666666667+500=666.6666666666667!
Hilo tunda la tufaa katika logo yao lina historia ndefu, logo ya mwanzo kabisa ilikuwa picha ya Isack Newton akiwa chini ya mti wa mtufaa (kama umesoma sayansi niskuchoshe unaijua vizuri habari ya huyu jamaa na story ya tufaa). Jobs pia amewahi kufanya kazi katika mashamba ya tufaa.
Kadri muda ulivokuwa ukienda Apple walianza kuangalia sana suala la design na mvuto wa bidhaa kwa mteja, walibadili nembo yao mara kadhaa ili kuleta apeal mbele za watu. Hilo tunda la Apple na lenyewe ni miongoni ya alama za mnyama?...teh! Tuache mawazo hasi. Nikiangalia kwa umakini kichwa chako naona kimekaa kipembetatu, chicks zako zinafanya vipembe tatu ukitabasamu, kidevu kimechongoka chini na kufanya pembe tatu...wewe nawe vipi, siyo free masson kweli wewe....lol!