KESI YA MFANYABIASHARA BASIL AENDELEA KUSOTA BUTIMBA
Kesi inayomkabili Mfanyabiashara na mmiliki wa kiwanda cha kutengeneza nyavu cha Nyamagara Fishing LTD cha jijini Dar es salaam, Basil Kyando, imehairishwa kufuatia wadau muhimu katika kesi hiyo kutofika mahakamani.
Kesi hiyo namba 10606 ya mwaka 2026 ilipelekwa na serikali ya Tanzania wakimtuhumu mfanyabiashara huyo kujipatia shilingi zaidi ya bilioni 1 kwa biashara ya utengenezaji wa nyavu za uvuvi.
Kesi hiyo ya uhujumu uchumi, ipo kwa hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama ya hakimu mkazi Mwanza, Erick Marley.
Akizungumza nje ya mahakama hiyo, Wakili wa upande wa utetezi, Elphace Rweshabua, amesema sababu zilizosababisha kesi hiyo kutosikilizwa imetokana na wadau muhimu katika kesi hiyo kushindwa kufika mahakamani na kupangiwa terehe nyingine.
Inaelezwa kuwa mfanyabiashara huyo anayefahamika kwa jina la Basil Daud Kyando, alikamatwa Aprili 30 mwaka huu na watu waliojitambulisha kuwa ni askari Polisi, akiwa dukani kwake.
Pamoja na kumkamata maafisa hao walichukua shehena kubwa ya nyavu ambazo zilikuwa dukani na kuondoka nazo na mpaka sasa hazijulikani zilipo.
Hata hivyo inaelezwa kuwa baada ya kumkamata Mfanyabiashara huyo alifichwa kwenye nyumba moja ya TAFICO jijini Dar Es salaam na kukaa hapo kwa siku mbili.
Wakili wa mshtakiwa huyo, Elphace, anasema kukwamatwa na kufikishwa mahakamani kwa Mfanyabiashara huyo, anafafanua kuwa Aprili 4 mwaka huu, maafisa hao kwa kushirikiana na askari polisi walimsafirisha kwenda jijini Mwanza.
Kabla ya kufikishwa Mwanza walifikia mkoani Singida katika kituo kimoja cha mafuta (jina linahifadhiwa)baada ya siku moja iliyofuata Aprili 5 mwaka huu,alisafirishwa mpaka jijini Mwanza na kupelekwa eneo la Igogo kwenye meli ya New Mv. Mwanza na kuwekwa hapo kwa siku tatu.
Baada ya kukaa kwenye meli hiyo kwa siku tatu, Mei 5, mwaka huu alipelekwa kituo kikuu cha Polisi kwa ajili ya mahojiano.
Kufikishwa kwa mara ya kwanza katika kituo kikuu cha Polisi jijini Mwanza, ndipo ndugu zake walipata taarifa na kuomba ndugu yao afikishwe mahakamani kwa ajili ya kusomewa tuhuma zinazomkabili.
Jeshi la Polisi mkoa wa Mwanza liliwaeleza ndugu wa Mfanyabiashara huyo kuwa watamfikishwa Mahakama kuu mei 18 mwaka huu, hata hivyo kabla ya tarehe hiyo Polisi walimfikisha mahakama ya mkoa wa Mwanza Mei 15 kitendo ambacho kinazua wasiwasi kuhusiana na kesi hiyo.
Kwa mjibu wa Wakili wa mshtakiwa anaeleza kuwa mfanyabiashara huyo baada ya kufikishwa mahakamani alisomewa kesi ya utakatishaji fedha namba 10606 ya mwaka 2026 ambayo haina dhamana.
Kesi hiyo itatajwa mahakamani hapo Juni 22 kwa ajili ya kupitia maombi ya mteja huyo ili kumaliza kesi nje ya Mahakama.
Kesi inayomkabili Mfanyabiashara na mmiliki wa kiwanda cha kutengeneza nyavu cha Nyamagara Fishing LTD cha jijini Dar es salaam, Basil Kyando, imehairishwa kufuatia wadau muhimu katika kesi hiyo kutofika mahakamani.
Kesi hiyo namba 10606 ya mwaka 2026 ilipelekwa na serikali ya Tanzania wakimtuhumu mfanyabiashara huyo kujipatia shilingi zaidi ya bilioni 1 kwa biashara ya utengenezaji wa nyavu za uvuvi.
Kesi hiyo ya uhujumu uchumi, ipo kwa hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama ya hakimu mkazi Mwanza, Erick Marley.
Akizungumza nje ya mahakama hiyo, Wakili wa upande wa utetezi, Elphace Rweshabua, amesema sababu zilizosababisha kesi hiyo kutosikilizwa imetokana na wadau muhimu katika kesi hiyo kushindwa kufika mahakamani na kupangiwa terehe nyingine.
Inaelezwa kuwa mfanyabiashara huyo anayefahamika kwa jina la Basil Daud Kyando, alikamatwa Aprili 30 mwaka huu na watu waliojitambulisha kuwa ni askari Polisi, akiwa dukani kwake.
Pamoja na kumkamata maafisa hao walichukua shehena kubwa ya nyavu ambazo zilikuwa dukani na kuondoka nazo na mpaka sasa hazijulikani zilipo.
Hata hivyo inaelezwa kuwa baada ya kumkamata Mfanyabiashara huyo alifichwa kwenye nyumba moja ya TAFICO jijini Dar Es salaam na kukaa hapo kwa siku mbili.
Wakili wa mshtakiwa huyo, Elphace, anasema kukwamatwa na kufikishwa mahakamani kwa Mfanyabiashara huyo, anafafanua kuwa Aprili 4 mwaka huu, maafisa hao kwa kushirikiana na askari polisi walimsafirisha kwenda jijini Mwanza.
Kabla ya kufikishwa Mwanza walifikia mkoani Singida katika kituo kimoja cha mafuta (jina linahifadhiwa)baada ya siku moja iliyofuata Aprili 5 mwaka huu,alisafirishwa mpaka jijini Mwanza na kupelekwa eneo la Igogo kwenye meli ya New Mv. Mwanza na kuwekwa hapo kwa siku tatu.
Baada ya kukaa kwenye meli hiyo kwa siku tatu, Mei 5, mwaka huu alipelekwa kituo kikuu cha Polisi kwa ajili ya mahojiano.
Kufikishwa kwa mara ya kwanza katika kituo kikuu cha Polisi jijini Mwanza, ndipo ndugu zake walipata taarifa na kuomba ndugu yao afikishwe mahakamani kwa ajili ya kusomewa tuhuma zinazomkabili.
Jeshi la Polisi mkoa wa Mwanza liliwaeleza ndugu wa Mfanyabiashara huyo kuwa watamfikishwa Mahakama kuu mei 18 mwaka huu, hata hivyo kabla ya tarehe hiyo Polisi walimfikisha mahakama ya mkoa wa Mwanza Mei 15 kitendo ambacho kinazua wasiwasi kuhusiana na kesi hiyo.
Kwa mjibu wa Wakili wa mshtakiwa anaeleza kuwa mfanyabiashara huyo baada ya kufikishwa mahakamani alisomewa kesi ya utakatishaji fedha namba 10606 ya mwaka 2026 ambayo haina dhamana.
Kesi hiyo itatajwa mahakamani hapo Juni 22 kwa ajili ya kupitia maombi ya mteja huyo ili kumaliza kesi nje ya Mahakama.