Ahsante sana Wakili Msomi Peter Kibatala

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,789
288,011
"Ahsante sana Askofu! Wamewaruhusu [watu] hatimaye [kuingia Mahakamani] baada ya jitihada kubwa. Tunaanza sasa kuendelea na Kesi, Tuombeeni - Peter Kibatala"

Ujumbe huo ni wa Wakili Msomi Peter Kibatala (pichani) ukionyesha kuwa zuio la Polisi na Mahakama kutaka watu wasiingie Mahakamani na kutokuingia na simu, sasa limeondolewa! Tunawapongenza wahusika kwa kusikia hitaji la wenye nchi. Tunapongeza pia hekima ya Jaji katika wakati huo mgumu kwake! Ajue kuwa tunamuombea! Pia, tunapongenza jitihada za Mawakili Wasomi wote waliosimama imara katika kutetea haki ya umma wa Watanzania wa kupata haki yao ya kufuatilia na kusikiliza Kesi ya Mbowe na wenzake.

Kwa namna ya pekee tunawapongeza na kuwashukuru wote waliopaza sauti kupitia mitandao ya kijamii wakiwemo walioshiriki kusambaza ujumbe wetu sisi Askofu. Kesi imeanza tena baada ya 'wingu zito' kuondoka! Mungu bado yupo katika Kiti chake cha Enzi!

Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula

BFFC04EA-19F6-4D67-B4AD-C5BB4CB4D899.jpeg
 
Back
Top Bottom