HANGAYA THE CHIEF
JF-Expert Member
- Sep 10, 2021
- 329
- 947
Wiki ya pili na tunaelekea wiki ya tatu saasa , masikio, macho na mioyo ya wana wa tanganyika yamegoma kuelewa, kupokea, au kusikia nyimbo, mapambio na kelele, maelekezo juu ya uwekezaji tata ulioambatana na mkataba tata wa DP world na mama JMT juu ya bandari za Tanganyika pekee zenye muundo muungano wa TAnzania bara na Tanzania visiwani.
swali kubwa sasa tunafanyaje sasa wakati mfalme kasha saini? na Bunge lao la JMT limesharidhia,? je tunazimaje kelele za watu nje? wapo wanaosema tuwaache huu ni upepo tu utapita, wapo wanaowaza funika kombe mwanaharamu apite, sisi tunendee kutekeleza jambo letu, wapo wanaosema, lakini upande wa pili pia wapo wanaosema, hatutanyamaza kamwe mpaka mpaka kieleweke,?
swali kubwa sasa tunafanyaje sasa wakati mfalme kasha saini? na Bunge lao la JMT limesharidhia,? je tunazimaje kelele za watu nje? wapo wanaosema tuwaache huu ni upepo tu utapita, wapo wanaowaza funika kombe mwanaharamu apite, sisi tunendee kutekeleza jambo letu, wapo wanaosema, lakini upande wa pili pia wapo wanaosema, hatutanyamaza kamwe mpaka mpaka kieleweke,?
lakini nani shujaa?
kwangu mimi, nimpongeze mtanganyika mwenzetu popote alipo apokee maua yake kwa kutoa zawadi kubwa kwa watanganyika wenzake, maana watawala na wataliwa wote wamezama kwenye mdahalo ambao chanzo chake hakijulikani, na hakuna hata aliyepinga kuwa mkataba huu ni fake, na wote tunarejea (nukuu zetu) ni kwenye mkataba huo huo. ni ishara wazi kuwa ndani ya serikali tuna wenzetu ambao ni wazalendo na hawapendi kuona ujinga ukitendeka, na ndio maana wamekuwa tayari kujitoa na kuonyesha wenzao nini kinaendelea katika nchi yao, kwa hiyo ni kazi yao na si yake tena.
napongeza sana juhudi za mwenzetu, na Mungu ampe maisha marefu, yeye na vizazi vyake vyote.
Mungu ibariki Tanganyika na watu wake wote.