Tetty
JF-Expert Member
- Jan 6, 2012
- 26,355
- 21,418
Tumuombe uzima na salama, maana mahabusu za polisi wetu na baadhi ya mbinu chafu za mahojiano, Mungu bariki Rwakatare sio tuu ni public fugure, bali pia anazijua hakizake mikononi mwa polisi!, angekuwa ni mwenzangu za mimi, saa hizi angekuwa umekwisha sema kila kitu!.
Pamoja na yote, mimi nimeiangalia clip ile na kujiridhisha ni "bonafide genuine!".
Pasco.
Kaka,mie ambaye siyo mwandishi wa habari wala mtu wa IT nimeiona clip hiyo kuwa ni fake kwa kupitiliza.Hivi huyo Lwakatare alikuwa anaongea mwenyewe?Pili yule binti aliye vaa pink hakuwataka kujua kinachoongelewa ilhali anaongea kwa sauti?Tatu aliokuwa anaongea nao mbona hawaonekani kwenye clip?Watanzania tusiwe wepesi wakunyoosha vidole kwa wenzetu tuwe wepesi pia wakufikiri nje ya kona.Na ninaamini hata hiyo CD anayosema Mwigulu anayo nayo itakuwa kiini macho,hasa ikitolewa leo.Hivi inakuingia akilini mtu alete suala zito kama hili kwenye mtandao aache kupeleka polisi kwanza?Tafadhali tumuogope mungu kwanza,serikali yetu na wale tuliowapa uongozi hawatutendei haki?Hainiingii akilini mpaka polisi aione clip kwenye mtandao ndio amkamate mtuhumiwa?Kwa kweli ni uongo usiopimika tuache siasa chafu jamani zitagharimu maisha yetu.Kinachofuatia ni kulipizana kisasi,tuache ni tabia isiyopendeza.