Ajali ya basi la Isamilo na Libanika, alfajiri ya leo

Ajali ya basi la Isamilo na Libanika, alfajiri ya leo

Hao wote wamefanyishwa mitihani na kuthibitishwa huko LATRA na pia ku-renew leseni zao waliombwa vyeti vya taaluma ya udereva kutoka VETA.

Bila kusahau hayo mabasi yamekaguliwa polisi yana sticker ya Wiki ya nenda kwa usalama.

Uzembe unadhibitiwaje?
Barabara zipanuliwe njia nne,
Huduma za treni mikoa yote, ni ushamba mkubwa sana karne hii watu wanalazimika kusafiri zaidi ya Km 200 kwa mabasi.
 
Hao wote wamefanyishwa mitihani na kuthibitishwa huko LATRA na pia ku-renew leseni zao waliombwa vyeti vya taaluma ya udereva kutoka VETA.

Bila kusahau hayo mabasi yamekaguliwa polisi yana sticker ya Wiki ya nenda kwa usalama.

Uzembe unadhibitiwaje?
Tatizo la kwanza ni rushwa ndiyo chanzo cha kwanza cha pili miundo mbinu
 
Ajali mbaya za basi la Isamilo linalofanya safari zake Mwanza-Dar kugongana uso kwa uso na basi la Libanika (Dar-Mwanza) iliyotokea alfajiri ya leo, kijiji cha Msembeta, kata ya Nala, wilaya ya Dodoma, mkoa wa Dodoma.

Kumekuwa na ripoti za vifo kadhaa na majeruhi wengi

Chanzo cha ajali ikiwa ni mwendokasi wa basi la Isamilo (linatoka Mwanza kwenda Dar) , ku overtake lori kwenye mlima na likiwa kwenye kona kali, kulivamia basi la Libanika lililokuwa linatoka Dar kwenda Mwanza

Updates
=========================
Wamefariki watu 9 ikiwemo dereva, makondakta na abiria
Jumla ya majeruhi ni 66 na 9 kati yao wameripotiwa kuwa katika hali mbaya na wanaendelea kupatiwa matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma
==========================

View attachment 3641954
View attachment 3641874View attachment 3641875
View attachment 3641983
View attachment 3641876
Kwenye ajali za mabasi akifa dereva na kondakta Mimi naita GG yaani both to score!
 
Hata juzi hapo kuna basi la Manyara limegongana uso Kwa uso na Lori, Kwa mujibu wa mashuhuda ni kwamba watu sita walifariki, watu wamekatika vibaya Sana and probably kuna zaidi watakaokufa maana Ile basi ni kama imekatika hivi....

Yani Ile trailer imekwenda kukata upande wa dereva kama kisu shwaa ikapita na wale waliokaa kulia, dereva mwenyewe licha ya kuwa kafariki lakini pia amekatika vibaya Sana, dereva Kipindi anaiona ajali hii hapa alisikika Tu akisema "Watoto wangu jamani" then kishindo Kikubwa...Konda hakuumia kabisa mzimaaa maana nasikia konda alivyoona Hapa kama kuna ajali basi akakimbilia kurudi nyuma ndio Pona Yake.

Mwenye Lori ndio mwenye Tatizo ame overtake reckless....
Ningekuwa na mamlaka ningepiga marufuku kuovertake.
Ajali zote duniani asilimia 99.ni kuovertake.
 
RIP marehemu na pole nying kwa majeruhi.
Hii week kumetokea ajali nying za mabus ya abiria.

NB: mm Huwa nakaa siti ya katikati .
Upande wa Dereva.
abadan sikaagi siti za mbele.

Hao Abiria wa mbele sijuo kama wametoka salama.
vipi siku ikigongwa katikati
 
Ajali haina kinga lakini ajali nyingi nchini kwetu zinachangiwa na mfumo wa kizamani wa miundombinu yetu. Tanzania asilimia kubwa ya usafiri tunategemea barabara lakini hatuko serious kabsaa kwenye issue ya barabara. Kwa hali ilivyo sasa hivi huwezi kukwepa njia nne (mbili zinaenda na mbili zinarudi) ambazo ni lazima katikati ziteganishwe na tuta/ bustani kuzuia magari kuhamia upande mwingine. Hiyo pekee itasaidia sana kupunguza ajali. Hapo labda watu wagongane back to back na sio head on collision 💥. SGR inajengwa sawa lakini bado issue ya barabara haipaswi kupuuzwa hata kidogo. Baadhi ya nchi Africa wanatumia barabara za namna hiyo siku nyingi tu so tusiseme hatuna uwezo huo Bali tuna changamoto kubwa ya vipaumbele muhimu vya kitaifa
 
Ningekuwa na mamlaka ningepiga marufuku kuovertake.
Ajali zote duniani asilimia 99.ni kuovertake.
Yaani mwenye Lori kabla haja overtake, mbele Yake Kulikuwa na Fuso, mwenye Fuso akampa ishara dereva wa Lori kuwa usinipite mbele kumekaa vibaya, dereva wa Lori akakaza fuvu akamu overtake mwenye Fuso, dereva wa Lori anamaliza akakutana na Hilo basi nalo limeiva, ndo wakachinjana...Yani ni harufu za damu, unaona nyama Tu kama watu wamechinjwa vile, watu wa malori wengi ukigongana nao lazima uumie vibaya...
 
