digba sowey
JF-Expert Member
- Mar 1, 2017
- 10,410
- 22,986
ðŸ˜ðŸ˜ðŸ˜
Ajali mbaya za basi la Isamilo linalofanya safari zake Mwanza-Dar kugongana uso kwa uso na basi la Libanika (Dar-Mwanza) iliyotokea alfajiri ya leo, kijiji cha Msembeta, kata ya Nala, wilaya ya Dodoma, mkoa wa Dodoma.
Kumekuwa na ripoti za vifo kadhaa na majeruhi wengi
Chanzo cha ajali ikiwa na mwendokasi wa basi la Isamilo (linatoka Mwanza kwenda Dar) , ku overtake lori kwenye mlima na likiwa kwenye kona kali, kulivamia basi la Libanika lililokuwa linatoka Dar kwenda Mwanza
Updates
=========================
Wamefariki watu 9 ikiwemo dereva, makondakta na abiria
Jumla ya majeruhi ni 66, 9 kati yao wameripotiwa kuwa katika hali mbaya na wanaendelea kupatiwa matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma
==========================
View attachment 3641954
View attachment 3641874View attachment 3641875View attachment 3641876
Kusoma siyo tatizo tatizo ni mamlaka zipo kimya kuwasimamia na kuwawajibishaInasikitisha sana, Ndo maana serikali imesema warudi shule kuwakomoa tu.
Ni sehemu nzuri kwa mawazo yetu binadamu lakini ya Mungu ni mengi.Ndo maana kuna baadhi ya watu wanapenda seat ya upande wa dereva.
Haya mapumbavu hata ukiwa Bagamoyo road kule Bunju,Boko yana vurugu kweli kujidai yana haraka wakati tayari wako Dar. Kuwachekea Hawa wapumbavu ndio sababu wanaua ndugu zetu kizembe.Haraka bila sababu ,kujiona kwamba wao ndio kipaumbele kwenye barabara hiyo ni shida kubwa. Njia nne ndio suluhisho kwa aina ya madereva wetu.
Kweli ya Mungu Mengi.Ni sehemu nzuri kwa mawazo yetu binadamu lakini ya Mungu ni mengi.
NB;Mmenifanya niwaze itakaa vipi kama abiria wote tukichagua upande mmoja na mwingine ukose abiria.Aiseee!
Yote hii ni shauri ya kutozingatia taaluma ya udereva. Una-overtake vipi kwenye mlima na uko mwendo kasi? Dereva lipungukiwa maarifa ya udereva! Ajali zinazotokana na ubovu wa gari ni chache mno, nyingi ni hizi za kusababishwa na binadamu.Ajali mbaya za basi la Isamilo linalofanya safari zake Mwanza-Dar kugongana uso kwa uso na basi la Libanika (Dar-Mwanza) iliyotokea alfajiri ya leo, kijiji cha Msembeta, kata ya Nala, wilaya ya Dodoma, mkoa wa Dodoma.
Kumekuwa na ripoti za vifo kadhaa na majeruhi wengi
Chanzo cha ajali ikiwa ni mwendokasi wa basi la Isamilo (linatoka Mwanza kwenda Dar) , ku overtake lori kwenye mlima na likiwa kwenye kona kali, kulivamia basi la Libanika lililokuwa linatoka Dar kwenda Mwanza
Updates
=========================
Wamefariki watu 9 ikiwemo dereva, makondakta na abiria
Jumla ya majeruhi ni 66 na 9 kati yao wameripotiwa kuwa katika hali mbaya na wanaendelea kupatiwa matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma
==========================
View attachment 3641954
View attachment 3641874View attachment 3641875
View attachment 3641983
View attachment 3641876
Poleni sana.Hii ajari imeondoka na brother masumbuko
Dereva wa gari la isamilo
Dah! Inauma sana kuona kifo kinakuja halafu huoni namna ya kukiepuka.dereva Kipindi anaiona ajali hii hapa alisikika Tu akisema "Watoto wangu jamani"