Aibu: Tundu Lissu adanganya tena

Aibu: Tundu Lissu adanganya tena

Hoja yangu kwa lisu JE WARAKA FEKI unatumika KUMUWAJIBISHA MTU........ so inamaana maamuzi yaliyotolewa na CC ya Mzee Mtei hayakuwa sahihi!!!!!!!!!! Sijajua lipi CHad..a Wamekusudia kwa ZZK mungu amuepushe yasimkute ya CHACHA WANGWE maana vijana kama D. Mallia wapo wengii....R.I.P CHACHA WANGWE.... damu yako haki yako itajulikana tu na Watanzania....
 
hoja yangu kwa lisu je waraka feki unatumika kumuwajibisha mtu........ So inamaana maamuzi yaliyotolewa na cc ya mzee mtei hayakuwa sahihi!!!!!!!!!! Sijajua lipi chad..a wamekusudia kwa zzk mungu amuepushe yasimkute ya chacha wangwe maana vijana kama d. Mallia wapo wengii....r.i.p chacha wangwe.... Damu yako haki yako itajulikana tu na watanzania....
wao ndio wenye orijino
 
Leo nimemsikia kitila akisema kwamba tunataka kuongozwa na wajinga
 
Zitto hana ubavu wa kuchezea vichwa za maelefu ya Watanzania wanaokiunga mkono chadema. Sauti ya wengi ni sauti ya Mungu. Mtu mmoja hawezi kushindana na nguvu za Mungu.

Muambieni akome kabisa, na wala hatuogopi kumtimuwa.
Kama sauti ya wengi ni sauti ya Mungu, basi CCM ndiyo yenyewe.
 
nyii wahuni wakubwa historio itawahukuma na njaa zenu hizo.wala hamtashiba kamwe hela zenye gharama ya kvuruga chama na Zito wenu mnapaswa kulaaniwa.Lecturer gani anaye hangaika na njaa kali ya uharibifu.huyo Kitilia aanzishe Chama chake aone kama atapata hata diwani mmoja Mbowe na Slaa wame hangaika mpaka.CDM imefikahapo.Wahuni sana nyie
 
kuku usiwe kama uharo wa kuku kishingo. Ameanza lini mie nimesema last time, sasa unajua ni lini ? Vyuo gani hivyo au evening classes ?

Acha uongo we kamanda! Lamwai anafundisha vyuo na anaishi vizuri tu! We akili yaki ndogo kama ya kuku!
 
Eti wanadai ule waraka alioukiri Kitila ni feki! Na kwamba baada ya kikao kijacho wakilazimika kuutoa ule orijino watafanya hivyo!
My take: chadema mtamfanya Zito aseme ambayo hakutaka kuyasema!itakula kwenu!
Ili kukijenga chama inapaswa tuache unafiki, eti watu waogope kuchukua maamuzi sahihi kwa sababu ya kuogopa kuwa wakifanya hivyo mtu Fulani atasema mambo yatakayo waharibia huo ni ujinga, tuwaogope sana viongozi wa namna hii. kama kuna anachokifahamu aweke wazi na sio kuleta unafiki na uwoga usio na maana, hatuwezi kuendelea kuishi kwa kulindana kwa kufanya hivyo hatutakuwa na tofauti na ccm.
 
Hahahaha mie huwa nasema wale chadema sio chama cha siasa kile,kipo tu kuwapa watu unaarufu wa siasa uchwara basiiii,mbowe alisema anao ushahid bomu ya arusha lakn mpaka leo kaficha kengeza zake ndan ya miwani kimyaaaa,nAungana na nape kuwa wao ndo walioratbu mabomu yale
Poor cdm

Chuki zako kwa Mbowe na Cdm hazitalisaidia taifa kama kipo kuwapa watu umaarufu, basi achana nacho, ulitaka Mbowe atoe ushahidi kwa nani mbona mliambiwa muunde Tume huru ya kuchunguza na ndio ingekabidhiwa huo ushahidi...
 
Upuuzi huu sasa malumbano ya nini? Mwenzao kajishusha sasa kwa nini wasikae mezani wakayamaliza. Nahisi kuchukia sasa, sina upande kwani kukosoana si ajabu
 
Duh hawa jamaa hawana aibu. Wameamua kuukana waraka. Watanzania watambue waraka uliochapishwa ni huohuo, na tena waliugawa wenyewe na kuutuma JF bila kujua madhara yake. Sasa wameumbuka kwa mambo yaliyopo ndani na sasa wanatapatapa.


Tundu Lissu aliwadanganya wajumbe wa Kamati Kuu kuwa 'tukiwafukuza hawa chama kitakuwa imara mara kumi'.

Eti waraka wa kufanya mapinduzi. Mapinduzi kwenye chama cha siasa yanafanyikaje? Hili sakata limempunguzia heshima sana TL. Sasa Mnyika naye hata kwenye kikao hakuwepo ameingia kichwakichwa.


Waache kabisa wao wanafanya yakwao.
''Huo ni ugomvi wa baba na mama,wewe mtoto chukua jembe kalime''
 
Duh hawa jamaa hawana aibu. Wameamua kuukana waraka. Watanzania watambue waraka uliochapishwa ni huohuo, na tena waliugawa wenyewe na kuutuma JF bila kujua madhara yake. Sasa wameumbuka kwa mambo yaliyopo ndani na sasa wanatapatapa.

Tundu Lissu aliwadanganya wajumbe wa Kamati Kuu kuwa 'tukiwafukuza hawa chama kitakuwa imara mara kumi'.

Eti waraka wa kufanya mapinduzi. Mapinduzi kwenye chama cha siasa yanafanyikaje? Hili sakata limempunguzia heshima sana TL. Sasa Mnyika naye hata kwenye kikao hakuwepo ameingia kichwakichwa.



Tundu Lissu ni mfanyibiashara siku hizi sishangai sana kuona ameshindwa hata kutumia akili yake ya uwakili; mtu huhukumiwa baada ya kesi; sio unamhukumu halafu unamwambia jitetee!
 
Kawachezea kwalipi? Yaleyaliyo semwa kwenye ule waraka msipofanyia kazi shauriyenu.

Zito hakatai kufukuzwa.yupo tayari.anacho kataa yeye kesho na keshokutwa cdm ikiwa vipande vipande asilaumiwe yeye.

muda utasema.
 
Wanatuchanganya tu, angalia kwenye mkutano na waandishi wa habari jana John Mnyika anasema barua zinapelekwa kwa wahusika kujieleza ndani ya siku kumi na nne. Tundu Lisu anatuambia hao wamafukuzwa chamani wakati tunafahamu kuwa wamevuliwa tu vyeo walivyokuwa navyo. Nadhani hapa pana JAZBA mno kuliko BUSARA.
 
Upuuzi huu sasa malumbano ya nini? Mwenzao kajishusha sasa kwa nini wasikae mezani wakayamaliza. Nahisi kuchukia sasa, sina upande kwani kukosoana si ajabu
Ni yale yale ya Simba na Yanga, panapokuwa na amani Simba panakuwa na mgogoro Yanga hivo hivo panapokuwa na amani Yanga basi panakuwepo mgogoro Simba.
 
Back
Top Bottom