Yote hii ni shauri ya kutozingatia taaluma ya udereva. Una-overtake vipi kwenye mlima na uko mwendo kasi? Dereva lipungukiwa maarifa ya udereva! Ajali zinazotokana na ubovu wa gari ni chache mno, nyingi ni hizi za kusababishwa na binadamu.
Sidhani kama kuna dereva wa bus huwa anazingatia sheria, hawa jamaa huwa wana overtake hadi kwenye zile kona za barabara ya Dom- Iringa.

Tena haoni mbele.
 
Sidhani kama kuna dereva wa bus huwa anazingatia sheria, hawa jamaa huwa wana overtake hadi kwenye zile kona za barabara ya Dom- Iringa.

Tena haoni mbele.
Ila madereva wengine sijui huwa wana nini, ningekuwa na mamlaka sheria za dereva anaefanya makosa zingekuwa kali vibaya mnoo, hawajali kuhusu roho za watu kabisa. Kuna siku nimepewa lifti kwenye gari wamejaa familia nzima baba mama na mtoto wanatoka mjini, tumefika mahali kumbe Lori limeovertake halafu limeiva ghafla liko upande wetu,baba wa familia akatupeleka kwenye mtaro ndo ilikuwa ponapona yetu, ile siku sitasahau na yule dereva wa lile lori hata kama simjui sijawahi kumsamehe. Yaani ile siku wote tulikua tunafia pale pale na kigari chetu. Kinachoniuma yule dereva aliendelea na kazi na pengine hata amesababisha ajali na vifo huko alipo. Uzembe wa kiwango cha SGR.
 
Serikali ikitaka Hawa mbwa waende kufanya mitihani Darasani mnawatetea
Ila madereva wengine sijui huwa wana nini, ningekuwa na mamlaka sheria za dereva anaefanya makosa zingekuwa kali vibaya mnoo, hawajali kuhusu roho za watu kabisa. Kuna siku nimepewa lifti kwenye gari wamejaa familia nzima baba mama na mtoto wanatoka mjini, tumefika mahali kumbe Lori limeovertake halafu limeiva ghafla liko upande wetu,baba wa familia akatupeleka kwenye mtaro ndo ilikuwa ponapona yetu, ile siku sitasahau na yule dereva wa lile lori hata kama simjui sijawahi kumsamehe. Yaani ile siku wote tulikua tunafia pale pale na kigari chetu. Kinachoniuma yule dereva aliendelea na kazi na pengine hata amesababisha ajali na vifo huko alipo. Uzembe wa kiwango cha SGR.
 
Serikali ikitaka Hawa mbwa waende kufanya mitihani Darasani mnawatetea
Mkuu, mi sitetei kitu chochote kinacholea uzembe wa madereva. Halafu sio tu kufanya mtihani, sheria ziwe Kali kiasi kwamba anaetaka kufanya uzembe anajiuliza mara 100. Halafu teknolojia itumike, trafiki hawezi kuwepo kila mahali, ila teknolojia inaweza kuwepo kila mahali, ukiovertake kijinga tu adhabu inakusubiri. Bado usalama wa barabarani sisi tunatania
 
RIP marehemu na pole nying kwa majeruhi.
Hii week kumetokea ajali nying za mabus ya abiria.

NB: mm Huwa nakaa siti ya katikati .
Upande wa Dereva.
abadan sikaagi siti za mbele.

Hao Abiria wa mbele sijuo kama wametoka salama.

Basi unajiona mjanja mwenyewe!
 
Hawa maoondakta wangekuwa wanawekewa siti yao mbali na huo mlango, hata kama dereva kapoteza maisha utaona hapo ajali imeelemea upande mwingine maana yake ni kwamba alijaribu kujinusuru akapeleka kwa Kondakta.

Pale mbele ni hatari sana hata madereva wa akiba kwa maaafa marefu hawathubutu kukaa pale. Wanachukua kigodoro na kulala kwenye korido au kama siti zipo wanaenda zao kujilaza mwisho kabisa.

Makonda hawashtuki hilo
 
Back
Top Bottom